Uozo wa UWEZO na TWAWEZA

Kinega Michapo

New Member
Apr 15, 2013
1
0
Ni mwaka wa nne huu Asasi za Uwezo na Tweweza zimekuwa zikifanya tathmini ya stadi kuu za kusoma na kuhesabu kwa lugh zote mbili za kiingereza na Kiswahili. Utafiti huu hufanywa na watu wanaochaguliwa na kupewa cheo cha Uratibu wa wilaya (DC). Uoza wa tafiti yao hii kuanzia ukusanyaji wa data hadi matokeo yanayotangazwa kwa Watanzania unakuja kutokana na upatikanaji wa hao waratibu wa wilaya ambao ndiyo wanaoenda kusimamia zoezi zima la kukusanya taarifa zinazohitajika kwa kupitia watafiti wa kujitolea.

Asilimia 90 ya hao waratibu wa wilaya, na kwa mwaka huu wameongezwa wa mikoa hawana sifa zinazoendana na aina ya zoezi hilo na kazi yenyewe ya utafiti huo. Waratibu hawa wa wilaya na mikoa hupatikana kwa njia za ajabu zisizojali merit factor, usishangae umekaa kijiweni nukapigiwa simu "kesho njoo Morogoro kwenye semina, tafuta na marafiki zako watatu uje nao" bila ya kujali elimu, uwezo wa hao watu na sifa zao.

Waratibu hao wa Wilaya na mikoa wengi wao ni waalimu wa upe na diploma holders tena za ualimu. Cha ajabu tayari Uwezo/Tweweza ilishatangaza nafasi hizo za uratibu wa Wilaya na Mikoa na kutaja kuwa sifa ya kielimu ni lazima uwe na Degree kwenye masomo ya Sayansi ya Jamii, kizuri zaidi watu wenye kiwango hicho cha elimu wameomba tena kwa wingi tu.

Wachache walifanyiwa usaili kwa njia ya simu na wengi wao hawajafanyiwa usaili na hao wachache waliofanyiwa usaili kwa njia ya simu wengi wao hawajaitwa na badala yake, Waratibu wenye uzoefu ndiyo wanapewa jukumu la kuwaunganishia kazi hiyo washkaji zao kwa kushirikiana na viongozi wa Uwezo kwa ahadi ya kuwatoa kirushwa hao viongozi wa Uwezo/Twaweza.

Watu hawa ndiyo tunaotarajia waende vijijini kufanya ama kusimamia zoezi hili, lakini tangu wanaingizwa kwenye timu ya Waratibu tayari washaandaliwa mazingira ya CCM yaani Chukua Chako Mapema. Si ajabu mtaribu akajifungia chumbani kwake na washkaji zake watatu wakamaliza kujaza madodoso 30 ukatembezwa mgao watu haoo! Halafu kesho Uwezo inatoa taarifa za uongo kwa Watanzania.

Hakuna mratibu anayeweza kumsimamia mwenzake iwe wa Wialaya au Mkoa ikiwa wote wamemegeana pande la hiyo kazi, unless watakaa pamoja na kujadiliana jinsi ya kuchakachua mshiko na kufichiana siri tu. Twaweza wana jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa waratibu hawa wote wa Wilaya na Mikoa kwa kuangalia upya sifa zao, ila wasishangae watakapojikuta wana waratibu ambao ofisi haina taarifa zao maana walitoka kwao baada ya kupigiwa simu jana na kwenda direct kwenye kwenye mafunzo bila ya kuomba nafasi hizo za kuwatumikia Watanzania.

Kwa uzoefu wangu hata kama na mimi ni mmoja wa waratibu kwenye zoezi hili, lakini sijawahi na sitawahi kuja kuwa na imani juu ya matokea ya tafiti hii ya Uwezo mpaka pale watu sahihi waliomo ndani watakapochanganywa na watu sahihi walioachwa watakapopewa jukumu la kuifanya kazi hii hata kama ni ya kujitolea.
 
