Upotoshaji habari Unachangia Kuua Uhuru na Demokrasia

TL. Marandu

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
3,625
5,807
Nilishawahi kuwasikiliza Karume, Babu na Okello wakihojiwa Katika Video mara baada ya Mapinnduzi ya Zanzibaar 1964, Karume akijibu swali alisema sababu zilizofanya wafanye mapinduzi ni Kuwa, "Serikali hii haikuchaguliwa Kihalali" alisema, Sasa Leo Iweje Hii ya Sultani Shein iwe sahihi?



Kinachonisikitisha ni Aliserema za Vyombo vya habari Kushiriki Kuhalalisha Uharamu huu, Mfano Ni Hicho Kikatuni, Kikionyesha, "Zanzibar" Ikitunisha Misuli dhidi ya Dunia, Ukweli Ni Kuwa "Shein na CCM" Ndio waliokuwa waandikwe hapo Kifuani sio, "Zenji" Kwani Asilimia Kubwa ya Wazanzibari Pia Wanashutumu Uhuni uliofanyika.

Pia Jana Kulikuwa na Gazeti lilokuwa na Habari, "Zanzibar wako tayari kufa njaa Kuliko Kushinikiswa na Marekani na Ulaya. Ukweli Ni Kuwa Habari Hiyo ilitakiwa iwe, "Shein na CCM" Wako Tayari Wazanzibar wafe njaa Kuliko Kuachia Madaraka.
Katuni-24Machi2016.png

Katuni-24Machi2016.png
 
Back
Top Bottom