Ungekuwa wewe ungefanyaje?

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,793
Reaction score
5,042
Kuna mwanamke wa Uganda nilitokea kumpenda sana kazini kwetu, na kwa bahati nzuri nikampa ukweli wangu lakini maskini ya Mungu akanipotezea. Nilijaribu njia nyingi kumfanya anipende lakini alikataa kabisa

Ila akatokea kumpenda Mhispania fulani hivi ambaye tunafanya naye kazi hapo kazini. Nikaona siyo kesi acha ni potezee tu, labda siyo riziki.

Sasa leo tulikuwa kwenye mapumziko, nilikuwa nimeweka 'headphones' masikioni kwangu, lakini nilikuwa sisikii mziki, wao wakafikiri mimi nasikiliza muziki. Nikaskia huyo mwanamke akawa anamwambia huyo mwenzake kuwa mimi nina tabia za kishamba sana.

Aliongea maneno mengi ya kunidharaulisha kwa huyo mpenzi wake. Nilivyokwenda kumwambia ukweli, ananijibu jeuri kuwa sina cha kumfanya!

Ungekuwa wewe ungefanyaje?
 
Achana naye we chapa kazi tu. Fainali uzeeni
 
"Kuna demu wa kiuganda nilitokea kumpenda saana kazini kwetu
Na kwa bahati nzuri nikampa ukweli wangu lakini maskini ya Mungu akanipotezea
Nilijaribu njia nyingi kumfanya anipende lakini alikataa kabisa" jifunze ku balance shobo mq.un..d wewe(sorry)
 
Sasa baba hapo unataka umfanye nn??[emoji28]

We palepale alipomaliza kuongea ungemwambia tu sio kumfuata pembeni, ataona umechukulia advantage hilo swala kumuweka kati akubali [emoji28][emoji28]

Pole sana mkuu
 
tulia endelea na mitikasi yako Wewe Ni bora sana kwa ajili yako binafsi
 
Achana naye huyo binti, fanya kilichokupeleka hapo, Huyo mwingine umemtukana sababu gani? Alikuwa anakusema naye? Au ndo tabia za kishamba unazo? Kosa lake nn?
 
Wewe unaenda kuvamia mtumbwi alafu unakuja kuomba huruma ya wananchi, kama ulijua ana msenge mwenzie ulimshobokea ili nini kama sio ushamba, unakuja kutupotezea muda na kujaza seva za watu
 
Kuna watu sijui wa najikuta kina nani hapa dunianj
 
Cool down brother, silence is the best answer for fools, ukishindana na mwanamke wew ndio umeshindwa just let her be and keep ur standards.
 
Mkuu kwisha yaani unahangaika na huo ujinga ilihali ushatoka eneo la tukio ?

Embu kuwa mwanaume songa mbele achana na mambo ya kitoto rafiki.
 
"Kuna demu wa kiuganda nilitokea kumpenda saana kazini kwetu
Na kwa bahati nzuri nikampa ukweli wangu lakini maskini ya Mungu akanipotezea
Nilijaribu njia nyingi kumfanya anipende lakini alikataa kabisa" jifunze ku balance shobo mq.un..d wewe(sorry)
Mnge.se huyu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…