Upungufu wa watumishi sekta ya Afya na Elimu Morogoro

Upungufu wa watumishi sekta ya Afya na Elimu Morogoro

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mkuu wa mkoa Mororgoro Adam Malima amedhiinisha kuwepo upungufu wa waalimu 800 na watumkishi zaidi ya 500 sekta ya Afya, amesema hayo katika baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mlimba leo Juni 11, 2025
====

Kikao cha Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba kimeibua changamoto ya upungufu wa watumishi wa umma katika sekta za elimu na afya, hali inayotajwa kudhoofisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa kikao maalum cha kupitia na kutathmini hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, ameeleza kuwa sekta ya elimu inakabiliwa na upungufu wa walimu 800, sawa na asilimia 41 kwa shule za msingi na sekondari, huku sekta ya afya ikiwa na upungufu wa zaidi ya watumishi 500, sawa na asilimia 70 ya mahitaji.

RC Malima amesema changamoto hiyo imeathiri sana utoaji wa huduma bora kwa wananchi, na kutoa wito kwa menejimenti ya halmashauri kushirikiana na ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa ili kuandaa hoja ya pamoja ya kudai watumishi wapya kutoka serikali kuu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlimba, Innocent Mwangasa, ameeleza kuwa licha ya changamoto hizo, halmashauri imefanikiwa kupata hati safi kwa miaka mitano mfululizo.

Nao baadhi ya madiwani wamesema kuwa vituo vya afya vinaelemewa kutokana na uhaba wa vifaa tiba na wataalam, huku uhaba wa walimu ukiathiri umakini wa wanafunzi na ubora wa elimu hivyo wameiomba Serikali kutupia jicho changamoto hizo



See translation
 
Mkuu wa mkoa Mororgoro Adam Malima amedhiinisha kuwepo upungufu wa waalimu 800 na watumkishi zaidi ya 500 sekta ya Afya, amesema hayo katika baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mlimba leo Juni 11, 2025
====

Kikao cha Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba kimeibua changamoto ya upungufu wa watumishi wa umma katika sekta za elimu na afya, hali inayotajwa kudhoofisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa kikao maalum cha kupitia na kutathmini hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, ameeleza kuwa sekta ya elimu inakabiliwa na upungufu wa walimu 800, sawa na asilimia 41 kwa shule za msingi na sekondari, huku sekta ya afya ikiwa na upungufu wa zaidi ya watumishi 500, sawa na asilimia 70 ya mahitaji.

RC Malima amesema changamoto hiyo imeathiri sana utoaji wa huduma bora kwa wananchi, na kutoa wito kwa menejimenti ya halmashauri kushirikiana na ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa ili kuandaa hoja ya pamoja ya kudai watumishi wapya kutoka serikali kuu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlimba, Innocent Mwangasa, ameeleza kuwa licha ya changamoto hizo, halmashauri imefanikiwa kupata hati safi kwa miaka mitano mfululizo.

Nao baadhi ya madiwani wamesema kuwa vituo vya afya vinaelemewa kutokana na uhaba wa vifaa tiba na wataalam, huku uhaba wa walimu ukiathiri umakini wa wanafunzi na ubora wa elimu hivyo wameiomba Serikali kutupia jicho changamoto hizo
View attachment 3364392



See translation
Wabunge huko wanajadili namna ya kuanza kutumia plate numbers maalumu za magari yao
 
Barua ya Wazi kwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania

Mheshimiwa Mkuu wa Chuo,
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,

Kwa heshima na taadhima, napenda kuchukua fursa hii kwa niaba ya wanafunzi wa kitivo cha elimu kukupongeza kwa dhati kwa kuteuliwa kwako kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. Uteuzi wako ni ishara ya imani kubwa waliyonayo viongozi na jamii ya kielimu juu ya uongozi wako thabiti, hekima na maono chanya kwa maendeleo ya elimu ya juu nchini. Tunakuombea mafanikio mema katika kutekeleza majukumu yako.

Hata hivyo, sambamba na pongezi hizi, napenda kwa unyenyekevu mkubwa kuwasilisha malalamiko ya wanafunzi wa kitivo cha elimu tunaosoma shahada za uzamili na uzamivu kuhusu changamoto sugu ya ucheleweshaji wa kazi za utafiti unaofanywa na baadhi ya wasimamizi. Wasimamizi hawa wamekuwa wakichelewesha kwa makusudi kabisa kupitia kazi za wanafunzi, kuchelewa kutoa mrejesho au hata kutotoa majibu kwa mawasiliano ya mara kwa mara kutoka kwa wanafunzi.

Tabia hii isiyo ya kitaaluma imekuwa ikiwavunja moyo wanafunzi, kuwachelewesha kuhitimu kwa muda uliopangwa, na hata kuleta msongo wa mawazo miongoni mwao. Kwa mtazamo wetu, ucheleweshaji huu si wa bahati mbaya tena, bali ni wa makusudi, jambo linalodhoofisha lengo la chuo la kuwahudumia wanafunzi kwa njia ya haki na kwa wakati.
Mheshimiwa Mkuu wa Chuo, kwa kuzingatia dhamira yako ya kuboresha elimu, tunapendekeza hatua zifuatazo:
1. Kuweka miongozo yenye muda maalum wa kupokea, kupitia na kujibu kazi za wanafunzi.
2. Kuwabana wasimamizi kwa kuweka mfumo wa tathmini ya utendaji wao unaoshirikisha mrejesho wa wanafunzi.
3. Kuwepo kwa chombo maalum cha kushughulikia malalamiko ya wanafunzi kwa haraka na kwa siri.
4. Kuchukua hatua za kinidhamu kwa msimamizi yeyote atakayekiuka kwa makusudi majukumu yake.

Tunaamini chini ya uongozi wako mpya, matatizo kama haya yatapatiwa suluhisho la kudumu kwa ajili ya maendeleo ya elimu na ustawi wa wanafunzi wote.
NI SISI WAHANGA WA KITIVO CHA ELIMU CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA
 
Back
Top Bottom