Uraibu wa ngono

chiko

JF-Expert Member
Feb 24, 2010
580
245
Wanajamvi, Hube Someni;


Im a Recovering Sex Addict

Jennifer (not her real name), 36, lives in Miami. Although shes never touched drugs or alcohol, she has an addiction all the samesex addiction. Although not an official psychiatric diagnosis, Jennifers sex addiction has caused her tremendous pain and suffering over the years. Her compulsive behavior, which she thinks may have been triggered by childhood abuse, destroyed relationships and ultimately wrecked her marriage. She sought treatment and has been sober for six years.

You often hear stories about sex addicts who have multiple partners, or who have sex in parking lots, or hook up with strangers they meet on the Internet. That wasnt my style.
I had long affairs. I wanted sex, but I also wanted somebodys soul, in this really ego-driven way. My life was a constant juggling act of at least two men, making sure they didnt find out about each other. I was unfaithful to every boyfriend I ever had.

I thought that getting married would cure me. I hoped that I would never look at anyone else but my husband again. I remember praying the week of my wedding, God, please let me be faithful. Two weeks later, I started looking around. I got married in January 2000 and by April I was in a full-blown affair.

Overall, while I was married, I had two 2-year affairs with only a four-month break in between the affairs.

I felt like I got love from my husband, but as the intimacy level went up, my sex interest went down. My husband was really good-looking, nice, smart, funnyeverybody says hes such a great guybut because he was so familiar I was tired of him. Im just sort of wired wrong. Other women get turned on by a romantic date with their husbands. Me? I wanted to have sex if I had 10 minutes and there was a broom closet nearby. If we were in a fight and I wasnt sure if he was going to stay with me, thats when I felt really aroused. Ive spent the last six years trying to rewire my brain when it comes to sex.

Marriage didnt cure me
Were the same as heroin addicts; it just usually takes us longer to get caught because the symptoms arent as noticeable. You can tell when an employee is coming into work high or drunk, but its harder to identify sex addiction. Most of us are very productive and good at our jobs. Were compulsively efficient. Were clever, manipulative, and a little evil. I never touched drugs or alcohol; sex was my drug of choice. I thought I was better than other addicts. The truth is that I was not.

I got caught when my husband found a bunch of sex emails between me and my boyfriend. He Fed-Exed the emails to my grandmother, my parents, and my brother, saying, Im filing for divorce from Jennifer, and heres why. It was very clear through the emails that we were having a very sexual relationship. I said all sorts of things because it never occurred to me anyone else would read them. I remember telling my dad that I really loved my husband and wanted it to work. He said, Well, its hard to tell.

My husband confronted me and asked me over and over again, Why did you do this, why did you do this? I dont remember ever hearing the words sex addict before that moment, but they just popped out. I said, Because Im a sex addict! I remember thinking, I wonder if thats true? I was so used to lying that I would just say things like that. I went home and bought a book by Patrick Carnes, PhD, called Out of the Shadows, and I read it and realized it described me through and through.

After I got sober, my husband and I tried to make a go of it. We lasted another two and a half years before we got divorced. There was just too much damage done.

I will always be a recovering sex addict. Thats true of most sex addicts. We believe sex is the most important need, more important than food. If my partner says he doesnt want to be sexual with me, I read that as he doesnt love me. Its been hard to retrain myself to realize that it doesnt mean Im not worthy, but just that hes tired and has had a long day. Now when I have sex, Im present for it. Im there with the person that Im with. But its been really hard to reprogram my brain to think like that.


Kumbe sisi twafikiria hawa wenye kupenda sana..........wana pepo wa ngono, ama wamerogwa, tusiwachukulie vibaya kina INFIDELITY, Kumbe ni URAIBU(Yaani ADDICTION), Mateja wa ngono, kama vile wa madawa ya kulevya ambayo lazima mtu kuona mtaalam ama matibabu.

