URAIS 2015: Wanawake kuvuruga mambo CCM

URAIS 2015: Wanawake kuvuruga mambo CCM

2mbaku

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2010
Posts
316
Reaction score
67
HARAKATI za urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimeingia katika hatua mpya baada ya kuvuja kwa taarifa za kuwapo mkakati wa kuwapa nafasi wanasiasa wanawake na kuwatosa wanaume kwa kile kinachodaiwa kuvunja makundi yenye uhasama.Habari za ndani ya makundi makuu ya wataka urais ndani ya CCM, zimethibitisha kuwapo taharuki kubwa miongoni mwao baada ya taarifa za wanawake kupewa nafasi kubwa kuzidi kushika kasi siku zinavyozidi kwenda.


Wataka urais wanaolengwa kuzimwa ni pamoja na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa, Edward Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Wanawake wanaotajwa kufanikisha mpango huu ni Dk. Mary Nagu, Prof. Anna Tibaijuka na Dk. Asha Migiro ambao wote watasukumwa na makundi yenye fedha nyingi ili angalao wawili kati yao waingie hatua ya mwisho.

Kutokana na nguvu ya CHADEMA na kile kinachoonekana kwa wana CCM wenye ushawishi mkubwa kuogopana kwa sababu mbalimbali, kuna mkakati wa kuwa na 'plan B' ya kusimamisha wanawake, mkakati kama uliotumika kumzima aliyekuwa Spika wa Bunge, Samwel Sitta.

Source: Tanzania Daima
Kazi kwelikweli! Je hii plan B itafaulu?
 
Kama ni mwanamke awe Prof Tibaijuka pekeyake ndio ataweza kupasuana vichwa na vichaa waliojaa hapa tanzania la sivyo hao wengine bado sana hawajakomaa kupambana na vichaa hawa na serikali hovyo hii!mtawapasua vichwa bure
 
Hapo ndiyo CCM itakufa KIBUDU bila kuchinjwa kwanini huo mwaka kwa plan B bora wasimamishe mgombea yoyote.Ukweli Vyama vya upinzani vina nafasi nzuri kwenda IKULU.
 
Mbele ya Dr. Slaa, Prof. Tibaijuka hana jipya na siyo mtendaji mzuri kihivyo. CDM jiimarisheni, Mungu anaweza kutusaidia watanzania
 
Yani yeyote watakeyemsimamisha lazima CDM tuchuke nchi, acha tu waendelee kutapatapa!
 
Kuna siku nilikuwa nasafiri njiani abiria mwenzangu baada ya kumdodosa alinijuza juu ya Plann B hiyo na chaguo hasa atakuwa ni Prof. Anna Tibaijuka.

Vigezo alivyonijuza mshikadau ni kama vilovyoelezwa na Tanzania Daima,

Moja, kuvunja makundi ndani ya CCM.

Pili, kukabiliana na nguvu ya CDM ambayo dhahiri imeonyesha kutaka kuitwaa Ikulu. The only way ni kutumia mwanamke na wanawake wengi watahamasika kupigia kura mwanamke mwenzao na kwa mtindo huo CDM itakabiliwa na upinzani mkali na hatimaye kushindwa.
 
Mbele ya Dr. Slaa, Prof. Tibaijuka hana jipya na siyo mtendaji mzuri kihivyo. CDM jiimarisheni, Mungu anaweza kutusaidia watanzania

Kumbuka itakuwa vita ya jinsia, wanawake wataaminishwa wakiwezeshwa wanaweza. Sasa sijui kama njia hii itafanya kazi.
 
Ngoja tusubiri nini kitatokea hapo mika miwili ilyobakia.
 
Kwanza hakuna ushahidi based on utafiti uliofanywa kuwa wanawake wanapendelea kuchagua wanawake wenzao kwenye nafasi za uongozi and suprisingly, it may be quite the opposite.

Pili, sijaona mwanamke kati ya wanaotajwa amegusa maisha ya wanawake wenyewe na jamii kwa ujumla katika utendaji kazi. An impressive track record would have been a bait.

Tatu, tumekuwa na viongozi wanawake katika ngazi mbali mbali ikiwemo za juu kabisa za uwaziri, uspika tz, uspika afrika, unaibu katibu UN n.k. Nini tunaweza kujivunia kwa hawa wanawake zaidi ya sifa za kisiasa tu? Pointi hapa ni kwamba walipewa nafasi kubwa lakini bado walishindwa kuonesha uwezo wao kwa kiwango cha juu hadi kufaa kufikiriwa kwa nafasi ya Urais.
 
