Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,804
- 24,434
Kama kweli Lowasa na Kikwete ni marafiki wazuri sana na wanategemea kurithishiana madaraka, basi wote wawili hawana akili. Iwapo Lowassa ndiye anayejitangaza kuwa ni rafiki wa karibu sana wa Kikwete na urafiki wao haukuanza jana, basi huenda atakauwa anajipendekeza kusudi Kikwete asimtose kwenye kinyang'anyiro cha urais.
Iwapo Kikwete ndiye anayemshauri Lowasa kugombea kwa nia ya kumsaidia kulinda legacy yake, basi atakuwa amepotea sana kwa sababu Lowasa alishasema kuwa baada ya yeye kuondoka Uwaziri mkuu serikali ya Kikwete iliyumba sana; alisema hivyo kwa maana ya kuwa yeye ndiye aliyekuwa serikali ya Kikwete.
Urafiki wao huu ama haupo au ni wa kinafiki, kwani sijasoma mahala popote ambapo Kikwete ama amemsaidia rafiki yake huyo kupata uteuzi hata kwa mawazo tu au kuuandaa umma kwa kuushawishi kumkubali Lowasa kuwa ndiye kiongozi bora.
Nyerere alishawishi sana watu kumkubali Mwinyi na vile vile kumkubali Mkapa.
Iwapo Kikwete ndiye anayemshauri Lowasa kugombea kwa nia ya kumsaidia kulinda legacy yake, basi atakuwa amepotea sana kwa sababu Lowasa alishasema kuwa baada ya yeye kuondoka Uwaziri mkuu serikali ya Kikwete iliyumba sana; alisema hivyo kwa maana ya kuwa yeye ndiye aliyekuwa serikali ya Kikwete.
Urafiki wao huu ama haupo au ni wa kinafiki, kwani sijasoma mahala popote ambapo Kikwete ama amemsaidia rafiki yake huyo kupata uteuzi hata kwa mawazo tu au kuuandaa umma kwa kuushawishi kumkubali Lowasa kuwa ndiye kiongozi bora.
Nyerere alishawishi sana watu kumkubali Mwinyi na vile vile kumkubali Mkapa.