Uongozi wa Awamu ya Tano, Shule Kubwa Kwetu

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,654
41,309
Uongozi wa awamu ya 5, uligubikwa na kila aina ya uovu, kuanzia kwenye mauaji, utekaji, utesaji, ubambikiaji watu kesi, ugandamizaji wa haki, demokrasia na haki za watu.

Watawala waliostahili kuwalinda raia dhidi ya dhuluma wakageuka kuwa wadhulumaji.

Ben Sanane akapotezwa moja kwa moja baada ya kuhoji uhali wa PhD yake.

Azory Gwanda akapotezwa moja kwa moja baada ya kuandika kuwa kulikuwa na mauaji ya watu wasio na hatia kwenye operesheni za Kibiti.

Tundu Lisu akamiminiwa risasi baada ya kutoa angalizo kuwa ukiukaji wa mkataba na Accacia kutasababisha nchi kushtakiwa, na pia kwa kutamka kuwa tulikuwa na rais wa ajabu.


Kuna taarifa pia kuwa Mo alitekwa baada ya kutaka fidia kutokana na ardhi aliyokuwa anamiliki huko Rufiji ambako sasa kungejengwa bwawa la umeme.

Madiwani kupitia CHADEMA wa Dar na huko Morogoro waliishia kuchanjwa na mapanga kama wanyama wa kitoweo.

Kuhoji utendaji wa Serikali au kumkosoa Rais, hiyo ilikuwa ni death penalty au kutekwa.

Waliotakiwa kuunga mkono juhudi halafu wakakataa, baadhi waliishia kwenye mahabusu kwa muda mrefu, wakitafutiwa makosa ya kubambikwa ili wafungwe.

Chaguzi katika maana halisi zikafutwa. Wagombea wa ubunge kupitia CCM, 75% ya waliopitishwa na wajumbe, majina yao yalikatwa na mtu mmoja, na kupachikwa aliyemtaka. Na hao waliopachikwa, wakapewa ubunge kwa agizo lake kwa wakurugenzi, na ikawa hivyo.

Ukikubali kusifu na kuwa msaidizi kwa uovu ulikula mema ya nchi utakavyo na kuwa huru hata kumpora mtu yeyote uliyetaka.


Kutokana na mtu mmoja, nchi ikafutiwa pesa za misaada, kuanzia zile za MCC mpaka za Jumuia ya Madola. Hizi pesa hazikuwa za.mikopo, na ndiyo zilizotumika kupeleka umeme vijijini kwa karibia 75%.

Mwisho wa yote akajitafutia utajiri kwa kuwabambikia kesi za uhujumu uchumi matajiri kwa kuwaweka magerezani kwa muda mrefu, halafu mwishoni akawaambia kama wanataka kuwa huru watoe pesa, na watakaokataa wateswe zaidi. Pesa walizozitoa akazifanya zake binafsi na washirika wake, akiamini kuwa hata siku akitoka madarakani awe na utajiri wa kutosha.

LA KUJIFUNZA

Umetesa watu ili upate pesa. Umewaua wasio na hatia, ukiamini pesa ulizozikusanya siku za mbeleni zitakupa nafasi ya kustarehe kwenye utajiri mkubwa. Je, pamoja na uwingi huo wa pesa, aliweza kuzitumia? Aliweza kustarehe? Jibu ni HAPANA.

Tuliobakia, hata kama tuna madaraka, jamani tuchukue kilicho halali yetu, kupora visivyo vyetu, na kuwadhulumu wengine kwa sababu tu ya uchoyo na tamaa ya utajiri, tusidhani kama ndiyo uhakika wa maisha.

Hata pale tunapotafuta mali, hata kama ni kwa njia halali, utajiri na mali visitupofushe akili na mioyo yetu. Tusifanane na yule wa kwenye andiko hili kwenye biblia:

Luka 12: 13 - 21

13 Na mtu mmoja katika umati akasema, “Bwana, mwambie ndugu yangu anigawie urithi aliotuachia baba yetu.” 14 Yesu akamwambia, Rafiki, ni nani aliyenifanya mimi niwe hakimu wenu au mgawanyaji wa urithi wenu?”

15 Ndipo akawaambia, “Jihadharini na jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana uhai wa mtu hautokani na wingi wa mali aliyo nayo.”

16 Kisha akawaambia mfano, “Shamba la tajiri mmoja lilizaa sana. 17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Maana sina mahali pa kuweka mavuno yangu.’ 18 Kisha akasema, ‘Nitafanya hivi: nitabomoa maghala yangu na kujenga maghala makubwa zaidi na huko nitaweka mavuno yangu yote na vitu vyangu. 19 Na nitasema moyoni, ‘Hakika nina bahati! Ninayo mali ya kunitosha kwa miaka mingi. Sasa nitapumzika: nile, ninywe na kustarehe.’ 20 Lakini Mungu akamwambia, ‘Mjinga wewe! Usiku huu huu utakufa! Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea vitakuwa vya nani?’ 21 Hivi ndivyo itakavyokuwa kwa mtu ye yote anayehangaika kujikusanyia utajiri duniani lakini si tajiri mbinguni kwa Mungu.”

ANDIKO HILO NI KWAAJILI YA TULIO HAI SIYO KWAAJILI YA MAREHEMU.
 
Mauaji yalikuwepo hata awamu wa 4 na ufisadi tu.hapa umejaa chuki Tu na ushamba.

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
Mimi mshamba kwa sababu nachukia uovu? Kwa hiyo uuaji ndiyo ujanja? Yawezekana uuaji na utekaji ni ujanja katika Ulimwengu wa giza.

Kama kuchukia uovu ni ushamba, basi namwomba Mungu anijalie ushamba wa namna hiyo maisha yangu yote.
 
Unatuchosha na tuhuma fikirika za mauaji/kupotea kwa hao uliowataja ukihusisha na Rais wa Awamu ya Tano pasipo ushahidi
Ushahidi, watu watautoa barabarani kama hakuna kesi iliyofunguliwa? Unajua ni nani huwa wanafungua jalada la uchunguzi? Unafahamu ni nani huwa wana mamlaka ya kufungua kesi ya jina mahakamani?
 
Uongozi wa awamu ya 5, uligubikwa na kila aina ya uovu, kuanzia kwenye mauaji, utekaji, utesaji, ubambikiaji watu kesi, ugandamizaji wa haki, demokrasia na haki za watu.

Watawala waliostahili kuwalinda raia dhidi ya dhuluma wakageuka kuwa wadhulumaji.

Ben Sanane akapotezwa moja kwa moja baada ya kuhoji uhali wa PhD yake.

Azory Gwanda akapotezwa moja kwa moja baada ya kuandika kuwa kulikuwa na mauaji ya watu wasio na hatia kwenye operesheni za Kibiti.

Tundu Lisu akamiminiwa risasi baada ya kutoa angalizo kuwa ukiukaji wa mkataba na Accacia kutasababisha nchi kushtakiwa, na pia kwa kutamka kuwa tulikuwa na rais wa ajabu.


Kuna taarifa pia kuwa Mo alitekwa baada ya kutaka fidia kutokana na ardhi aliyokuwa anamiliki huko Rufiji ambako sasa kungejengwa bwawa la umeme.

Madiwani kupitia CHADEMA wa Dar na huko Morogoro waliishia kuchanjwa na mapanga kama wanyama wa kitoweo.

Kuhoji utendaji wa Serikali au kumkosoa Rais, hiyo ilikuwa ni death penalty au kutekwa.

Waliotakiwa kuunga mkono juhudi halafu wakakataa, baadhi waliishia kwenye mahabusu kwa muda mrefu, wakitafutiwa makosa ya kubambikwa ili wafungwe.

Chaguzi katika maana halisi zikafutwa. Wagombea wa ubunge kupitia CCM, 75% ya waliopitishwa na wajumbe, majina yao yalikatwa na mtu mmoja, na kupachikwa aliyemtaka. Na hao waliopachikwa, wakapewa ubunge kwa agizo lake kwa wakurugenzi, na ikawa hivyo.

Ukikubali kusifu na kuwa msaidizi kwa uovu ulikula mema ya nchi utakavyo na kuwa huru hata kumpora mtu yeyote uliyetaka.


Kutokana na mtu mmoja, nchi ikafutiwa pesa za misaada, kuanzia zile za MCC mpaka za Jumuia ya Madola. Hizi pesa hazikuwa za.mikopo, na ndiyo zilizotumika kupeleka umeme vijijini kwa karibia 75%.

Mwisho wa yote akajitafutia utajiri kwa kuwabambikia kesi za uhujumu uchumi matajiri kwa kuwaweka magerezani kwa muda mrefu, halafu mwishoni akawaambia kama wanataka kuwa huru watoe pesa, na watakaokataa wateswe zaidi. Pesa walizozitoa akazifanya zake binafsi na washirika wake, akiamini kuwa hata siku akitoka madarakani awe na utajiri wa kutosha.

