Urasimu wa NIDA, vitambulisho vya Taifa

Urasimu wa NIDA, vitambulisho vya Taifa

PLAN B

Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
30
Reaction score
6
Wana jamvi,

Mamlaka ya iliyopewa dhamana ya kuratibu mchakato wa vitambilisho vya taifa imeonesha udhaifu mkubwa sana na urasimu wa hali ya juu.

Kwanza,utoaji wa ajira za muda mfupi kwa vijana wanaohusika na upigaji picha.NIDA wametoa ujira kwa usiri mkubwa sana na kwa taarifa za kuaminika ni kwamba ajira zimetolewa kwa kujuana wakati wapo vijana waliomaliza vyuo vikuu nchini hawana kazi ya kufanya.

Na wale waliopo hawakidhi vigezo kwani wanafanya kazi taratibu sana ivo kuweka foleni kubwa sana sehemu za kupigia picha.

Pili,kuna wananchi ambao majina yao hayapo kwenye mbao za matangazo mfano kata ya Kijichi wilaya ya Temeke majina ya watu hayaonekani na hakuna jibu lilotolewa la kuridhisha wananchi.

tatu,kuna wananchi wa jiji la Dar es Salaam ambao hawakuwepo kipindi cha kujiandikisha mwaka jana kwa minajili kuwa walisafiri na kwa muda huu wapo DSM lakini NIDA wameshindwa kutoa utaratibu kuhusu suala ili.

NINAOMBA NIDA NA WANABODI WOTE WENYE MAELEZO YA KUTOSHA KUHUSU SUALA HILI WAWEZE KULITOLEA UFAFANUZI.
 
Bora useme wewe ....Mimi nI mmoja wapo jina langu halipo halafu wananiuliza eti ulijiandikisha hapa?...WTF ....wakati me ni mzawa zaidi ya miaka 20 hapo....nitakua mjinga nikatafute jina langu wkt sikuandikisha...huu ni upuuzi na uzembe wa NIDA...sielew hatma yangu coz hata hao serikali ya mtaa hawana majibu...upumbavu kabisa
 
Hapohapo kuna walijiandikisha mwaka jana wakiwa DAR na sasa wamerudi kwenye maeneo yao ya kazi kama KIGOMA, MWANZA na kwingineko, je watapiga picha lini na kuchukua vitambulisho vyao, ushauri wangefanya kama NEC tu.
 
Bora useme wewe ....Mimi
nI mmoja wapo jina langu halipo halafu wananiuliza eti ulijiandikisha
hapa?...WTF ....wakati me ni mzawa zaidi ya miaka 20 hapo....nitakua
mjinga nikatafute jina langu wkt sikuandikisha...huu ni upuuzi na uzembe
wa NIDA...sielew hatma yangu coz hata hao serikali ya mtaa hawana
majibu...upumbavu kabisa

nyie si ndo mligoma wakati ule kujiandikisha? majina yenu hayamo mnaanza kulalamika
 
Una uhakika na uloonge mpuuzi wewe....au ili mradi unacomment uonekane nigome kwa kisa gani...km huna la kushauri kaa kimya...tunajua humu NIDA wapo na watatupa majibu ya nn cha kufanya...SAWA
 
NIDA wangekuwa na utaratibu wa kufanya kazi zote kwa muda mmoja, Yaani kazi ya kuandikisha kupiga picha na kuchukua alama za vidole. Hii ingesaidia sana kuondoa usumbufu wa majina kukosekana kama ilivyo sasa. Ikiwa ni pamoja na kutotoa mwanya wa wale wanaojiandikisha halfu wanahama na kusubiri kuanza zoezi upya tena.

Ni bora kuhudumia watu wachache kwa siku lakini ukawa na ufanisi katika utendaji.
 