Ukiona umejaribu kila njia lakini mwenzio haridhiki, atoka hapo ni kama ana njaa ya miaka, jua..........
 
sas dawa yake nini mkubwa, tafuta na makala ya dawa ya hako kaugonjwa
 
Emotional Symptoms of Sex Addiction

If you or someone you love suffers from a sex addiction, you might not have healthy boundaries. If your husband is addicted to pornor sex, you may feel alienated, isolated, depressed, angry, or humiliated and need treatment yourself. If you are addicted to sex, you might become easily involved with people sexually or emotionally regardless of how well you know them, according to Sex and Love Addicts Anonymous. Because most sex addicts fear being abandoned, they might stay in relationships that aren’t healthy, or they may jump from relationship to relationship. When alone, they might feel empty or incomplete. They might also sexualize feelings like guilt, loneliness or fear.

Physical Symptoms of Sex Addiction

Although a sex addiction or pornography addiction can create many physical side effects, few physical symptoms of this disorder exist. However, the most common physical sex addict symptoms you might notice from having a sexual addiction is feeling immobilized due to sexual or emotional obsessions.

Effects of Sex Addiction

The effects of a sex addiction can be severe.

· According to Departmental Management of the USDA, about 38% of men and 45% of women with sex addictions have a venereal disease as a result of their behavior.

· Pregnancy is also a common side effect that can occur due to risky behavior. In one survey, nearly 70% of women with sex addictions reported they’d experienced at least one unwanted pregnancy as a result of their addiction.

Additionally, sex addiction likely has a negative impact on several areas of one’s life. It can lead to:

· A decline in personal relationships, social, and family engagement.

· Decreased concentration and productivity at work.

· Physical consequences like sexual dysfunction or sexually transmitted diseases (STDs).

It can have profound psychological effects, like generating feelings of shame, inadequacy, and emotional distress. It can lead to, or stem from, comorbid psychological disorders like:

· Anxiety.

· Depression.

· Substance abuse.

· Problems related to impulse control and emotion dysregulation.

· Obsessive-Compulsive type symptoms.

It is important to know that addressing co-occurring problems in one’s life, like depression, social anxiety, or social isolation, can make it easier to recover from sexual addiction.

Am I Addicted to Sex?

It is best to consult with a healthcare professional for proper evaluation of your sex addiction, however, you may also want to look out for the following signs:

· You feel powerless over how you act sexually.

· Your sexual choices are making your life unmanageable.

· You feel shame, embarrassment or even self-loathing over your sexual acts.

· You promise yourself you’ll change, but fail to keep those promises.

· You’re so preoccupied with sex it becomes like a ritual to you.

If you’re exhibiting any of these symptoms, it might be time to seek sex addiction treatment. If you also have a co-occurring substance addiction (e.g., alcohol, cocaine), call 1-888-481-5639 to learn more about treatment options.

Get Help For Sex Addiction

It is important to understand that although sex and porn addiction are not “formally” diagnosable, these conditions exist and often present with very adverse consequences and high levels of distress, guilt, and emotional turmoil.

If you can relate to the symptoms mentioned above, or know somebody who meets these criteria, do not hesitate to ask for help. Call +255 713 806 726 to speak to a treatment support specialist who can provide you with more information.
 
Uraibu wa kingono upo
Ni mwaka sasa tangu mwandaaji maarufu wa filamu duniani Harvey Weinstein alifanya maamuzi ya kwenda kwenye kituo maalumu cha kupambana na uraibu wa kingono.

Hii ni baada ya mfululizo wa shutuma za kuwadhulumu watu kingono, shutuma ambazo zilisababisha kukua kwa kampeni ya #Metoo iliyolenga waathirika wa ubakaji kuweka wazi yaliowasibu.

Mwandishi wa BBC Sangita Myska amekutana na watu wanao sema kuwa wamesumbuliwa na uraibu wa kingono ili kufahamu zaidi kama tatizo hilo lipo kweli, na kama lipo ni la aina gani.

Kazi ya kwanza ya Neila huko Uingereza baada ya kutoka katikati ya bara la Asia miaka 15 iliyopita, ilikuwa ni kwenye kampuni ya fedha ambayo ilikuwa imezungukwa na wanaume wababe kama asemavyo yeye kwamba walikuwa wanajipatia pauni milioni moja kama hela ya ziada.

