Uraia wa nchi mbili ushauri ndugu zangu!

Aluta

Member
Aug 16, 2008
69
3
Habari zangu ndugu wana jamiiforums. Swali langu ni kuwa nimeishi EU (European Union) for 9years. Nilisoma degree hapa bure na kupata professional job hapa kwa muda wa miaka mitano. Leo hii wana suggest ni apply citizenship kwa kuwa nina creteria zote; kwamba wamenipostia applicationa forms; but note it's not a must. Sheria ya Tanzania hairuhusu uraia wa nchi mbili. Ila in my street knowledge I can handle those two passports in an inapropriate approach kama Wahindi wa Bongo; which is bad!Sasa swali niachane nao au ni apply? Of course passport ya nchi nchi hii niliyopo is one the most valuable passport in the World; ya Marekani is nothing.
 
sasa kwa nn usichukue mkoba wao tu na ukaupotezea wa kibongo??kwani mkoba wa kibongo utakusaidia nini???zaidi ya kupekuliwa hadi ma.t.ako kwa kushukiwa una madawa ya kulevya aka sembe....potezea mkoba wa bongo na haraka sana chukua mkoba wa mamtoni ulinde heshima ya kutokupekuliwa kama kuku ananyolewa manyoya kumbe wanatafuta sembe..mkoba wa bongo una shombo sasa hivi!!!
 
Changamkia huo uraia wa huko uliko usiulazie damu kabisa.
 
Mwenzetu unaishi utopia gani ambako pass ya Marekani is nothing!?

mkuu hata mimi nimeshangaa hapo,mkwaju wa Obama ndo mambo yote banaa....nchi nyingi unaingia kama unaterezaa vile no visa wala nini....wewe endelea kung'ang'ania huo mkoba wa kibongo uendelee kukaa airport masaa mawili unapekechuliwa kila sehemu...usiwaige mafisadi au watoto wa elites wa bongo wenzako wana mikwaju myeusi ya diplomats sio ya kijani atii....za kusikia changanya na zako!!!
 
Kabla ya kuchukuwa uamuzi wowote jiulize maswali yafuatayo
1.kwa nini unahitaji uraia wa Eu? Je ni ili nawe uonekane mzungu mwafrica kusafiri na passport yao kwenda nchi yoyote kama ulivyosema? Au kuna masilahi mengine utakayopata zaidi kuliko unayoyapata kwa sasa ukiwa na uraia wa bongo?
2.je unapenda uwe mzarendo kwa nchi gani Tz au Eu?
 
Back
Top Bottom