Wakuu, sasa hivi nadhani tunaelekea pazuri, mahala ambapo tunaweza pata solution ya matatizo haya yote..
Nimefikiria sana swala hili na kusema kweli nashindwa kabisa kuamini kinachotokea kila siku.. Kuna wakati vyama vya Upinzani vilishikamana vikawa pamoja karibu kabisa kufikia Muafaka...wakatokea wachawi wakasambaratika ktk chaguzi ndogo zilizofuata...
Haya tunakaribia uchaguzi mkuu, vyama vyote vya Upinzani umejenga upinzani mkubwa sana kiasi kwamba siamini ati J.J. Mnyika na Zitto leo ni wapinzani ndani ya chama. Sababu hata siielewi zaidi ya ku wonder if kweli hawa ni viongozi wazuri au wana agenda zao binafsi.
Kisha mawazo ya mkuu wangu Kichuguu kuhusiana na kiti cha mwenyekiti wa chama kuwa ndiye mgombea wa kiti cha Urais kwa tiketi ya chama ni mfumo mbaya sana..ndio maana tumeona uchaguzi TLP, CUF na sasa hivi Chadema umezua utata mkubwa sana ndani ya chama. Kama kweli vyama vya upinzani vinapenda mageuzi basi bila shaka sauti ya Umma iwe mbele ya maamuzi yao. wananchi tutapenda kuona muungano wa vyama hivyo wakimsimamisha mtu mwingine kabisa nje ya kundi la wazee au wababe walioshindwa na JK mwaka 2005. Ushindi kwao hauwezekani, watrudi kugombea Ubunge na mtu mwingine kabisa mwenye sifa na uwezo wa kupambana na JK achaguliwe kuwakilisha vyama vyote.. Mtu huyo awe Dr. Slaa!.
Mbowe mshikaji, napenda sana kumwona Ikulu (maanake nitauchinja) kwi kwi kwi!... lakini ni lazima niukubali ukweli kwamba anahitajiwa mtu mwingine kabisa kupambana na JK mwaka 2005. Mbowe, Zitto, Lipumba, Mrema na wengine wote wataweza kujitokeza tu ikiwa Upinzani utachukua utawala na hapo ndipo wananchi tunaweza kuwapima hawa viongoizi wakiwa ktk nafasi za utawala. na kama Muungano au mshikamano wao utavunjika basi sii haba kumwona Mbowe, Lipumba, na Mrema wakirudi mwaka 2015 wakati Upinzani wameshachukua nchi mwaka 2010.. Mbowe bado kijana, Zitto bado hata kufika Umri wa kugombea kiti hicho, Lipumba, Mrema na Cheyo hawa hawawezi kushinda hata kwa miaka 20 ijayo ikiwa vyama vyao vitasimama pekee.
Hivyo kusimama kwao wakitumia neno Demokrasia ktk swala ambalo wanajua kabisa haawezi kujenga ila kubomoa ni upuuzi mtupu..
Uchaguzi mwaka kesho 2010, Kikwete atapeta vibaya sana kwa sababu tu ya wajinga fulani wanaofikiria wao ndio nguzo ya Upinzani nchini..Mafisadi wamekuwa hatua moja mbele yetu kwa kila siku ya matumaini yetu kiasi kwamba tunapoteza imani...Tunaupoteza muda muhimu sana ktk mapinduzi ya siasa nchini..