Mimi katika maajabu yote yaliyonishangaza na ambalo sijawahi kulisikia tangu Tanzania iumbwe ni suala la serikali kukosa pesa kabisa ya dharula kwa wahanga wa tetemeko huko Kagera, wakati kuna kitengo cha maafa na majanga chini ya ofisi ya w/Mkuu.
Na ajabu zaidi bajeti imepitishwa mwezi wa sita tu hapo kwa mbwembwe nyingi, kumbe ni bajeti hewa hakuna chochote, pesa ziko kwenye makaratasi, hazina hakuna.
Na hakujatokea janga tangu bajeti ipitishwe pengine wangetudanganya kuwa pesa za maafa na majanga zimetumika ktk janga flani, la Kagera ndo janga la kwanza kutokea tangu bajeti ipitishwe na hakuna hela ya dharula ya kuwasaidia wahanga, ni maajabu sana kwangu.