Duu naona washasahau kilichowakuta arusha walitumia propaganda hi hi,kama wakiweka mwanamke hawa magmba cdm mbn njia nyeupe ikulu,plan d ya baba mwanaasha itawashangaza weng maana kama co kilaza mwanaasha basi itakuwa yule maza alyesababsha babu seya awe jela.tym wl tel tusubri hii ndo tanzania bana nchi iyowezekana kutokea kitu chochote wakat wowote.PEACE
 
HARAKATI za urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimeingia katika hatua mpya baada ya kuvuja kwa taarifa za kuwapo mkakati wa kuwapa nafasi wanasiasa wanawake na kuwatosa wanaume kwa kile kinachodaiwa kuvunja makundi yenye uhasama.Habari za ndani ya makundi makuu ya wataka urais ndani ya CCM, zimethibitisha kuwapo taharuki kubwa miongoni mwao baada ya taarifa za wanawake kupewa nafasi kubwa kuzidi kushika kasi siku zinavyozidi kwenda.


Wataka urais wanaolengwa kuzimwa ni pamoja na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa, Edward Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Wanawake wanaotajwa kufanikisha mpango huu ni Dk. Mary Nagu, Prof. Anna Tibaijuka na Dk. Asha Migiro ambao wote watasukumwa na makundi yenye fedha nyingi ili angalao wawili kati yao waingie hatua ya mwisho.

Kutokana na nguvu ya CHADEMA na kile kinachoonekana kwa wana CCM wenye ushawishi mkubwa kuogopana kwa sababu mbalimbali, kuna mkakati wa kuwa na 'plan B' ya kusimamisha wanawake, mkakati kama uliotumika kumzima aliyekuwa Spika wa Bunge, Samwel Sitta.

Source: Tanzania Daima
Kazi kwelikweli! Je hii plan B itafaulu?

:cheer2:Kuvuja kwa Pakacha (ccm) nafuu ya MCHUKUZI (CDM). Acha 2 waendelee kujikoroga, 2015 itayaweka bayana haya yote
 
Kama ni mwanamke awe Prof Tibaijuka pekeyake ndio ataweza kupasuana vichwa na vichaa waliojaa hapa tanzania la sivyo hao wengine bado sana hawajakomaa kupambana na vichaa hawa na serikali hovyo hii!mtawapasua vichwa bure

Huyu Mama anafagiliwa sana for Nothing!! Wizara hiyo ya Ardhi ni so demanding!! Simuoni anachokifanya!! Fikiria miji yote Tanzania inazidi Kuwa squatter Yeye anadhamana na Hana Plan b"" Kuna maeneo ambayo anaweza Hata kuwahi na kuweka becons kuzuia maeneo ya barabara, Just to deploy surveyors na kuwapa watu awareness ya kujua umuhimu wa kuwa na barabara za Mitaa!! Yeye amekalia kulita mambo makubwa! Adress without Haya Madogo!! Poor on her!! Shallow minded!!
 
Toka nimeanza kusikia majina ya viongozi wanawake kwenye hili taifa sijaona aliye strong wa
kusema anaweza kubeba vichwa vya watanzania.Kama wengine wamepewa favor mpaka umoja
wa mataifa na wameshindwa.Hii nchi ilipofikishwa kwa sasa inahitaji rais ambae kweli anadhamira
ya dhati ya kuleta mabadiliko,kitu ambacho hao wanawake wamefeli wote.
 
Mkuu REMSA makinda amefanya lipi la ziada kumshinda tiba la kupigiwa mfano?hayo usemayo ni upepo tu and as usual utapita.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu REMSA makinda amefanya lipi la ziada kumshinda tiba la kupigiwa mfano?hayo usemayo ni upepo tu and as usual utapita....

Hapa hakuna cha Makinda wala Tiba wala huyo aliyetoka kwa mzee Ban,wote wachemfu tu,huyo
Makinda ameweza nini anaongoza Bunge utafikiri anaongoza familia yake!?wakati anaongoza vichwa
akina Mnyika.
 
Wana bodi

CCM ikimsimamisha mmoja wa makundi haya, itashindwa kabla ya saa 4 siku ya kupiga kura 2015:
-Mzanzibari
-Mwanamke
-Fisadi Papa
-Asiyetoka Kaskazini

Mnisamehe kama mchango wangu unanuka udini, ukabila na ueneo. Nchi yetu imekaa vibaya kwa sasa, na mawazo yetu lazima yakae vibaya.
 
Hapa hakuna cha Makinda wala Tiba wala huyo aliyetoka kwa mzee Ban,wote wachemfu tu,huyo
Makinda ameweza nini anaongoza Bunge utafikiri anaongoza familia yake!?wakati anaongoza vichwa
akina Mnyika.

mtatokwa povu sana ila kama si tiba bac mama migiro tutamtuma subirin kusoma no. 2015
 
Back
Top Bottom