Upotoshaji : "Serikali ya Magufuli" badala ya "Serikali ya JMT"

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
40,432
73,078
Sasa hivi viongozi wa serikali kuanzia mawaziri kuja chini wamejenga tabia ya kutoa maagizo huku wakitumia kauli kuwa serikali ya Magufuli inaagiza hili au lile na haitaki hili au lile.

Huu ni upotoshaji, hakuna serikali ya Magufuli popote hapa duniani zaidi ya nyumbani kwake, iliyopo ni ya Wananchi wa JMT inayoongozwa na Magufuli kama Rais aliyepewa ajira hiyo na masharti ya jinsi ya kufanya kazi na hao wananchi.

Huu mtindo wa kazi na maamuzi ya kidola haiwezekani kubinafsisha kwa mtu hali ambayo inamfanya hata akili yake ijijenge kuwa serikali hii ni mali "yangu".

Waziri akisimama kuzungumzia umeme anasema serikali ya Magufuli imeamua hivi, wakati huo ni mpango wa kitaifa. Na mikoani RC akishughulikia kisina atasema hivyohivyo wakati visima hivyovya serikali hata Magufuli havijui.

Hatari ya tabia hii itafikia hata Polisi wakizuia maandamano au fujo kujikuta wakitoa amri "Serikali ya Magufuli inatoa watu wote watawanyike mara moja kwa amani la sivyo ...."

Viongozi warudi kwenye matari, tunayo SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA pekee.
 
Hivi mleta mada ina maana mpaka leo hii ujagundua kwamba Serikali tuliyonayo ni ya Magufuli na si ya CCM wala JMT kama tulivyozoea. Ukitaka kuamini angalia utendaji. Mfano: Matumizi ya fedha kwa sasa si lazima yapitishwe na bunge, yanaweza tolewa maagizo kwamba fedha fulani iliyookolewa mahali fulani itumike kutengeneza barabara fulani.
 
Bush, Clinton administration???!!!
Hata Uganda kwenye vielement vya udikteta huwezi kumsikia waziri anasema " Serikali ya Yoweri Museveni inaagiza hili na lile" sasa haya ya hapa yametokea wapi? Na mbona yanashika kasi na kuwa desturi? Jee ndio sababu inayochangia viongozi kuwa na tabia za kinafiki kumridhisha mtu mwenye "serikali yake?"
 
Hata Uganda kwenye vielement vya udikteta huwezi kumsikia waziri anasema " Serikali ya Yoweri Museveni inaagiza hili na lile" sasa haya ya hapa yametokea wapi? Na mbona yanashika kasi na kuwa desturi? Jee ndio sababu inayochangia viongozi kuwa na tabia za kinafiki kumridhisha mtu mwenye "serikali yake?"
The Obama administration..!!!
Siku zote serikali ni ya rais husika na uongozwa kwa dira na ilani ya chama kilichomuingiza madarakani
 
I once said here, the current government is a one man government.
They're right in one thing, most of the government officers are working under President's directives.
Thus why we have raised our voice for the country to have a clear directives, terms and principles which will be followed without president hand.
Under current leadership, the leader is evaluated not on how well he fulfill his/her duties but how ready he/she is to bend the law,principles,guidelines etc only to act promptly to the problem without finding the sustainable solution.
I agree with you that, it is not right to say " Serikali ya Magufuli" they can say utawala wa Magufuli.
 
Bush, Clinton administration???!!!

Umetoa mfano sahihi! Wengine hutumia mf. "...Serikali ya Ahmed Nejad na utawala wa Tehran kwa jumla umeapa kuendelea na urutubishaji kwenye vinu vyake vya Nyuklia..." Hapo Tehran ikimaanisha Iran
 
Sasa hivi viongozi wa serikali kuanzia mawaziri kuja chini wamejenga tabia ya kutoa maagizo huku wakitumia kauli kuwa serikali ya Magufuli inaagiza hili au lile na haitaki hili au lile.
Huu ni upotoshaji, hakuna serikali ya Magufuli popote hapa duniani zaidi ya nyumbani kwake, iliyopo ni ya Wananchi wa JMT inayoongozwa na Magufuli kama Rais aliyepewa ajira hiyo na masharti ya jinsi ya kufanya kazi na hao wananchi.
Huu mtindo wa kazi na maamuzi ya kidola haiwezekani kubinafsisha kwa mtu hali ambayo inamfanya hata akili yake ijijenge kuwa serikali hii ni mali "yangu".
Waziri akisimama kuzungumzia umeme anasema serikali ya Magufuli imeamua hivi, wakati huo ni mpango wa kitaifa. Na mikoani RC akishughulikia kisina atasema hivyohivyo wakati visima hivyovya serikali hata Magufuli havijui.
Hatari ya tabia hii itafikia hata Polisi wakizuia maandamano au fujo kujikuta wakitoa amri "Serikali ya Magufuli inatoa watu wote watawanyike mara moja kwa amani la sivyo ...."
Viongozi warudi kwenye matari, tunayo SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA pekee

Kumbe wewe bado sana! Duuuh! Ushawahi kusikia Bush Administration or Obama administration sehemu yoyote?
 
Swali lako halijaeleweka. Unataka kusema nini?

Ningeshangaa sana kama ungelielewa! Mimi nimeanza kufungua milango yako ya fahamu, naamini watakuja watu kukuelewesha zaidi. Kama hata hili ulikuwa hujui bora ungeleta huu uzi katika mfumo wa swali (kuwapa benefit of doubt ya wanaolitumia). Mfano Kuita serikali yetu serikalia ya MAGUFULI badala ya serikali ya JMT sio upotoshaji? Naamini ungepata jibu muafaka. Kuongezea tu na kukupanua vizuri, je umewahi kusikia serikali ya Dar e salaam? Ikulu ya Nairobi? Ikulu ya White House?
 
Hivi mleta mada ina maana mpaka leo hii ujagundua kwamba Serikali tuliyonayo ni ya Magufuli na si ya CCM wala JMT kama tulivyozoea. Ukitaka kuamini angalia utendaji. Mfano: Matumizi ya fedha kwa sasa si lazima yapitishwe na bunge, yanaweza tolewa maagizo kwamba fedha fulani iliyookolewa mahali fulani itumike kutengeneza barabara fulani.

Wewe hujui, tena hujui kabisaaaaaaaa!
 
Hili nalo mna complain

Kweli wasomi wetu wanapenda kuumiza akili kwenye mambo yasiyo ba tija
 
Back
Top Bottom