Alikuwa ni mmoja kati ya wanawake wawili tu katika timu nzima, na wafanyakazi wenzao wakiume walikua wakiwachokoza kwa kucheza video za ngono kwenye televisheni kubwa ambazo zilitakiwa kuonyesha taarifa za masoko.

"Sikupenda lakini ilikuwa ndio mwanzo wa ajira kwangu iliyo nifungulia njia katika jiji. Ilinilipa vizuri na ilikua kazi ya kisasa na sikutaka kupoteza fursa hiyo," anasema.

"Nilijua wanaume wa ofisini walikua wakitaka niwajibu, walitaka kunishitua. Hivyo nilianza kwenda nyumbani na kuangalia video za ngono mwenyewe, hivyo ofisini sikushtuka tena. Kwa haraka nilibobea japo nilizaliwa katika familia yenye maadili makali ambapo ngono si jambo la kujadiliwa," anasema.

Kila siku alikuwa akifikiria atafikaje nyumbani kwa haraka ili achague filamu ya ngono na midoli yake ya ngono ili aaanze kujichua.

Hali hii huanza kidogo kidogo na baadhi ni kutokana na kutazama picha za ngono

Neila alimwelezea mwandishi wa BBC namna alivyokuwa anajiskia.

"Ilianza kidogo kidogo, hisia zinapanda sanaa. Na unaendelea kuangalia na kila mara unahamia kwenye vifaa vyako. Kila famamu zako zime sisimuka, unatazama kitu kinacho kufurahisha.Akili yako ipo mahali kwingine kabisa. Unajua haiwezi kuacha mpaka ubonyeze kitufe cha kusimamisha video. Unajua unasimamia mwenyewe raha yote unayoipata na inakufanya unafika kileleni namna ambayo binadamu hawezi kuku fikisha- na hasa mwanaume.

"Hali ya kujichua na kufika kileleni itakuchukua muda wa dakika tano mpaka kumi, lakini unarudi nyuma kwasababu hutaki kabisa kuiacha hiyo hali, ambayo ni kama umelewa,"

Akitumia njia hiyo alikuwa akitazama video za ngono kwa masaa mawili mpaka matatu kwa siku saba za wiki.

Tabia yake ilibadilika, anasema, asipo angalia picha za ngono, alipata kiu. Alikua akitumia masaa na masaa akijiambia kuwa anachokifanya si kosa alijiambia "Kila kitu kipo salama,huwezi pata magonjwa ya zinaa, huna haja ya kujipodoa. Kila kitu ni kwa maamuzi yako na unapata matokeo ya uhakika".

Lakini ili kuendelea kupata matokeo ya uhakika aina ya picha za ngono alizokuwa akiangalia zilimpeleka upande mbaya zaidi.

"Kwa kawaida unanza kuangalia picha za ngono za Vanilla, yaani mwanaume kwa mwanamke au mwanamke kwa mwanamke, hizi za kawaida. Lakini baada ya muda zinakuwa hazikupi midadi tena. Mwili wako unazizoea. Nisawa sawa na madawa ya kulevya unahitaji kuongeza dozi. Ili kuongeza unatazama zile picha za ngono za kibabe zaidi.

"Unaanza kuangalia zile za kufanya mapenzi kinyume na maumbile, baada ya muda ile inakuwa kawaida hivyo unaanza kutafuta nyingine ngumu kama vile zile picha za ngono za mtungo mfano wanaume wengi wanawake wawili.
Uraibu wa kingono ni matendo ya ngono yasiyo ya kawaida.

Hii ilianza kumkosesha raha Neila, ambaye alianza kuona ana kosa raha kadiri anavyo endelea.

Suala la kudhalilika ndio kitu abacho huleta hofu kubwa kwa kila mtu anayeamini kuwa yeye ni mraibu wa kingono. Aibu huwafanya waendelee kujificha na huwaendesha zaidi kuendelea na hali yao. Picha za ngono ni mchanganyiko wa mihemko na aibu," Neila anasema

Picha za ngono zimebadilisha namna anavyo tazama wanaume. Alipokuwa akijaribu kutafuta mwanaume wa kudumu tabia zao zilikuwa haziendani na alivyotaka.

