Stephano Mango
Member
- Mar 23, 2012
- 64
- 13
WAZIRI wa sera na uratibu wa Bunge Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jenista Mhagama amepita bila kupingwa kwa sasabu wakati wa mchakato wa kuchukua fomu za kuomba uongozi ndani ya chama wagombea wenzake wawili waliojitokeza kuwania nafasi hiyo mmoja fomu ilisahiniwa na mtu mwingine ambaye si mgombea na mwingine siku moja kabla ya kuanza kampeni alianguka ghafla chooni wakati akijisaidia.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake katibu chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea Vijijini Rajab Huonde aliwataja wagombea ambao walishindwa kuingilia kwenye kinyanganyiri hicho kuwa ni Lazaro Komba Bunungu mfanyakazi wa Tanroads mkoa wa Tanga , pamoja na Clement Makaburi Mwinuka mkazi wa Magagula .
Alifafanua kuwa, sababu zilizomfanya bunungu kushindwa kugombea nafasi hiyo ni kwamba baada ya kupata ajali hiyo hakuweza kuleta taarifa yoyote juu ya maendeleo ya ugonjwa wake hadi kampeni zilipokwisha ,na mwinuka fomu yake ya kuomba uongozi ndani ya chama haikusainiwa na mgombea mwenyewe.
Alisema kuwa jimbo la peramiho ambalo linakata 17 wanachama wameridhia kumpitisha Jenista Mhagama kutokana na wagombea wengine kutoonekana siku ya uchaguzi .
Wakati huo huo Mkurugenzi shirika lisilo la kiserikali RUCCODIA Joseph Mhagama amewabwaga makada wenzake nane baada ya kupata kura 5081 ,akifatiwa na profesa Elieuther Mwageni makamu mkuu wa chuo cha Ardhi wa fedha na utawala jijini Dar es salaam aliyepata kura 993, wengine ni Mkuu wa wilaya ya Tarime Glolius Luoga (838), mkurugenzi mkuu mstaafu wa Idara ya uhamiaji nchini Kinemo kihanamo (734),mkuu wa shule ya sekondari ya kutwa London manispaa ya Songea Christopher Mwageni (200) Limo Mwageni mwalimu shule ya sekondari mpanda (84)
Huonde alifafanua kuwa, wagombea wengine wawili ambao ni Tasilo Mahuwi na Venance Mgaya siku ya mwisho waliamua kujitoa kwa sababu ambazo hawakuziweka wazi wakati pius mwageni fomu yake ya kuomba uongozi baadaye ilibainika kuwa haikusainiwa na mgombea mwenyewe hivyo ilimfanya akose sifa ya kugombea nafasi hiyo.
Na Stephano Mango, Songea
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake katibu chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea Vijijini Rajab Huonde aliwataja wagombea ambao walishindwa kuingilia kwenye kinyanganyiri hicho kuwa ni Lazaro Komba Bunungu mfanyakazi wa Tanroads mkoa wa Tanga , pamoja na Clement Makaburi Mwinuka mkazi wa Magagula .
Alifafanua kuwa, sababu zilizomfanya bunungu kushindwa kugombea nafasi hiyo ni kwamba baada ya kupata ajali hiyo hakuweza kuleta taarifa yoyote juu ya maendeleo ya ugonjwa wake hadi kampeni zilipokwisha ,na mwinuka fomu yake ya kuomba uongozi ndani ya chama haikusainiwa na mgombea mwenyewe.
Alisema kuwa jimbo la peramiho ambalo linakata 17 wanachama wameridhia kumpitisha Jenista Mhagama kutokana na wagombea wengine kutoonekana siku ya uchaguzi .
Wakati huo huo Mkurugenzi shirika lisilo la kiserikali RUCCODIA Joseph Mhagama amewabwaga makada wenzake nane baada ya kupata kura 5081 ,akifatiwa na profesa Elieuther Mwageni makamu mkuu wa chuo cha Ardhi wa fedha na utawala jijini Dar es salaam aliyepata kura 993, wengine ni Mkuu wa wilaya ya Tarime Glolius Luoga (838), mkurugenzi mkuu mstaafu wa Idara ya uhamiaji nchini Kinemo kihanamo (734),mkuu wa shule ya sekondari ya kutwa London manispaa ya Songea Christopher Mwageni (200) Limo Mwageni mwalimu shule ya sekondari mpanda (84)
Huonde alifafanua kuwa, wagombea wengine wawili ambao ni Tasilo Mahuwi na Venance Mgaya siku ya mwisho waliamua kujitoa kwa sababu ambazo hawakuziweka wazi wakati pius mwageni fomu yake ya kuomba uongozi baadaye ilibainika kuwa haikusainiwa na mgombea mwenyewe hivyo ilimfanya akose sifa ya kugombea nafasi hiyo.
Na Stephano Mango, Songea