Kodi zingetozwa kwenye harusi ingefaa sana

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,634
7,006
Napendekeza Serikali ianze kuangalia suala la kodi kwenye harusi.

Binafsi kwa mwaka nachangia karibu laki sita kwenye shughuli za sherehe za harusi. Huko nakunywa soda zisizozidi 6 na maji madogo 6 pamoja na chakula ambacho nikiagiza hotelini hakizidi sh.elfu 60 yaani milo sita.

Sasa ukiangalia pesa nyingi inaenda wapi?

Kuna wanaokunywa bia hao ndio wanakunywa angalau vinywaji vingi.Pia gharama za kumbi,keki na mapambo kwa ujumla.

Hivi vyote ni anasa tu ni tofauti sana na suala kama kutuma pesa.Unaweza kuwa unamtumia mtu mwenye shida sana mfano ugonjwa n.k.

Serikali ingeweka kikokotoo kama cha kununua gari kwenye hizi arusi. Maana watu huchanga kama wana wazimu na hawaoni uchungu kutoa pesa hizo.

Watu wenye kumbi nao kutokana na uchache wa kumbi wanatoza gharama kubwa sana kwa sherehe ya siku moja.

Serikali ingeweka utaratibu kuwe na risiti za efd kwa anayechanga ili iambatanishwe na kadi yake ya arusi.Na waweke mtu wao pale mlangoni wanapoingia ili akague kila mtu awe na risiti.

Ni mawazo yangu tu
 
Taxi zote bubu na zisizo bubu ziwekewe mashine za kukusanya kodi kwenye nauli zao ili kupanua wigo wa kodi.
 
Haya ni maeneo ambayo serikali inapata fedha bila kusubiri ya kutolea

Na itahamasisha watu kupunguza unnecessary expenditure
 
... yaani kamati ikianza kikao cha kwanza tu TRA hawa hapa!
1626502700410.png
 
Mbona Kodi zinalipwa au unataka cheti Cha Ndoa ndio kiambatane na Risiti ya EFD??
 
Mbona kodi kwenye harusi zinalipwa .Mwenye ukumbi lazima alipie 100,000 kila harusi au sherehe inayofanyika pale toa ile kuwa inayoendesha ukumbi ni kampuni hii 100,000 inaenda halmashauri ukifanyia nyumbani ikizidi watu 50 unalipa 50,000.

MC wanalipa kodi ,watu wa chqkula ,vinywaji nk.Sasa wewe kodi nuingine ipi unataka ilipwe
 
Niliskia kuhusu maMC kusajiliwa na kulipa kodi. Waende pia kwa wapishi wa maharusin, wapambaji coz hao ndio wanaingiza faida.

Utatoza vipi kodi kwa michango ya watu ambayo haiingizi faida yoyote. Ila kwakua serikali yetu ni ya kujitoa akili hawataweka kwenye harusi tu ni mapaka vipaimara, birthdays na misibaa.

Kwanza kufanya sherehe si mpaka ulipie serikali ya mtaa kwanzaaa 🤔🤔.
 
Napendekeza Serikali ianze kuangalia suala la kodi kwenye harusi.

Binafsi kwa mwaka nachangia karibu laki sita kwenye shughuli za sherehe za harusi. Huko nakunywa soda zisizozidi 6 na maji madogo 6 pamoja na chakula ambacho nikiagiza hotelini hakizidi sh.elfu 60 yaani milo sita.

Sasa ukiangalia pesa nyingi inaenda wapi?

Kuna wanaokunywa bia hao ndio wanakunywa angalau vinywaji vingi.Pia gharama za kumbi,keki na mapambo kwa ujumla.

Hivi vyote ni anasa tu ni tofauti sana na suala kama kutuma pesa.Unaweza kuwa unamtumia mtu mwenye shida sana mfano ugonjwa n.k.

Serikali ingeweka kikokotoo kama cha kununua gari kwenye hizi arusi. Maana watu huchanga kama wana wazimu na hawaoni uchungu kutoa pesa hizo.

Watu wenye kumbi nao kutokana na uchache wa kumbi wanatoza gharama kubwa sana kwa sherehe ya siku moja.

Serikali ingeweka utaratibu kuwe na risiti za efd kwa anayechanga ili iambatanishwe na kadi yake ya arusi.Na waweke mtu wao pale mlangoni wanapoingia ili akague kila mtu awe na risiti.

Ni mawazo yangu tu
Kweli aisee...hii nayo inaweza kuwa chanzo kingine cha mapato bila kutumia nguvu na inafikirisha... si unajua arusi nyingi bongoland ndo sehemu mojawapo ambayo huwa inakuwa na matumizi mengi ambayo ni yakujitakia tu ...arusi ni yako na kwa raha yako, sasa wataka watu wengine lazima wakuchangie..yaani mie huwa napenda mabara mengi mengine wanavyofanya eg.ulaya, Marekani na kwingineko, arusi zao nyingi wahusika wakuu kwa gharama za arudi ni ndugu,marafiki na wale wa karibu, na watu wachache tu,sio gharama kubwa kama zetu za arusi, kuanza mwaka mzima kuchangisha watu,na watu huwa wanachangia kwelikweli, na kushona nguo za gharama kibao kwa kitu cha masaa machache tu ya siku moja...anyway kupanga ni kuchagua...yaani Mwigulu uhamie na huko kwenye arusi maana vilevile utapata tozo za bure nyingi...si ndo kuongeza wigo wa kodi....au nadanganya jamani....kazi iendelee.
 
Hatuwezi tukamlaumu kiongozi naamini siku zote maendeleo ya kweli lzm yawe na changamoto kwhiyo tujenge taifa letu kunasiku tutafurahia matunda haya.
 
Back
Top Bottom