Nayo issue!
Wizara ya Elimu au moja ya vyuo vikuu vifanye evaluation ya tafiti zao kwa kuangalia sample ya eneo mojawapo kwaajili ya kuverify ukweli wa taarifa zao.
 
kwa hiyo wewe diploma ya ualimu umeidharau kiasi kwamba unaiita ''diploma tena ya ualimu''.. Thats why mungu aliwaonesha njia wakakupiga chini...kwanini wewe usiwe miongoni mwa hao washikaji... Pathetic..
 
kwa hiyo wewe diploma ya ualimu umeidharau kiasi kwamba unaiita ''diploma tena ya ualimu''.. Thats why mungu aliwaonesha njia wakakupiga chini...kwanini wewe usiwe miongoni mwa hao washikaji... Pathetic..

huyu ameonyesha dharau kaka
 
Nilishawahi kupost humu siku 1 kuhusu hizi research za NGOs na wataalam wetu wengi ni uongo na adulteration tupu..iliwahi kuandikwa et 26.5% ya wanawake wanafanya mapenzi kinyume na maumbile,40% ya watoto sio wa baba zao halisi n.k...
Hayo mnjoos ni majizi tu,kula hela za warangirangi,judrive nice SUVs na kumiliki office maikocheni na masaki..
to hell with their craps..sisomagi wala huwa siziamini..
 
Nimesoma habari za huyu jamaa kwa umakini na nimegundua kuwa:-
-Huyu jamaa alichokiandika NI MALALAMIKO na SI UHALISIA WA HALI ILIVYO. Ameandika kwa HISIA na SI KWA UKWELI.Mtu anapoandika kwa kulalamika maana yake ni kuwa alikuwa na matarajio ya kupata kitu fulani kwa faida yake binafsi na sasa amekikosa.

-Mimi nilikuwa ni mmoja wa waratibu wa wilaya na sasa wa Mkoa.Sijawahi kukutana na hali anayoieleza huyu jamaa. Je, amefanya utafiti wa kina kwa kiasi gani kama kweli zoezi la kubainisha waratibu lilifanyika kwa upendeleo? Mbona haweki wazi ushahidi wake? INAKATISHA TAMAA!!

-Yaonekana hata upeo wake wa kuelewa nini Uwezo na nini Twaweza ameshindwa, je atawezaje kujua kiufasaha yanayotendeka? Uwezo si asasi/taasisi kama alivyoanza kujieleza, hii inaonesha kuwa huyu jamaa ni mtu wa kutunga tunga mambo kwa faida yake binafsi.Sisi tunalitazama Taifa letu na hatima ya kizazi chetu kwenye sekta ya elimu, kwa nini utukoroge?

Mimi naomba wana Uwezo wenzangu-DCs na RCs na wote wenye mapenzi mema tusikatishwe na maneno haya bali yatupe nguvu ya kufanya kazi iliyo mbele yetu kwa kujituma na ujasiri mkubwa.

Venance
 
Duh, hii kali jamaa kajiunga Aprili 15, 2013 baada ya anaowalalamikia kumaliza mafunzo yao Morogoro, na hii ni post yake ya kwanza!!!!

Natoka kwenye moja ya shirika linalofanya kazi na UWEZO katika huo utafiti, DC tuliyewapatia ni msomi wa shahada ya kwanza, akiwa ameshiriki katika tafiti za elimu mbali mbali hapa nchini na ni mtu mwenye heshima yake nchini kutokana na weledi wake.

UWEZO haiwasiliani na watu binafsi bali NGOs zilizoko kwenye wilaya wanakofanya kazi zao, sasa hizo hongo sijui zinatolewaje.

Ni wazi wewe ni mmoja kati ya walioenguliwa mwaka huu kutokana na kuvunda katika kazi ya mwaka jana au ni yule mtoto wake aliyenguliwa kwa kukosa sifa, sasa umekuja na hasira, hivyo uko radhi sasa kubomoa kazi nzima kwa ajili ya maslahi binafsi.

Tafiti za UWEZO ndizo kwa mara ya kwanza zilizofuchua kuhusu watoto kumaliza elimu ya msingi wakiwa hawajui kusoma na kuhesabu, mambo yaliyothibitishwa na ufuatiliaji uliofanywa na mawaziri wenyewe, ni wazi basi ni zoezi lenye tija.

Pole sana.
 
Tunafanyia tathmini ya hizo tafiti. Yote kwa yote, tafiti za Elimu, ikiwemo za HakiElimu, zimekuwa na uhalisia, ikilinganishwa na tafiti za kisiasa, japokuwa serikali imekuwa ikizipinga kupitia methodolojia. Kunaweza kukawa na mapungufu kadhaa, kama ilivyo kwa tafiti nyingine kama zinazofanywa na NBS n.k, japo si rahisi kupelekea tofauti kubwa katika matokeo.
 
Back
Top Bottom