jerrytz
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 5,960
- 4,209
we
Wewe una degree ya uzamivu kwenye kutunga uongo. Nimekukubali aisee
Wenzangu habari bwana,
Mapenzi mapenzii yanahitaji ubunifu Na ujanja, kwanza ukitaka kuya mantain mapenzi yako uwe muongo yaan si uongo mbaya hapana ule wa kukuokoa mazingira uliyobanwa Na mwenzako anapohisi sintofahamu.
Sasa bwana mimi nimedanganya sanaaa Na nika win Sijawahi kamatwa, au shutukiwa.
Nikiwa shule ya sekondari makongo nilikipata kidemu Cha IFM nikakidanganya nami niko chuo, kumbe niko zangu form 5, sasa akapanga aje kunitembelea chuoni duhhh sasa hapo.
Nikabeba kitabu Cha michoro michoro nikaenda kwenye vimbweta vya ardhi university (UCLAS) kipindi hicho, nikamsubiri nje pale akaja tukapiga stori hadi noma, akaondoka, lakin safari zake nyingi zikawa mlimani city, nikapanga siku akiniona natoka Makongo nasema nafundisha tuition kule, sema huyu alitaka hela sana siku za boom lao ananiomba hela wakati mimi sina, nikamwambia nasomesha wadogo zangu, Ila tuliachana.
Mwingine sasa duh Alikuwa classic sana kipindi nimemaliza chuo sina kazi, si unajua wanaume hatutati kujishusha? Nikamualika aje sehem tupate kinywaji, kabeba na ndugu Zake watatu wakati sina hela ya kutosha wakaanza kuagiza Na katimu kake ka basketball, nikamwambia baby nisubirie niweke simu chaji naja, dah ninaenda kibandani nikaiweka rehani bwana wakaniongezea 40,000 maana ilikuwa NOKIA N70, nikaja nikalipa nikajiona mjanja kumbe natoboa mfuko.
Ya tatu hiiiii akataka aje napopanga mabonde kwinama, ilibidi niende kuazima room kwa mshikaji, alafu nikajifanya kila kitu najua kilivyo pale, akataka kupika akaanza kuuliza vitu sasa heheeee duh mpaka nitume mesej kwa alonipa room anielekeze, Ila nika win.
Ushauri kwa madada Na makaka
Kwanza mapenzi ya kupretend ni waswas utatoboka mpaka baasi.
Wadada pia ninyi mnadanganywa sana japo nanyi hamjambo sana,
Je wewe umekumbuka uliwahi kumdanganyaje wa kwako?
Tuambie tujue hapaa
Wewe una degree ya uzamivu kwenye kutunga uongo. Nimekukubali aisee