Upole!!

Upole!!

ukiendelea kubisha nitalembea album zima la koffi hewani, bora ukuwe mpole tu kama sredi inavyosema. halaf mbona Keren Happuch simuoni tena aisee! nimeanza kupoteza nguvu za kutype hafla!

Hujasoma quote yangu nini??
Nilipo-type tu kwamba KH anapenda miksa baaaaasi
Nikawa nimeua tembo kwa kijiti cha kutolea nyama nilichokipata pale manzese
Saa hizi yuko hapa anavaa nguo za ku . . . . .
 
Huu wimbo uliimbwa na CPU sambamba na Asha D



Ongea ukweli.... I wont feel bad kwamba sikuhusika sana ktk utunzi, yaani mimi kukubembeleza wakati unamlilia Lizzy ndo ionekane ilikua sambamba???
 
They always see but CPU no need ya kuogopa kwani una nia mbaya???


Wala usikonde, DA ndo anania mbaya na jinsi kemiko zetu zilivyoweza kutambuana
Ngoja nivae nguo nije . . .
 
Ongea ukweli.... I wont feel bad kwamba sikuhusika sana ktk utunzi, yaani mimi kukubembeleza wakati unamlilia Lizzy ndo ionekane ilikua sambamba???

Mdogo mdogo basi, si unajua tena . . . .
 
Njoo kwangu Lizzy,Mm ni mkali Tundu Lissu haoni ndani,halafu mkono wangu huwa mwepesi kama Sufu na ninapata joto haraka kama Petrol!!
Hahahah hapo kwenye mkono mwepesi ndo umeharibu!
 
Kwa faida ya kina kaka embu wadada tujuzane mnapenda wapenzi/wenzi wenu waweje linapokuja swala la upole.Hapa siongelei ule upole wa muda kwamba ikitokea ugomvi mara moja moja anaweza kujishusha ...naongelea ule upole ambao ndio tabia yake.Yani kila kitu ye anakua mdogo tu....hata kama kosa sio lake anakua mdogo...hata kama anaonewa anakua mdogo!!

Binafsi mi naogopa kua na mtu wa aina hii kwenye mahusiano kwasababu najijua ni mkorofi kidogo kwahiyo naona kama ntamuonea sana.Iwe kwa makusudi au la najua mwisho wa siku ntaishia kujisikia vibaya na ntakua nimeshamuonea tayari!!Napenda mtu ambae nikikosea atanipa live na sio kwakunibembeleza maana wakati mwingine mtu akikwambia kitu kwa utaratibu ni rahisi kupotezea ila ukiona kakasirika kweli usikilizaji na uelewaji unaongezeka!!

Michango tafadhali......

Lizzy,

Wengine ni wapole naturally. Ndio personality yao. Wengine wanakuwa wapole kwa sababu ya yaliyowatokea huko nyuma, kwenye familia, etc. Others may be suffering from a social disorder. Wengine wanaamua tuu kuwa wapole ili ku-compromise mambo. Wengine wanakuwa wapole kuepukana na domestic violence. Wengine kuepukana na kushtakiwa mara kwa mara kwa mjumbe wa nyumba kumi, nk. Wengine just want to keep the conflict btn them and you.

Lakini pia wapo ambao wana tabia ya kukupa a "silent treatment". Baadhi ya wanawake wanachukulia hili kama ni upole, but actually is not. Some other women can't stand the silent treatment at all. Wengine wanaamua kuwa wapole kwa sababu wanahisi kuwa kama hawatasema lolote it will drive the women crazy because women thrive on communication and when they dont get any of it they freak. Wengine wanajua kuwa wakiwa wakali they may end up losing their tempers. And, if they lose their tempers they lose you too.

Pia inawezekana wanaume wengine ni wapole simply because of the the women emancipation movements which burst into our living-rooms with a strident, demanding, angry, divisive and separatist energy. These movements have enabled women to reclaim their masculine energy. This may have led to some men to just assert themselves in a quiet (and often unsupported) way when they come across with a women's movement with masculine energy.

But the majority of men believe that whenever whenever they have an argument with a woman, the only way to win, is to lose. No matter what the argument is, they men usually has to do nothing or let her feel that she won. Lizzy kama ukikosea halafu akakupa live you may continue to attack him (with words) a lot (even though it was your own mistake) that it gets to a point of non-sense. But if he doesn't respond, then you can't do anything because he's not reacting. He'll talk when he feels that you can stay calm and not try to go into an argument. This is the most approach adopted by modern men.
 
Mimi ni mpole sana ila tatizo langu ni mjeuri. mwanamke atachonga anavyojua, mimi kimya. Hata akiamua kunishushia kipigo,mi poa tu ila asinitoe ngeu tu, mpaka naitwa Bushoke na washikaji.Sasa sijui kama wapole wengine ni jeuri.
 
Basi nimetubu mamii, usiende kwa kolokuwini

Kosa gani mimi nililokukosea wanitupa

Mrembo mwenye hadhi, pokea tena waraka
Usome na kuhifadhi, Yote nilioyoyandika
Nilipi lililokuudhi, Hebu niambie haraka

Fanya haraka muhibu, unipe hili hakika
Uneleze taratibu, Nipate kutoa shaka
Ni ipi hiyo sababu, Ilokupa kunepuka

Muhibu Lizzy nasema nawe, Hebu mwepushe shetani
Nyonda sinizuzuwe, Kanitia fedhehani
Toka kuniepuka wewe, Nimengia matesoni

Usione ni mzaha, mwenzio ni maradhini
Umenitia jeraha, La huba ndani kwa ndani
Naishi sina furaha, Kwa yondi lako Fulani

Kukurai si aibu, maadamu nakutaka
Na lau kama muhibu, Liko kosa limetuka
Basi mwana nimetubu, Msamaha nautaka

Kaditama tafadhali, wata kunihangiasha
Mwenzio kucha silali, Kwa huba huwa nakesha
Kumbuka na jambo hili, Kwako mahaba sijesha
Ohhh hubby..nimekusamehe kwasababu nakupenda sana!Usirudie tena lakini!
 
Mimi nilikuwa mkali kweli. Ilikuwa kila my nanilii wangu akikosea ninaye. Siku moja akaamua kunitolea uvivu, nikapata kipondo cha nguvu; kwa hiyo nikaamua kuwa mpole. Sasa sijui mimi utaniweka kwenye kundi gani?
 
[klorokwini; afazali leo umetuongelea wanaume wapole, yaani tunanyanyaswa kweli aisee.]


tehe tehe eti Klorokwini mpole na Asprini je asemeje?
 
Back
Top Bottom