Uraia Pacha Tanzania: Siasa ya Bernard Membe na hatma yake

Ni suala usiloweza kulipinga na kwa kweli haliwezi kupingika hususan kipindi hichi cha utandawazi.

Ni jukumu lenu kuamua kusuka au kunyoa.
 
Katiba mpya ije mapema jamani usikute hata hizi shida tunazozipata sasa hivi tusingezipata.Nadhani hii ingepunguza makali kidogo manake Bongo kumekua sio sasa leo madr kesho walimu.Ili ukiona huku sio unahamia zako hata nchi yako nyingine
 
Ndugu zangu hebu naomba tuchangie hii mada ya kuwa na uraia pacha au kwa kimombo dual or multiple citizenships, pamoja na kwamba tunajua itatuletea faida nyingi nchini mwetu kama itaruhusiwa kuliko hasara zake, je watakaokuwa na
dual citizenship wataruhusiwa pia kujiingiza katika masuala ya kisiasa kama vile kuwa na haki ya kugombea au kushiriki katika chaguzi mbalimbali nchini mwetu? Nini kinaweza kutokea kama wataruhusiwa au kutokuruhusiwa kujiingiza moja kwa moja katika siasa ?
 
Uzoefu ktk nchi nyingine unaonesha kuwa mtu anaweza kuwa na uraia wa nchi moja, mbili, nyingi (multiple citizenship) au asiwe na uraia wa nchi yoyote kabisa.

Lakini ktk mambo ya kisiasa au utumishi wa umma wowote ule suala hili linabidi lipewe mkakati maalumu wa kuwa-screen, sio kila mtu maadamu ni raia tu anapewa nafasi nyeti. Ktk nchi zilizoendelea multiple citizenship sio tatizo ktk siasa/uongozi wa nchi ingawa sio kitu kinachotokea mara nyingi..

Mfano Anold Schwarzenegger (USA) alikuwa Gavana wa Jimbo la Carfonia na huku akishikilia uraia wake wa Australia.

Lkn kwa sababu USA iko makini waliangalia uwezo wake wakaona anafaa kupewa nafasi hiyo. Multiple citizenship inafaa sana ktk mambo ya biashara na uwekezaji. Hapo tunaweza kunufaika nayo sana. Lakini tukirudi nyuma pia tunaona ktk nchi yetu, hata hawa wazalendo tulionao wenye uraia mmoja wa nchi hii, bado ni hatari kwa usalama na uchumi wetu.

Hakuna uzalendo kwa nchi yetu. Tena ndo wanaonekana wabaya zaidi kuliko hata hao ambao tunawaogopa kuwa hawatakuwa wazalendo wakiwa na passport zaidi ya moja.
 
Hakuna Hasara ya uraia wa nchi mbili. Watu tunaowaongelea wengi ni raia wa Tanzania kwa sasa wengi wamezaliwa Tanzania na watoto wao. Watanzania wengi sana wazawa wapo nje kutafuta maisha na wakati mwingine ni muhimu kuchukua uraia wa nchi wanaoishi kwasababu ya familia na mafao yao ambayo mengi yanaenda Tanzania.

Mfano hapa USA sijaona tofauti ya uzalendo kwa watu wenye Dual na wasionao na sijaweza kujua kwasababu wote wana mapenzi sawa kwa nchi kwa mtazamo wangu. Ghana na Nigeria wanao Dual na Ghana hasa imewasaidia sana kwasababu watu wanajua hawatachukuliwa mali zao wanatuma pesa Ghana sana.
 
Hakuna Hasara ya uraia wa nchi mbili. Watu tunaowaongelea wengi ni raia wa Tanzania kwa sasa wengi wamezaliwa Tanzania na watoto wao. Watanzania wengi sana wazawa wapo nje kutafuta maisha na wakati mwingine ni muhimu kuchukua uraia wa nchi wanaoishi kwasababu ya familia na mafao yao ambayo mengi yanaenda Tanzania. Mfano hapa USA sijaona tofauti ya uzalendo kwa watu wenye Dual na wasionao na sijaweza kujua kwasababu wote wana mapenzi sawa kwa nchi kwa mtazamo wangu. Ghana na Nigeria wanao Dual na Ghana hasa imewasaidia sana kwasababu watu wanajua hawatachukuliwa mali zao wanatuma pesa Ghana sana.

...Labda hili la uDC litaruhusiwa kwenye katiba mpya lakini hata wasiporuhusu Watanzania watakaopata nafasi ya kuchukua uraia nyingine hawatalaza damu na kuacha nafasi hiyo ipotee. Kuna nchi nyingi ambazo baadhi ya kazi kuzipata ni lazima uwe raia...sasa kama unalipa kodi kama raia kwanini ujiwekee vikwazo kimaisha vya kutoruhusiwa kuchangamkia baadhi ya kazi ambazo zina mishahara minono na marupurupu ya hali ya juu?

Uraia wa nchi mbili hauna tatizo lakini kuna watu bado wanaamini mbongo yoyote yule ambaye amechukua uraia wa nchi nyingine ni msaliti....Hivi kuna wasaliti nchini kwetu kama hawa tuliowakabidhi madaraka makubwa nchi akina Mkapa & Co? Wanaishia kujaza bank accounts zao kwa ukwapuaji usiku na mchana na kuiacha nchi ikiwa uchi?

 
Hii kitu ina madhara sana kwa nchi kama TZ kwa kuwa wengi wanaotaka kukimbilia huku ni kutoka India, china, Somalia, na Uarabuni .. ni kwa sababu hali ni mbaya kule kwao.

