Upinzani kufa kifo cha Mende 2020

Upinzani kufa kifo cha Mende 2020

Dan Muhina

Member
Joined
Jul 14, 2018
Posts
64
Reaction score
71
Wimbi la Madiwani wengi kutoka Upinzani kujivua Uanachama na kuhamia CCM ni dhahiri shahiri kuwa 2020 Upinzani hautokuwepo kabisa! Yapo mambo mengi ya kujiuliza ni kwanini mambo hayo kutokea sasa? Jibu ni moja tu kuwa zilizokuwa kero nyingi zikiisakama jamii ya wa Tanzania hadi kufikia Tanzania kuitwa Shamba la Bibi sasa zinatatuliwa moja baada ya nyingine, nidhani katika taasisi za Umma zimebadilika mno na kuwa zenye kuwaridhisha Wananchi,Aidha udhibiti wa upotevu wa Mali za Umma na udhibiti wa Uchumi umepelekea kila Mtanzania Mzalendo mwenye kuipenda Nchi yake( sio vibaraka)kufurahia hali hii hivyo kutokuwa na sababu ya kuuchagua Upinzani 2020 kwa maana hiyo tutegemee Upinzani kufa 2020
 
Mimi ningewashauri wapinzani wasisimamishe mgombea kwa nafasi yeyote ile nchi nzima. Then Watanzania tukae miaka mitano bila upinzani ili tuone kwa vitendo kazi ya vyama vya upinzani katika maendeleo ya nchi.
 
CCM mnatamani Bungeni mbaki peke yenu hilo halina shida nendeni wenyewe huko mjengoni ikifika 2020 then mtatupa majibu kuwa upinzani ni muhimu au hapana
 
Wimbi la Madiwani wengi kutoka Upinzani kujivua Uanachama na kuhamia CCM ni dhahiri shahiri kuwa 2020 Upinzani hautokuwepo kabisa! Yapo mambo mengi ya kujiuliza ni kwanini mambo hayo kutokea sasa? Jibu ni moja tu kuwa zilizokuwa kero nyingi zikiisakama jamii ya wa Tanzania hadi kufikia Tanzania kuitwa Shamba la Bibi sasa zinatatuliwa moja baada ya nyingine, nidhani katika taasisi za Umma zimebadilika mno na kuwa zenye kuwaridhisha Wananchi,Aidha udhibiti wa upotevu wa Mali za Umma na udhibiti wa Uchumi umepelekea kila Mtanzania Mzalendo mwenye kuipenda Nchi yake( sio vibaraka)kufurahia hali hii hivyo kutokuwa na sababu ya kuuchagua Upinzani 2020 kwa maana hiyo tutegemee Upinzani kufa 2020
Usikariri mkubwa hiyo 2020 usishangae huko ccm wakakimbia wengi kuja upinzani maana nako kumekuwa kwa moto kwa baadhi yao
 
Jiwe linapoipeleka ccm sijui.....

Haiwezekani utujazie wapinzani ndani ya chama chetu then uwape vyeo....

Humphrey polepole; video zipo akiiponda ccm live leo jiwe limempa ukatibu itikadi wa chama.

Julianza shoza; huyu umemtoa chadema leo waziri

Kitila mkumbo; leo umempa ukatu mkuu serikalini.

Mrema; mwenyekiti wa parole
 
Kwa nini ufe wakati upinzani upo kisheria,hiyo mkwara wanayopigwa ni suala la muda tu, muda wenyewe ndio utaamua baada ya kuwepo mbwembwe nyingi lakini hali ya maisha inazidi kudorora.
 
Wimbi la Madiwani wengi kutoka Upinzani kujivua Uanachama na kuhamia CCM ni dhahiri shahiri kuwa 2020 Upinzani hautokuwepo kabisa! Yapo mambo mengi ya kujiuliza ni kwanini mambo hayo kutokea sasa? Jibu ni moja tu kuwa zilizokuwa kero nyingi zikiisakama jamii ya wa Tanzania hadi kufikia Tanzania kuitwa Shamba la Bibi sasa zinatatuliwa moja baada ya nyingine, nidhani katika taasisi za Umma zimebadilika mno na kuwa zenye kuwaridhisha Wananchi,Aidha udhibiti wa upotevu wa Mali za Umma na udhibiti wa Uchumi umepelekea kila Mtanzania Mzalendo mwenye kuipenda Nchi yake( sio vibaraka)kufurahia hali hii hivyo kutokuwa na sababu ya kuuchagua Upinzani 2020 kwa maana hiyo tutegemee Upinzani kufa 2020
Umemaliza kuota? Elimu yako ni ya bei na kiwango gani? Hukufundishwa na walimu wako kuwa hakuna kitakachosemekana kufanyika hadi pawepo na nguvu mbadala na kinyume? Au ulifundishwa na kuyaacha maarifa yale kwenye kizingiti cha mlango wa darasa?
Kwa taarifa yako tu upinzani upo hata kwenye imani zetu na ndio maana kuna Mungu na shetani ambaye wewe unamwabudu kuliko kitu chochote!
 
Muumba wa mbingu na nchi ana mpinzani mpaka sasa.
 
Mleta maana unajua maana ya Upinzani?
Au unaungalia upinzani ndani ya vyama?!
 
Huu uzi una habari njema.
tumblr_oeoh3nLzRW1rchkzlo1_400.gif
 
Wapuuzi, wajinga, narrow minded ndio Wenye akili na mtazamo Kama huo! Acheni wizi muone, Acheni kutumia jeshi la Polisi muone mziki wake.
 
Et kero zinatatuliwa wabongo bana hatari sana sijui elimu yetu imekaaje lakin utakuwa ugonjwa waafrika wengi kuwa na ufinyu wa fikra
 
Ungezungumza kwa kurejea tume ya uchaguzi (NEC) Katiba iliyopo na polisi ungeni-impress!
 
Ningekuwa naruhusiwa kutukana hapa JF ningekutukana kuwa una*iwa wewe siyo bure!
 
Ni ujinga uliopitiliza kushadidia hoja za kufa kwa upinzani nchini..
Anyway ninavyofahamu mimi ni kuwa hata huko ccm wapinzani wapo kibao sema tu wanashughulikia maslahi ya matumbo yao kwanza!
Zaidi ya yote.. Nchi au taasisi au jumuiya yoyote ya watu iliyokosa upinzani (utofauti wa maono/mawazo) ni sawa na maiti..!
 
Jiwe linapoipeleka ccm sijui.....

Haiwezekani utujazie wapinzani ndani ya chama chetu then uwape vyeo....

Humphrey polepole; video zipo akiiponda ccm live leo jiwe limempa ukatibu itikadi wa chama.

Julianza shoza; huyu umemtoa chadema leo waziri

Kitila mkumbo; leo umempa ukatu mkuu serikalini.

Mrema; mwenyekiti wa parole
Rais Magufuli amejipambanua si mbaguzi wa kiitikadi ndio maana ameweza kuwateua Wapinzani kwenye nafasi nyeti Serikalini. Hongera Rais Magufuli kwa kujenga umoja wa kitaifa
 
Back
Top Bottom