Ilisolokobwe
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 1,850
- 803
wanajf hamjambo????
kama wiki 2 zilizopita hapa jf kulikuwa na topiki ya mwanamke kukatwa na mumewe hapa tarime!!!,mimi kama mwanajf sikuchangia chochote ktk mada ile'
jana mchana nilifika nyumbani kwao ghati chacha kwa ajili ya kumjulia hali maana sasa ametoka hospitalini,kweli nimkuta akiwa ameketi ktk kiti pembeni yake kuna jani la mgomba kwa ajili ya kufukuza mbu walimsumbua.
Ama kweli hujafa hujaumbika,ndugu zangu nishindwa kuyazuia machozi kwa hali niliyomkuta nayo yule binti mrembo.niliongea naye kwa muda wa masaa2 baadaye nikaondoka zangu.
kwa mujibu wa maelezo yake alisema yeye hakuwa na ugomvi wowote na mumewe chacha mwita. siku ya tukio walipotoka shambani ghati alipika wakala wote kisha mumewe akaaga kwenda sokoni na kaahidi angerudi baada ya muda mfupi lakini hakurudi mchana ule mpaka ilipofika saa 2 usiku alirudi akiwa amelewa na akagonga mlango huku akimuuliza ghati nani amekuoa hapa nyumbani?ghafla maskini akampiga na panga kichwani akaanguka chini na akaanza kumkata mguu wake hadi kautenganisha kabisa(picha ya kipande cha mguu ninayo,niliipata polisi jana).naye pia nilimpiga picha.
Tangu siku ya tukio mumewe yupo ndani ila kuna tetesi kuwa ndugu zake wana mpango wa kumtoa jela.
katika kipindi hiki ghati anakabiliwa na changamoto mbalimbali ukosefu wa pesa maana kwa muda huu alitakiwa awe bugando hospital kama alivyoshwauriwa na madaktari wa hospital ya wilaya tarime.
kibaya zaidi anaambiwa na ndugu za mumewe kuwa amesababisha ndugu yao kafungwa na anateseka jela kwa ajili yake.
Baada ya maelezo marefu bila shaka mmeelewa hali ya ghati ikoje mpaka sasa.
kama wiki 2 zilizopita hapa jf kulikuwa na topiki ya mwanamke kukatwa na mumewe hapa tarime!!!,mimi kama mwanajf sikuchangia chochote ktk mada ile'
jana mchana nilifika nyumbani kwao ghati chacha kwa ajili ya kumjulia hali maana sasa ametoka hospitalini,kweli nimkuta akiwa ameketi ktk kiti pembeni yake kuna jani la mgomba kwa ajili ya kufukuza mbu walimsumbua.
Ama kweli hujafa hujaumbika,ndugu zangu nishindwa kuyazuia machozi kwa hali niliyomkuta nayo yule binti mrembo.niliongea naye kwa muda wa masaa2 baadaye nikaondoka zangu.
kwa mujibu wa maelezo yake alisema yeye hakuwa na ugomvi wowote na mumewe chacha mwita. siku ya tukio walipotoka shambani ghati alipika wakala wote kisha mumewe akaaga kwenda sokoni na kaahidi angerudi baada ya muda mfupi lakini hakurudi mchana ule mpaka ilipofika saa 2 usiku alirudi akiwa amelewa na akagonga mlango huku akimuuliza ghati nani amekuoa hapa nyumbani?ghafla maskini akampiga na panga kichwani akaanguka chini na akaanza kumkata mguu wake hadi kautenganisha kabisa(picha ya kipande cha mguu ninayo,niliipata polisi jana).naye pia nilimpiga picha.
Tangu siku ya tukio mumewe yupo ndani ila kuna tetesi kuwa ndugu zake wana mpango wa kumtoa jela.
katika kipindi hiki ghati anakabiliwa na changamoto mbalimbali ukosefu wa pesa maana kwa muda huu alitakiwa awe bugando hospital kama alivyoshwauriwa na madaktari wa hospital ya wilaya tarime.
kibaya zaidi anaambiwa na ndugu za mumewe kuwa amesababisha ndugu yao kafungwa na anateseka jela kwa ajili yake.
Baada ya maelezo marefu bila shaka mmeelewa hali ya ghati ikoje mpaka sasa.