Lj Mwambar
JF-Expert Member
- Apr 23, 2013
- 605
- 355
Lizaboni
Mkuu LISABON nimekuwa ninafuatilia michango yako hapa JF kwa karibu sana, na kwa sasa ninaomba nikujulishe haya kwani ni kwa faida yako:
1. Ukimtaja EL kuwa ni fisadi ni moja kwa moja kuwa viongozi wakuu wako nao ni mafisadi (hii haitaji justification)
2. Kama Mwenyekiti wenu alishindwa kumfukuza au kumkemea mbele ya watanzania wote, basi nafikiri jibu unalo.
3. Kama mna amini kweli ni fisadi basi mwambie mwanasheria wa serikali au chama chenu ampeleke mahakamani ( hapa mtakuwa wengine mashahidi au washitakiwa wakubwa, nafikiri unaelewa maana yake)
4. Huyu mtu tumchukulie kama binadamu yeyote. Na jaribu kufikiria mchango wake kwa taifa. Haikutakiwa kumdharalisha kama mlivyofanya DODOMA. Na sababu zenyewe hazikuwa za kimsingi (hapa tunaweza kuwaita wakina Dr. Nchimbi, Mhs Simba, na Mhs Adamu .. ni malaika wateule)
5.Ikumbukwe katika hali yoyote ile ya kumtendea mtu mabaya na hasa kumyima haki, basi matukio kama haya yatatokea na ndiyo maana unaona hili swala linashika kasi!
ONYO:
Ni viongozi wengi ndani ya chama chako na hasa wale wenye nyazifa kuliko wewe kada wa Lumumba wamekaa kimya kwani wanajua hasa KOSA liko wapi. Na hutaona wanalopoka kuhusu huyu mhs EL kwa sababu anajua mengi mabovu ambayo yakiwekwa wazi hakauna atakaye salimika. Ni bahati mbaya wewe unacheza ngoma USIYO IJUA.
LENGO:
Hapa lengo kubwa ni kubadiri mfumo mbaya wa kuruhusu vitendo vya kifisadi. Ingeleikuwa rahisi kwenu kumuacha EL agombee lkn mnakubaliana kuuvunja mfumo wenu ulio ota mizizi ya kifisadi.
Mkuu ukisema kanyimwa haki una maana gani? Alizuiwa kuchukua fomu? Alizuiwa kutafta wazamini au vp mkuu? Alikatwa kama wenzake walivokatwa mbona wenzie wametulia ye ni nani hasa hadi iwe nongwa .ccm haiogopi mtu amekuja huko mnapomuabudu
Last edited by a moderator: