TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,866
- 5,742
Ndoto ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi , maarufu kwa jina la UKAWA , ya kutaka kusimamisha mgombea mmoja wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , inaweza isifanikiwe kutokana na msuguano wa chini unaoendelea ndani ya vyama vikuu viwili vinavyounda umoja huo; Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na chama cha Wananchi(CUF).Habari za uhakika zilizopatikana kutoka katika duru za siasa za vyama hivyo viwili zinaeleza kwamba wakati viongozi wakuu wa CHADEMA wanataka kutumia mbinu ya Mwai Kibaki wa Kenya , iliyomuwezesha kukiondoa madarakani chama kilichoipatia uhuru nchi hiyo cha KANU mwaka 2002 kwa kutumia muungano wa wanasiasa muhimu katika siasa za Kenya uliopewa jina la NARC , baadhi ya viongozi na wanachama wa CUF wameeleza kushtushwa na mbinu hiyo.
Kwa mujibu wa habari hizo, viongozi wa na wanachama wa hao wa CUF, wameeleza mbinu hiyo ya viongozi wa CHadema kwamba inalenga kukidhoofisha chama chama chao kwa upande wa Bara, hali ambayo wanasema hawawezi kukubali kuona Mwenyekiti wao Profesa Ibrahimu Lipumba akishawishika kwa namna yoyote ile kuacha kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupumbazwa na hicho kinachoitwa UKAWA.
Source: gazeti la TAZAMA Tanzania.
Kwa mujibu wa habari hizo, viongozi wa na wanachama wa hao wa CUF, wameeleza mbinu hiyo ya viongozi wa CHadema kwamba inalenga kukidhoofisha chama chama chao kwa upande wa Bara, hali ambayo wanasema hawawezi kukubali kuona Mwenyekiti wao Profesa Ibrahimu Lipumba akishawishika kwa namna yoyote ile kuacha kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupumbazwa na hicho kinachoitwa UKAWA.
Source: gazeti la TAZAMA Tanzania.