Mfano Wasomali ndiyo wanaofanya kule kwao kusitawalike. wakuja huku itakuwaje?

Note: kuna Kiongozi kasha kula pesa za watu na anashabikia kinoma hili swala na yeye anao uraia wa Nchi mbili... Kuna mwingine Kapewa Uraia na anataka kuja Kuwa Rais wa Nchi hii na wote wako serikalini, Majina na details tunazo tunawakaushia tu.
 
Hii kitu ina madhara sana kwa nchi kama TZ kwa kuwa wengi wanaotaka kukimbilia huku ni kutoka India, china, Somalia, na Uarabuni .. ni kwa sababu hali ni mbaya kule kwao.

Mfano Wasomali ndiyo wanaofanya kule kwao kusitawalike. wakuja huku itakuwaje?

Note: kuna Kiongozi kasha kula pesa za watu na anashabikia kinoma hili swala na yeye anao uraia wa Nchi mbili... Kuna mwingine Kapewa Uraia na anataka kuja Kuwa Rais wa Nchi hii na wote wako serikalini, Majina na details tunazo tunawakaushia tu.


....lazima kuwekwe utaratibu maalum wa kuchuja watu hawa. Kuna vikwazo mbali mbali ambavyo nchi nyingine wanatumia ili kutowapatia uraia wale ambao hawafikii vigezo vilivyowekwa. Kwa mfano ni lazima ujue kuzungumza/kuandika lugha ya nchi hiyo, ni lazima uwe umeishi katika nchi hiyo kwa kipindi cha muda fulani na katika muda huo ulikuwa na biashara zako za halali au ulikuwa umeajiriwa kihalali na unalipa kodi. Ni lazima uwe umeenda shule angalau una 1st degree. Kunakuwa na mitihani ya kuhakikisha unajua mambo mbali ya nchi kama vile historia na Jiographia ya nchi ambayo ni lazima upate pass marks ambazo zinatofautiana kati ya nchi na nchi.

Na kuna kingunge mmoja sikumbuki kama ni Membe aliwahi kutamka siku za nyuma kwamba kama uDC utaruhusiwa basi kwanza wataanza kupewa Watanzania waliozaliwa Tanzania ambao wana uraia wa nchi nyingine na watoto wao waliozaliwa nje huku wakiangalia taratibu gani ziwekwe/zifuatwe ili kuwaruhusu wageni toka nchi tofauti kuomba kuwa raia wa Tanzania, lakini kama tujuavyo nchini mwetu hili la wageni litatawaliwa na rushwa ya hali ya juu.
 
Dual citizenship itatusaidia sana iwapo tutapitisha sheria ya kutambua, kuna watu wengi wenye asili ya nchi yetu nje wameshachukua uraia wa nchi hizo mathalan USA, UK na nchi nyingine Ulaya, Middle East or Far East. Hawa watu since wana uchungu na nchi ya asili yaio wangekuwa msaada sana, mfano wachezaji, wafanyabiashara, wasomi n.k. Nafurahi mada hii kuwa mezani na serikali ichukue hatua kuruhusu haraka iwezekanavyo
 
BAK

Ni hofu miongoni mwa watawala tu lakini uraia wa kuzaliwa wa mtu haufi kwani hata huko wanapopewa urai pacha wanaweka bayana uraia asilia.
 
Last edited by a moderator:
Mfano Anold Schwarzenegger (USA) alikuwa Gavana wa Jimbo la Carfonia na huku akishikilia uraia wake wa Australia. Lkn kwa sababu USA iko makini waliangalia uwezo wake wakaona anafaa kupewa nafasi hiyo. Multiple citizenship inafaa sana ktk mambo ya biashara na uwekezaji. Hapo tunaweza kunufaika nayo sana.

Arnold Schwarzenegger hajawahi kuwa na uraia wa AUSTRALIA - alizaliwa Osterreich a.k.a AUSTRIA
 
Wengine hata cha kuwekeza hatuna. Ila hatuoni sababu yoyote ile kwa nini tunyang'anywe uraia wetu endapo tukiamua kuchukua uraia wa kwingine.

ahahahaha ironically kama una cha kuwekeza basi ni rahisi ukiwa na uraia wa nchi nyingine maana wanakuabudu na hii sijawahi fahamu inatokana na nini labda inasababishwa na kasumba yetu ya kupenda "wageni"
 
Kumekuwepo na msukumo kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu uwepo wa sheria inayoruhusu uraia wa nchi mbili au zaidi ( dual citizenship) msukumo huu unazidi kushika kasi zaidi hasa wakati huu tunapojiandaa kuandika katiba mpya! huwa najiuliza maswali kadhaa kwamba je kuna umuhimu wa sheria hiyo kuwepo? nini faida na hasara za kuwa na sheria ya aina hiyo?

Watanzania wa kawaida wakulima na wafanyakazi watafaidikaje na sheria ya kuwa na uraia wa nchi mbili? Sheria hii itasaidia watanzania kutoka zaidi na kufanya kazi au biashara nje au ndio tutakuwa tumefungua mlango rasmi kwa wageni wenye pesa na mitaji mikubwa kuja kumiliki uchumi wetu wakiwa na haki sawa kama raia?
 
Wadau wote mliochangia nawashukuru sana,maana hili linatugusa kwa namna moja ama nyingine-kama si wewe unaweza kuwa na ndugu,rafiki au mtoto ambaye anaishi au ataishi nje miaka ijayo. Ahsante sana
 
Back
Top Bottom