"Nitaangalia kupitia mashati yao kama wana six pack" anasema. Urefu wa uume wa wanaume wa uingereza haukua unatosha kwangu. Lakini najua si njia nzuri ya kuchagua mwenza wa maisha."

Alikuwa namahusiano mengi yaliyo shindikana, lakini ukweli ni kwamba video za ngono alizokuwa anaangalia zilizokuwa zimebeba maudhui ya unyanyasaji dhidi ya wanawake ili kupata mihemko ndizo zilikuwa zikimpa hofu.

"Ilibidi nijiulize mwisho wake ni nini sasa, je nitaendelea kutazama video za ngono ili kujiridhisha na kukidhi hamu yangu.

Neila ameondoka mjini humo na sasa ni mtoa ushauri nasaha. Akiwa katika miaka 40 ameamua kuwa mtoa ushauri kwa wagonjwa wengine ambao wanaamini kuwa wameathirika na uraibu wa kingono.

Na kituo anacho tumia kuelimisha watu ndio kituo pekee kinachohudumia watu wa aina kama hiyo huko uingereza. Kupata huduma hiyo unalipia ma elfu ya pound kwa muda wa saa moja kwasababu kituo cha taifa cha kushughulika na Uraibu hakitambui kama uraibu wa kingono ni tatizo. Lakini inakadiriwa kuwa mamia kama sio ma elfu ya watu wanahitaji kupata matibabu ya hali hiyo kila mwaka huko uingereza, wengi wao ni wanaume.

Sababu ya tatizo hili ni kwamba wanawake wanaona aibu zaidi na inawapa ugumu katika kukiri tatizo na kuomba msaada. Lakini pamoja na maelezo yote. Paul ni mmoja wa wale waathirika zaidi na anahitaji msaada kuachana na uraibu wa kingono, moja ni kwa sababu ni mwanaume na pia hufika kileleni kwa kufanya ngono na si kuangalia picha za ngono.

Mawazo ya kujihukumu baada ya kumaliza ngono hubaki kichwani

Akiwa na takribani miaka 50 mreefu na aliyevalia vyema shati jeupe na koti. Paul anamwambia mwandishi wa BBC kuwa uraibu wake ulianza miaka 30 iliyopita akiwa chuo kikuu. Alikuwa na mahusiano mazuri na msichana wake lakini siku moja mahusiano yale yalikuwa hayatoshi kwake.

"Nilimpenda, kweli nilimpenda lakini sijui kwa sababu gani nilienda kumfwata kahaba," anasema. Nilikuwa nina haja sana ya kufanya ngono ya kipekee na tofauti na nilijua hiki ni kitu ambacho sitakiwi kukifanya. Sikuwahi kumsaliti lakini kwa kahaba niliona ni kitu tofauti."

Ndani ya wiki kadhaa tabia hii ilibadilika kabisa.

"Nilikuwa na mahusiano na wasichana sita kwa wakati mmoja na nilikuwa nakutana na makahaba wawili au watatu kwa wiki. Ilikua ni kama kuagiza chakula kwa sababu nina njaa. Nahitaji kitu, naagiza kinakuja kisha nasahau."

Anasema alijua kunakitu hakiko sawa. Na muda alipoanza kufikiria kumshirikisha mtu au kuto kufanya hivyo au hata kupata msaada, akapata kazi yake ya kwanza huko London - na akajikuta yupo kwenye mazingira ambayo tabia kama hii yake inakubalika sana.

"Huwezi amini, kusafiri nchi mbali mbali duniani, kujiingizia pesa nyingi sana kuhudhuria mara kwamara kwenye makasino na Bar Londonunajikuta mpaka unaingia kufanya ngono na watu unao fanya nao kazi, Paul anakumbuka. Sasa kwa kipindi hiki nafikiria labda nina tatizo? Au labda ni mwanaume tu wa kawaida?"

Je Uraibu wa kingono kweli upo?

