Urgent!...ushauri unahitajika kuninusuru

Urgent!...ushauri unahitajika kuninusuru

wanajamvi mi kijana mwenye umri wa miaka 23,kwa sasa ni mwanachuo hapa udsm.nimekuwa na mahusiano na dada mmoja ambaye nimepanga kumuoa aje awe mke halali.mdada huyu ye ni mwalim wa secondary huko mkoani,kabla ya mi kurudi huku dar chuoni nilikuwa naye kwa mda fulan ka week mbili hivi.lakini baada ya mi kuwa nimeondoka watu anaoishi nao wanasema amebadirika kkiasi cha wao kutokumwelewa vizuri!amekuwa akiomba ruhusa za mara kwa mara kwend mjini bila reason maalum,alaf kunatuhuma zngine nyingi tu ambazo yeye amezkana kabisa...hivi sasa mpaka naandika uzi huu yeye hayupo tena kituon amesafiri kwenda kumwona mamake.ila kabla ya kusafiri alinijulisha anakwenda tu nyumban na nilipomuuliza anaenda kufanyeje akasema anataka akaonane na babake aliyeko mwanza...ila jana kabadili na kunieleza anaenda kumwona mamake-mzee na mama hawaishi pamoja.inasemekana kutoka vyanzo vya uhakika kuwa amekuwa na uhusiano hivi karibun na mwalim fulan aliyekuja hapo shulen kwao ksimamia mtihani wa kidato cha nne......jamani nishaurini nifanyeje!? kwa sababu kila nikimuuliza anakataa na kusema haiwez ikatokea hivyo hata siku moja....msinikejeli kwa kuwa hiz ni changamoto za maisha ndani ya mapenz.naomba kuwasilisha uzi huu kwaajili ya msaada wenu tafadhari...

Nakushauri fanya uchunguzi wako wa kina na utafahamu kama huyo dada anakucheat au vipi. kama unataka kujua umchunguzeje ni pm ntakufundisha, im serious!!
 
Nenda darasani! Acha ujinga
23 yrs bado mdogo sana
saka elimu chaliiii
au mpaka wale kichwa ndo akili atakaa sawa,

huyo si saizi yako, hesabu hapo umalize chuo utafute ajira ( approx 3yrs) ndo unapata ajira, atakuwa anakusubiri ww?

Au unafikiri naniliu yako ni almas, POLE SANA
 
Achana na habari za kumfuatilia kwa sasa, komaa na kitabu utaliwa kichwa shauri yako.
 
23 yrs bado mdogo sana
saka elimu chaliiii
au mpaka wale kichwa ndo akili atakaa sawa,

huyo si saizi yako, hesabu hapo umalize chuo utafute ajira ( approx 3yrs) ndo unapata ajira, atakuwa anakusubiri ww?

Au unafikiri naniliu yako ni almas, POLE SANA
Kweli kabisa jamaa ni kijana mdogo sana kuanza kumfikiria huyo mwanamke, akomae na kitabu kwa sasa.
 
duh!! naona sasa itabidi tuwaambia nyie watu kuwa viboko kuwa long distance relationships never work!!! msidanganyike na hao wazungu na vi article vyao vya jinsi ya kumanage long distance relationship...full uzushi tuu.
hesabu hasara mwana na endelea kukamatia magoma hapa jijini.
 
Nakushauri fanya uchunguzi wako wa kina na utafahamu kama huyo dada anakucheat au vipi. kama unataka kujua umchunguzeje ni pm ntakufundisha, im serious!!

ka vp ncheki kwa cm yangu 0753914344&0682800341 au vp bro?
 
Naunga mkono, aendelee na uchunguzi. Mapenzi ni kama kikohozi, huwa hayafichi ipo siku atagundua!

hiyo ni kweli kaka,tatizo ni kuwa palikuwa vilevile na ushindani kati yangu na mkuu wa shule ile sote tulirusha nyanga zetu ila mie nkapata....labda anawatumia hao walim wenzake kuniraghai ili apate chance ya kuingia kirahisi...cwez kujua kwa kuwa sasa hivi nipo chuoni tena mwaka wa pili sasa!
 
Kweli kabisa jamaa ni kijana mdogo sana kuanza kumfikiria huyo mwanamke, akomae na kitabu kwa sasa.

mie npo mwaka wa pili sasa manake mwaka 2014 naua bendi kaka wala cyo kwamba ndo naanza ila yote kumi mjomba dem mkali na ananipa nisichonacho....kwa wengine cwez kaka maana niliaswa kaumpenda mmoja!
 
23 yrs bado mdogo sana
saka elimu chaliiii
au mpaka wale kichwa ndo akili atakaa sawa,

huyo si saizi yako, hesabu hapo umalize chuo utafute ajira ( approx 3yrs) ndo unapata ajira, atakuwa anakusubiri ww?

Au unafikiri naniliu yako ni almas, POLE SANA

love is blind man!.....waweza hata kupenda kkongwe ka pico.i think i've the chance to win the game.....i need your advice to makae me firm!
 
Usimkimbize mwizi kwa makelele
Mkimbize kimya kimya

Afu mbona chuo warembo kibao?
Mkuu Kongosho hapo kwenye RED...Kupenda ni kubaya sana warembo wa chuo sio issue yeye alishaweka moyo wake huko....
 
Last edited by a moderator:
mwana wala ucjali,GPA yangu inasoma 4.2 nipo CASS!
GPA ya 4.2 enh?walikwambia huwa zinabaki hivo hivo hata ukifeli sio?uliza wenzio walioanza na GPA za 4.5 wakamaliza na 1.2 ?chezeya kuwekeza kimoyomoyo!
soma kijana kama hyo binti unahisi sio mwaminifu we piga zako shule u still have a lot to learn kwenye haya maisha!usipoangalia hiyo GPA itabaki kwenye kuwa phrase tu " NILIKUWAGA MKALI MIE CHUO BASI TU!''
 
Naunga mkono hoja!
Ni bora kufanya uchunguzi ili kujua ukweli na kuweza kufanya maamuzi yaliyo sahihi, usitegemee kufanya maamuzi kwa kusikia kwa mtu ni bora ukapata uhakika wewe mwenyewe!
calm down......

fanya uchunguzi kimya kimya... saa nyingine si kila unaloambiwa / unalosikia ni la kweli au likutie presha...

mfano ukifunga chuo unaweza kwenda kufanya uchunguzi, na angalia mwendo wa mwenzio, amebadilika nk


 
Pole kijana, ni mapema sana umejingiza katika commitments kubwa kiasi hicho. Naungana na wadau kwamba piga shule kwanza, usiwe na presha. Ukipata kazi yako utawaona wengi tu ambao wako tayari kujenga mji. Wengi waliokuwa na mahusiano ya kimapenzi vyuoni mara tu baada ya shule na mapenzi yalikwisha. Piga moyo konde kijana, wewe ni mwanamme, mbegu zinazalishwa kila siku tofauti na mwananmke ambaye ana muda maalumu wa kutoa mayai.
 
Back
Top Bottom