LA KUJIFUNZA

Umetesa watu ili upate pesa. Umewaua wasio na hatia, ukiamini pesa ulizozikusanya siku za mbeleni zitakupa nafasi ya kustarehe kwenye utajiri mkubwa. Je, pamoja na uwingi huo wa pesa, aliweza kuzitumia? Aliweza kustarehe? Jibu ni HAPANA.

Tuliobakia, hata kama tuna madaraka, jamani tuchukue kilicho halali yetu, kupora visivyo vyetu, na kuwadhulumu wengine kwa sababu tu ya uchoyo na tamaa ya utajiri, tusidhani kama ndiyo uhakika wa maisha.

Hata pale tunapotafuta mali, hata kama ni kwa njia halali, utajiri na mali visitupofushe akili na mioyo yetu. Tusifanane na yule wa kwenye andiko hili kwenye biblia:

Luka 12: 13 - 21

13 Na mtu mmoja katika umati akasema, “Bwana, mwambie ndugu yangu anigawie urithi aliotuachia baba yetu.” 14 Yesu akamwambia, Rafiki, ni nani aliyenifanya mimi niwe hakimu wenu au mgawanyaji wa urithi wenu?”

15 Ndipo akawaambia, “Jihadharini na jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana uhai wa mtu hautokani na wingi wa mali aliyo nayo.”

16 Kisha akawaambia mfano, “Shamba la tajiri mmoja lilizaa sana. 17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Maana sina mahali pa kuweka mavuno yangu.’ 18 Kisha akasema, ‘Nitafanya hivi: nitabomoa maghala yangu na kujenga maghala makubwa zaidi na huko nitaweka mavuno yangu yote na vitu vyangu. 19 Na nitasema moyoni, ‘Hakika nina bahati! Ninayo mali ya kunitosha kwa miaka mingi. Sasa nitapumzika: nile, ninywe na kustarehe.’ 20 Lakini Mungu akamwambia, ‘Mjinga wewe! Usiku huu huu utakufa! Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea vitakuwa vya nani?’ 21 Hivi ndivyo itakavyokuwa kwa mtu ye yote anayehangaika kujikusanyia utajiri duniani lakini si tajiri mbinguni kwa Mungu.”

ANDIKO HILO NI KWAAJILI YA TULIO HAI SIYO KWAAJILI YA MAREHEMU.
sijawahi kuona watu walevi kama chadema wanakunywa konyagi km mwenyekiti wao na wakilewa wanamuota Magufuli yale jamaa majinga san
 
Chaguzi katika maana halisi zikafutwa. Wagombea wa ubunge kupitia CCM, 75% ya waliopitishwa na wajumbe, majina yao yalikatwa na mtu mmoja, na kupachikwa aliyemtaka. Na hao waliopachikwa, wakapewa ubunge kwa agizo lake kwa wakurugenzi, na ikawa hivyo.
Kazi ya Bashilu.....balozi huyu yuko wapi?
 
sijawahi kuona watu walevi kama chadema wanakunywa konyagi km mwenyekiti wao na wakilewa wanamuota Magufuli yale jamaa majinga san
Kwa hiyo viwanda vyote vya pombe nchini na pombe zote zinazoagizwa toka nje ni kwaajili ya CHADEMA?

Kama kwako pombe ni chakula, kuna wengine kwao ni haramu. Ila mada hii siyo kwaajili ya habari ya pombe. Ni mada kwaajili ya walio hai kwa funzo tulipatalo kutokana na uongoza mbaya wa awamu ya 5 uliokosa hekima ya Mungu.

Omba hekima ya Mungu ili usimchukie mtu bali uovu wake.
 
Umeacha Damage kubwa beyond Repair. Rais wa Sasa itamchukua muda mrefu kurekebisha
Repair, japo itachukua muda mrefu, siku moja itapatikana. Repair pekee ambayo hatutaipata ni maisha ya wenzetu waliopotezwa, na wale waliopewa ulemavu wa kudumu.

Basi Mungu amjalie hekima kuu huyu Rais wa kwanza Mama ili uongozi wake ukawe faraja kuu kwao waliodhulumiwa. Afumbe masikio dhidi ya kelele za wapenzi wa uovu. Daima aitazame na ailinde haki na uhuru wa watu. Mara nyingi Mungu hutenda makuu kupitia watu waliodhaniwa ni wanyonge. Wapo watu, kwa sababu ya mazoea, walidhani nchi itayumba kwa sababu Rais ni mwanamke, lakini mwanga unaonekana, amani na furaha miongoni mwa watu wema inazidi kudhihirika.
 
Back
Top Bottom