Hata kwa kipindi hicho, mawazo ya kujihukumu yalibaki kichwani kwa Paul.

Atakwenda na wafanya kazi wenzie kwenye bar zenye wadada ambao huwachezea wanaume na kuwa kalia wakiwa watupu na kila mmoja atatumia Euro 1000 kwa usiku mmoja kwa siku za jumanne labda na kwenda tena siku za alhamisi. Lakini Paul pekeake alijikuta anarudi tena pale siku za jumamosi.

Kama Neila, Paul anasema alianza kutafuta kitu kingine kisicho kawaida ili kumpa raha ambapo baada ya kuwa mwanaume anaye fanya mapenzi na wanawake kwa miaka zaidi ya kumi akaanza kushiriki ngono na wanaume wenzie.

"Nikahama kabisa kutoka kwa wanawake mpaka kwa wanaume.Kwa hiyo sikuzote nilianza kutoka na wanaume. Naweza sema nina kiasi cha ushoga ndani yangu. Ni kutafuta muhemko wa hali ya juu tu. Na kipindi chote hicho nilikuwa na wasichana wazuri sana.

Kama alivyo sema Neila, Paul anasema tabia yake ilikuwa haizuiliki, kama hafanyi ngono alikuwa anapata kiu ya ngono. Na malengo yake yalikuwa si kufka kileleni bali ilikuwa ni tabia tu ambazo zilikuwa zinampa raha.

"Raha yangu ilikuwa ni kuwaza kile kitu ninakwenda kukifanya, kitu ambacho nilikuwa sitaki kitokee ni ku fika kileleni kwa sababu hapo shughuli yote inakuwa imeisha."
Ilimchukua Paul muda mrefu kuanza kutazama picha za ngono, baada ya kuzijua akiwa na miaka 12.

Ilimchukua Paul muda mrefu kuanza kutazama picha za ngono, baada ya kuzijua akiwa na miaka 12.

"Niliwahi kutana na majarida nikiwa bado kwa wazazi, niliyakuta yamefichwa wazazi wangu wakiwa hawapo. Hivyo ndio nilivyo anza kujua ngono. Lakini kuwa muwazi sikuwahi kupata ashki." Hayo yalibadilika baada ya kupata mtandao wenye kasi. Kwa kipindi hicho mawazo yake yalihama kutoka makahaba mpaka kwenye picha za ngono ambazo aliangalia kwa masaa na masaa.

Paul amepokea msaada kwa muda mrefu kutoka katika kituo cha Laurel, na sasa anaamini anaendelea vizuri na anapona. Haja lala na makahaba kwa miaka sasa na hajaangalia picha za ngono kwa miezi kadhaa, anasema.

Malengo yake ni kutulia kuanza upya na mwanamke mmoja tu.

"Ni ugonjwa wa upweke,Unafika mahali unatambua kwamba una muda mchache wa kushi duniani. Sijawahi kufanya ngono na kusikia raha na mtu ambaye nina mpenda na nina mjali. Ni kitu ambacho nimekikosa kwa miaka 30."

Mwezi wa sita, shirika la afya duniani lilitambua rasmi kwamba tabia za ajabu za kingono ni ni ugonjwa wa kimataifa. Washauri wa afya wanasema japo kuwa hakuna utafiti wa kutosha kuthibitisha rasmi kuwa ufanyaji ngono kupita kiasi ni uraibu, ni muhimu kwa serikali kutoa huduma ya ushauri nasaha kupitia mashirika yake.

Mwandishi wa BBC anasema kwa utafiti mdogo alio ufanya uraibu wa kingono ni tatizo na watu wanahitaji kusaidiwa.

Hata hivyo baadhi huofia kwamba kwenda kwenye huduma za kupata msaada wa kupambana na uraibu yaani rehab inatoa ishara kwamba unatafuta kisingizio cha kukwepa kukubali tabia zako.