Serikali hii katika utendaji siku zote ni SIFURI. Haijawahi kufanya jambo lolote lile likakamilika kwa mafanikio makubwa, siku zote kunakuwa na dosari tena kubwa sana. Zoezi la kuhesabu watu walichemsha vibaya sana hili la vitambulisho vya Taifa nalo wamejikanyaga kupita kiasi, lakini kamwe huwezi kusikia wakisema utendaji wao si wa kuridhisha kabisa. Ni majanga ya Taifa kila leo!!!!
 
Kama kawaida hapa Tz inapotokea fursa wajanja hutumia hiyo Mianya kujinufaisha hapo kwenye ajila tayari wajanja wamepenyeza watu wao tena pengine kwa Rushwa mbali mbali si unajua tena kufa kufaana hivyo ufanisi itakuwa issue kwani hata Mashirika ya Umma mengi yalikufa kwa Sababu ya Undugu urafiki uhawara kutawala ktk ajila Matokeo yake utendaji ukawa hauna Tija kwa kukosa ujasiri wa kukemea maovu
 
Hawa NIDA wanafanya kazi kwa mazoea kwani ofisi zao za Wilaya ya Temeke zilizopo Kigamboni muda wote zimefungwa ila ukienda na gari ndo unaruhusiwa kuingia make kwa sisi wananchi wa kawaida haurusiwi kwenda pale hata kuulizia masuala ya utendaji wao wa kazi na kuhusu mapungufu yaliyopo kwa wananchi kutoona majina yao.NIDA inabidi wajipange upya bila ivo watatuletea majanga tupu.
 
Ni vema NIDA wakatoa tamko juu ya idadi ya walioandikishwa ikilinganishwa na uwiano wa takwimu za sensa. Pia waeleze mikakati iliyopo juu ya wale ambao kwa sababu moja au nyingine hawakuweza kujiandikisha hapo awali
 
Hapohapo kuna walijiandikisha mwaka jana wakiwa DAR na sasa wamerudi kwenye maeneo yao ya kazi kama KIGOMA, MWANZA na kwingineko, je watapiga picha lini na kuchukua vitambulisho vyao, ushauri wangefanya kama NEC tu.

1. nina case kama hii kwa mwandani wangu, alijiandikisha akiwa dar lkn kwa sasa yuko mkoani kikazi; kwa mujibu wa ufafanuzi niliopewa na afisa wa nida sehemu nilipojiandikishia ni kwamba, kuna vituo maalumu vitakavyokuwa vina adress hizo cases (kama sikosei ni kiwilaya), naamini NIDA wamejipanga kwa hili.

2. tusaidie zoezi hili likamilike kwa ufanisi mkubwa, kwani through huu mfumo ni rahisi kuwang'amua M23 na manyang'au wanaoishi nchini kinyemela na wale walionunua pasi za kusafiria za tanzania, vyeti vya kuzaliwa, voting IDs etc.

Kituo nilichochukuliwa finger prints, muhudumu aliniambia kwa wiki ile moja tu walishakama pasi 3 za kusafiria ambazo jamaa waliletewa mkononi bila kwenda immigration! ... namna hii M23 watashindwa kweli kunua passport zetu na kuzitumia ki-propaganda?? so saddening!
 
Vitambulisho vinatolewa kwa watu wa makundi maalum, na manyapara
 
Kupata kitambulisho sasa hivi ni tizi, unaenda na kila kitu uhamiaji wakiona umekamilisha unaambiwa ukahojiwe ofisi za ccm 😂 wacha nikakae na makabrasha yangu bana, ikifika siku ya kupelekwa kwetu watanichagulia nchi ya kunipeleka 😢
 
Hili suala kwa tabia za kitanzania ni mpaka mh rais aongee si vinginevyo hiyo ndiyo Tanzania
 
Jamani hv ile namba ya kujua namba yako ya kitambulisho unakatwa 100 ni ngapi vileeee??!
 
NIDA ni janga, tunaomba TISS waingie ofisi ya Mwanza kuna vituko vingi, rushwa hadi kuomba kupewa status ya application yako.
 
Back
Top Bottom