Urais 2015: UKAWA waanza safari

Urais 2015: UKAWA waanza safari

Leo unaskia watu fulani wenye nakisi ya uadilifu kwenye chama kilichoshindwa kwa Miongo zaidi ya 5(Nusu Karne) wanaibuka na kujifanya eti wao wana uwezo mkubwa sana wa kuliongoza kwa ufanisi taifa hili kwa kipindi hiki


Kama hatutatua suala la mfumo wetu mbovu ni ngumu kuleta mageuzi

Uchaguzi wa Mwaka ni uchaguzi wa njia ya mpito kuelekea mageuzi makuu ya kimfumo

Ni uchaguzi utakaoamua hatima ya Tanzania kama Mwanafamilia miongoni mwa familia kubwa ya kimataifa

Ni hatima ya vijana,akina Mama,wazee wa sasa na wa baadae wa taifa hili

Huu sio mwaka kufanya mchezo ule wa kutafuta kisafi katika jalala

Turudi katika misingi ya waasisi wa Taifa letu,tuangalie Dunia ambayo ni jamii pana inayoi-accomodate Tanzania inaelekea wapi

Tumepata nafasi mpya tena ya kistaarabu kufanya maamuzi.Hakuna atakayezuia maamuzi ya kuamua hatima yetu kama Umma wa Watanzania
Spot on,brother!
 
Nashangaa hujaizungumzia sera yake ya KUHALALISHA GONGO.
 
Alivyoomba ridhaa kwa Josephine alitekeleza yote...? Je kwa nchi ataweza kama ya Ufipa yanamshinda...z

Nafikir akiomba ridhaa kwa mama yako atatekeleza yote,ikiwa ni matatizo yote ya nyuma pamoja na ya mbele yatakayokuja.
 
Kura yangu na wengine wengi tutampa cha msingi ni kusimamia kura zetu zisichakachuliwe ili apewe ushindi wake.
Na sisi wananchi tuwe tayari kwa mabadiliko makubwa ya kimfumo yatakayotutoa hapa tulipo! Uwajibikaji kwa maana ya uchapa kazi kwa kila mtu uwe umeajiriwa au hukuajiriwa utaleta ufanisi mkubwa sana ktk uzalishaji kwa nchi yetu.
 
Teeh mkuu Majaar una hang over ya gongo...? Mbona umekuja kwa hasira au wewe ni Josephine
 
Tatizo la watz hatujajua vyema umuhimu wa nafasi hizi adimu za kuchagua viongozi!! Tunafuata zaidi mkumbo kama Kwereakwerea!! Tuko kama Mamba kusikia kwake hadi damu itoke sikioni!!

Kwa yanayoendelea Sasa nchini, hakuna hata mmoja leo angekuwa anafikria Kiongozi wa Taifa atoke CCM!! Watu badala wajadiri Uraisi kama taasisi wanajadili personal isues!! Hawako sirious!

DR. SLAA NDIE TUMAINI JIPYA LA TANZANIA MPYA!!
 
dr slaa atosha wengine wa nini wakati wamekaa nusu karne hamna jipya walilofanya
 
slaa akimrudishia mahimbo mke wake nitampa kura yangu
 
Unajua kuna watu wanashinda kujibishana kwa hoja wanaleta maswala ya mausiano towa hoja ya msingi kwann hafai kuwa kiongoz wa hii nchi sio blabla
 
umeandika ukweli ambao hata kamati kuu ya ccm inaujua na inaukubali , ubarikiwe sana .
 
Back
Top Bottom