Na katika kundi lililo hojiwa na BBC wanatambua kuwa kuna tofauti ya kufanya ngono kwa makubaliano na kuto kuwepo kwa makubaliano. Na wote hakuna aliyefanya uhalifu ila kwa kawaida watu hawa huanza kwa kujiumiza wenyewe kisha wapenzi wao. Wakati maharamia wa kingono wao huwajeruhi watu wanao watumikisha kingono.
 
Yap huo ni uraibu kabisa, na unaugumu wake namna ya kuuacha, kunahitajika nguvu kubwa sana kuacha.

Kuna kitabu nilisoma wacha nikupigie picha page angalau uone.
IMG_20181106_202035.jpeg
IMG_20181106_201938.jpeg
 
Huyo jamaa ni kama Mimi kuwa na wanawake sita lakini bado unaenda kununua
Na kwa Siku nilikuwa natongoza angalau wanawake watatu angalau mmoja au wawili hawakosi kunikubali

Kuna ambao nikimaliza kulala nao huwa hata siwapigii tena kujua wamefika makwao au vp na ndio basi tena
Nitamtafuta siku ambayo usingizi hauji
Na kila ninayempigia anashindwa kuja kwa sababu labda ni usiku sana wengine wanakaa mbali
Ikishindikana kabisa huwa naamka naondoka kwenda kusaka wauzaji wakati mwingine ni SAA sita usiku lakini lazima niende narudi nyumbani saa nane

Na hapo kesho mapema tu show zinaendelea kwa sababu hao wanaoshindwa kuja usiku wengine wanaahidi kuja asubuhi

Sikiwa na uwezo wa kukaa siku mbili bila sex nikiangalia idadi ya watu niliotembea nao na umri wangu huwa najiuliza kuna wale wazee ambao hawakubali kuzeeka
Bado tunagombea nao mademu si watakuwa wametembea na watu kama 1500 hivi au elfu 2000 na zaidi

Sex huwa INA uraibu sana ukiweza kukaa miezi miwili bila sex basis hata nyege huwa zinashuka na mwili kurudi kuwa sawa
 
Nafarijika sana kuona kuwa, kuna ambao walikuwa huwa na uraibu wa picha na video za ngono lakini wanaamua kutoka ingawa mara zote kuna vishawishi vya kuwarudisha huko. Kama zilivyo nyingi SITES za Pornography, hali kadhalika zipo pia nyingi SITES za kusaidia kuacha mambo hayo, hivyo mara zote kinachobaki ni kimoja tu.. MAAMUZI YA KIPI UNASOMA AU KUANGALIA!!

Lakini hivi karibuni kuna jambo ambalo nimeligundua. Mimi ni mdau mkubwa sana wa HADITHI na SIMULIZI ZA SAUTI!! Huko awali, hakukuwa na wimbi kubwa la simulizi zenye maudhui makubwa ya NGONO NGUMU!!

Lakini sasa hali sio ya kawaida!! Kuna utitiri wa SIMULIZI ZA SAUTI pamoja na tungo nyingine za maandishi ambazo ni NGONO TUPU!!! Hizi zinapatikana kwa wingi mitandaoni hasa Youtube na pia katika majarida mbalimbali.

Napenda sana kushauri kuwa, Ikiwa ulikuwa na uraibu wa picha na video za NGONO, na umeamua kuanza "Kujitibu", ni busara sana kuzikwepa simulizi hizi chafu. Uwepo wake hasa kwa lugha ya kawaida kabisa ambayo inatumika kila siku katika mazingira yetu unaamsha hisia zaidi ya mara mbili kuliko zile za kizungu tulizozoea na matokeo yake nadhani tunayafahamu..
 
Bora hizo sauti za wabongo kuliko Kule kwa wazungu Maadili yao kila kukicha wanatupotosha...
Tunachokiongelea hapa sio "uzungu wala uafrika wa ponography".. Tunajadili madhara mapana ya kitendo chenyewe. Ni madhara haya ambayo yanatupa nguvu ya kupambana taratibu taratibu na uraibu huu. Uafrika wetu tu kipekee unatuhamasisha sana kutunza sana thamani yetu badala ya kuutumia muda wote kukazana kuchungulia ngono...
 
Back
Top Bottom