Upotolo wa simu yangu

Upotolo wa simu yangu

Ilikuwa karibia Ni-spend sku nzima hakika bila kucheka hadi nilipokutana na uzi huu
Eti smu inaandika yenyewe 'Naomba hela ya kula' Duh!
 
Daaah s3 ram yake ndogo mkuu kwa matumizi yako ni kama unaibaka
Matumizi yepi? Mi nilitaka iwe reserve phone, nilidhani Ni simu kumbe toy. Saa hizi kamechemka Hadi natamani kukawekea radiator ikapooze.
Mpaka kameharibu mifuko yangu ya suruali, imepauka kwa joto
 
Mpe mtoto achezee kanunue ingine hiyo haikufai hata kidogo!
 
Hiyo ni Hali ya kawaida kwa sisi watumiaji nguli wa tecno, tunao elewa maana ya tecno huwa hatukai na simu zaid ya mwaka 1 tunauza ikafie kwa mtu mwngne
Hii ya kwangu haijatimiza hata mwezi, niliinunua

Kuwa makini na hiyo simu mkubwa inaweza siku ikalipuka ikiwa mfukoni na kuharibu 'mayai'.
Mayai adhimu hayana spea
 
Simu yangu ni utopolo mtupu, unaweza ukawa uko kwenye application nyingine kabisa ie uko kwenye chrome, mara ghafla unakuta simu inajipiga yenyewe kwa namba yoyote ya kwenye phone book.

Ukiiweka mfukoni unakuta imejirekodi mavideo na imejipiga mapicha zaidi ya buku.

Betri inapata moto sana kiasi kwamba kama simu iko mfukoni inakuunguza kabisa. Inabidi uizime na uiache ipoe.

Simu hii ikiwa mfukoni unakuta imejituma meseji ya ajabu na inajituma kwa mtu yoyote, na muhanga mkubwa ni baba mkwe.

Kuna siku ilijituma SMS kuwa ninaomba hela ya kula, na kuna siku ikajituma sms kwa ex-girlfriend wangu kuwa I love you, without you I am nothing.

Pia hi simu haikai kabisa na chaji. Ikiwa full charge, baada ya masaa matatu Inakubudi uiweke Tena chaji.

Simu iko slow, ukifungua browser, unaweza kukaa dakika sita huoni herufi

Hii simu nimeinunua kwenye duka la Tigo, mwishoni mwa mwezi wa sita. Aina ya simu ni tecno S3
Ndugu zetu TECNO Tanzania ongeeni na Wachina wenu waboreshe bidhaa.
tecno bhana hizi ndo sifa zake
 
Hii hii unayotumia humu JF mkuu? Kama ni hiyo amini ni nzima mkuu.

Kuna moja wakati smart zinatoka ilikuwa ni M3, ilkuwa inajifungua saiti za porn tu, na kuitoa sasa hiyo sehemu haitoki mpaka uzime.
naitumia tecno M3 hadi leo
hilo tatizo lilikuwa kwako tu

kwangu nikishapiga simu kioo kikishaondoa mwanga ndio nitolee hio mwanga haurudi mpaka nikate simu lol

kwa sasa natumia Vodafone Vf683

masimu ya zamani kishenz
 
Wewe Bujibuji jiangalie Mkuu, Hiyo uliyonayo siyo simu bali ni Msukule wa Simu. Naamini simu halisi alibaki nayo yuleeeeee rafiki yako uliyeambiwa ulamsalimie baada ya Kugonga taa ya Benzi Lake. Na bado Mkuuu mwaka huu lazima uisome namba teheteheeeeeee
Duh😲😲😲
 
Back
Top Bottom