Upungufu wa nguvu za kiume(hanisi)

Matapeli wameshatugundua waswahili kwamba tunapenda na kuendekeza sana NGONO. Ndiyo maana kila kukicha wanaleta sokoni dawa yenye maelezo lukuki tena basi yanayolenga maeneo yaleyale tunayoyapenda.

Kwa ufupi ni kwamba hakuna njia ya uhakika ya kupata nguvu NZURI za kiume zaidi ya kuwa na afya njema inayotokana na ulaji mzuri wa chakula na ufanyaji mazoezi ya viungo, full stop. Njia zingine ni batili na in fact, zinaendeleza uharibifu wa afya ya mwanaume na hupunguza maisha including kupata ukimwi.

biashara tu. nimeikamua lakini haina chochote. hakuna jipya
 
mkuu ukiwa na hilo tatizo utaiona ndogo sana...watu wameikia kujiua itakua kwa gharama hii?????any way wanasema watu wa uchumi kwamba usiangalie gharama ya pesa angalia faida ya kitu........

haya mambo jamani, biashara mtu! mi kwanza bora hili tatizo linipate na wala sitalitibu, manake vinanisumbuaga sana kunanilii.., watoto 6 in na 3 out wanatosha sana
 
Matapeli wameshatugundua waswahili kwamba tunapenda na kuendekeza sana NGONO. Ndiyo maana kila kukicha wanaleta sokoni dawa yenye maelezo lukuki tena basi yanayolenga maeneo yaleyale tunayoyapenda.

Kwa ufupi ni kwamba hakuna njia ya uhakika ya kupata nguvu NZURI za kiume zaidi ya kuwa na afya njema inayotokana na ulaji mzuri wa chakula na ufanyaji mazoezi ya viungo, full stop. Njia zingine ni batili na in fact, zinaendeleza uharibifu wa afya ya mwanaume na hupunguza maisha including kupata ukimwi.

Huo ni mtazamo wa mtu binafsi na ambaye hana matatizo haya ya kiafya. Watu wanatoa shuhuda zao kwa kupata tiba na hakuna awezaye kumkwamisha mtu mwenye tatizo aendelee kubaki na tatizo lake. Elimu ya afya ni nzuri sana kuzingatiwa na pia umuhimu wa kukabiliana na tatizo la kiafya ni muhimu pia kuzingatiwa katika jamii yoyote.
 
Kinga ni bora kuliko tiba. Vijana acheni ngono leo mpate vinono baadae.
  1. Kuanza mapenzi na umri mdogo unaharibu misuli ya uume na matokeo yake itawahi kuchoka.
  2. Kwa taarifa yenu mwanaume anapata complete intense orgasm ambayo imekomaa na inaraha zote kuanzia miaka 25. Chini yaho ni partial orgasm.

Zikiachwa tabia za kusababisha misuli kukosa nguvu haya pia huchangia katika mwanaume kukosa nguvu za kiume. Matatizo ya kisukari, ugonjwa sugu kama wa ini au kushindwa kufanya kazi kwa figo, matatizo ya hormones, matumizi ya madawa ya kulevya, matumizi makubwa ya pombe, uvutaji, matumizi makubwa ya dawa za hospitalini, msongo wa mawazo n.k
 
upumbavu mtupuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu! et nguvu za kiume, kwanza zikizidi sana zinasumbua tu.........
 
upumbavu mtupuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu! et nguvu za kiume, kwanza zikizidi sana zinasumbua tu.........

Zingatia sana yaliyochangiwa Ngakonda haya matatizo yasikukumbe sababu unakuwa na wakati mgumu sana
 
Hili ni kuhusu afya Safari_ni_Safari. Tuzingatie afya hilo wazo lako haliendani na linalozungumziwa

Kwani ukiongeza au kuimarisha nguvu za kiume matokeo yake nini? Ukhanithi (sio uhanisi) ni mojawapo ya njia za asili za kuzuia ongezeko la watu
 
Kwani ukiongeza au kuimarisha nguvu za kiume matokeo yake nini? Ukhanithi (sio uhanisi) ni mojawapo ya njia za asili za kuzuia ongezeko la watu

Mimi nahisi hujui ulisemalo katika jamii na haina haja ya kutoa comments kama hazijengi
 
haya mambo jamani, biashara mtu! mi kwanza bora hili tatizo linipate na wala sitalitibu, manake vinanisumbuaga sana kunanilii.., watoto 6 in na 3 out wanatosha sana

Hili tatizo siyo la kufanyia mzaha hata kidogo. Nadhani kama huna comment muhimu siyo lazima kuandika ili mradi umeandika chochote.
 
Elimu ni nzuri sana na watu wanaangamia kwa kukosa uelewa ndiyo maana inatakiwa kusambaza kwa wote pale inapobidi. Wapo wenye kuipokea kwa kejeli na wapo wenye kuipokea kwa mikono miwili. Hiyo ni kawaida ya binadamu lazima kuwe na makundi tofauti na lazima tuyakubali.
 
Nashukuru kwa wote waliotoa maoni yenye mtazamo chanya na wengi wamezingatia na kupata huduma nzuri. Inawezekana kuna ambao wanataka kutoa maoni pia nazidi kuwakaribisha
 
Shida wameshakuja kama wewe wengi sana hapa, watu amelipa pesa zao mara nyingi yu ndio manaa kila mtu anakutolea macho. wanatjuaje kama wewe ni taofauti na wale wengine wote? Hilo ndio swali kubwa
 
Shida wameshakuja kama wewe wengi sana hapa, watu amelipa pesa zao mara nyingi yu ndio manaa kila mtu anakutolea macho. wanatjuaje kama wewe ni taofauti na wale wengine wote? Hilo ndio swali kubwa

Wewe Mr bado upo kwenye kundi la watu wenye wasiwasi? Watu wameshapona na wengine wameulizia shuhuda mbalimbali sababu walikuwa kama unavyofikiri nimeshawapatia na wakaamini kuwa haya siyo mambo ya kutapeliana bali kweli kusaidia jamii.
 
Sawa mkuu tuwekee ushahidi kuwa hii sio biashara kama wenzako waliokutanvulia na ambao threads zao ziko kwenye stich notes.i am talking from experience
 
Sawa mkuu tuwekee ushahidi kuwa hii sio biashara kama wenzako waliokutanvulia na ambao threads zao ziko kwenye stich notes.i am talking from experience

Mwenye uhitaji zaidi wa hadi ushahidi tutaweza kuwasiliana. Email ipo na namba ya simu ipo katika hii thread.
 
Matapeli wameshatugundua waswahili kwamba tunapenda na kuendekeza sana NGONO. Ndiyo maana kila kukicha wanaleta sokoni dawa yenye maelezo lukuki tena basi yanayolenga maeneo yaleyale tunayoyapenda.

Kwa ufupi ni kwamba hakuna njia ya uhakika ya kupata nguvu NZURI za kiume zaidi ya kuwa na afya njema inayotokana na ulaji mzuri wa chakula na ufanyaji mazoezi ya viungo, full stop. Njia zingine ni batili na in fact, zinaendeleza uharibifu wa afya ya mwanaume na hupunguza maisha including kupata ukimwi.

huu ni wizi tu. kwa nn usimweleze mtu aende kwanza hospital. wewe unataka kutuaminisha kuwa hizi njugu zako ni mwisho wakati huna reference yeyote ile. acha bana, hurumieni watu nyie waganga wa kienyeji. tumechoka na mabango yenu kwenye nguzo za umeme, barabarani na humu jf. mm sasa naanza kuyang'oa.
 
Back
Top Bottom