Upigaji kwenye Kumbi za Shughuli

Edzone

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2017
Posts
2,016
Reaction score
1,858
Kuna ukumbi unaitwa Bridge Stone tangibovu ukiwa na harusi pale au sendo off, inabidi kua makini na wahudumu wale sita unaopewa,
Tokea nizaliwe sijawahi kuona wezi wa vinywaji kama pale. Wanapewa oda hawapeleki, kweli mtu anaiba kreti sita za bia.
 
Kama kuna mdau atakua na party pale awe macho na wahudumu hasa vinywaji.
 
Kama kuna mdau atakua na party pale awe macho na wahudumu hasa vinywaji.
Mwizi ni mwizi, ukielekeza macho kwenye vinywaji ataiba kingine kwakuwa ni mwiko mwizi kutoka mikono mitupu
 
Muhimu tuwe macho kwenye kamati zetu
 
Dawa yao ni kuwaambia wahudumie ile meza kuu pekee (yenye bibi na bwana harusi).
Watabaki wanapiga vigelegele tu maana wale watu hua hawanywi sana.
 
Kuna ukumbi unaitwa Bridge Stone tangibovu ukiwa na harusi pale au sendo off, inabidi kua makini na wahudumu wale sita unaopewa,
Tokea nizaliwe sijawahi kuona wezi wa vinywaji kama pale. Wanapewa oda hawapeleki, kweli mtu anaiba kreti sita za bia.
Hao sio wahudumu ni vibaka sugu
 
bora tuliwapa makfi ya kutosha ukumbini na shuhuli inaendelea. wenyewe ndo waende polisi
 
Kuna ukumbi unaitwa Bridge Stone tangibovu ukiwa na harusi pale au sendo off, inabidi kua makini na wahudumu wale sita unaopewa,
Tokea nizaliwe sijawahi kuona wezi wa vinywaji kama pale. Wanapewa oda hawapeleki, kweli mtu anaiba kreti sita za bia.
Hakuna siku niliumia nilichangia harusi pesa ndefu na ndio harusi niliwahi changia pesa ndefu sana maana ilikuwa ya rafiki yangu wa karibu.
Nafika kwenye harusi kuna juice na soda tu kwasababu baba bi harusi ni askofu.
Kumbe wanywa ulabu ilikuwa inabidi utoke nje kwenye bar hapo unaonyesha kadi unapiga za kutosha.
Nimekuja kujua mwishoni wakati harusi imeisha roho iliniuma na watu wengi hawakwenda walikuwa hawajui kama mimi.
 
Mimi unanirudishia hela yangu, napotoa mchango nawaambia kabisa
 
Mimi unanirudishia hela yangu, napotoa mchango nawaambia kabisa
Sema mimi sio mnywaji kivile ila wana niliokuwa nao ndo nkitaka wanywe maana nilichanga pesa ndefu sana mkuu, 500k maana ilikuwa harusi ya jamaa yangu hakuchangisha pesa, familia ilijichanga na mimi nikatoa kaka mshikaji tu, na wana wengine wa karibu yake. Ila hakutoa kadi za michango.
 
Siku nyingine unakunywa hata konyagi ndogo, inakuondoa uoga unaondoka na bibi harusi
 
Siku nyingine unakunywa hata konyagi ndogo, inakuondoa uoga unaondoka na bibi harusi
Mkuu mimi si mnywaji kihivyi na hasa vinywaji vikali kama konyag, whisky, vodka sigusi kabisa.
Kuna siku nilikunywa john walker black label almost nusu chupa, aisee shughuli niliyopata sitokuja kusahau.
Niliamka naumwa halafu nna njaa ya dunia nzima.
 
Mkuu mimi si mnywaji kihivyi na hasa vinywaji vikali kama konyag, whisky, vodka sigusi kabisa.
Kuna siku nilikunywa john walker black label almost nusu chupa, aisee shughuli niliyopata sitokuja kusahau.
Niliamka naumwa halafu nna njaa ya dunia nz
sasa hiyo hali ni hangover, au utajiri, mali, malupulupu na bati, ndo mtaji mkubwa. Haukula vizuri kaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…