Unazikumbuka enzi za Barua!

jamani kuna vitu flani vilikwepo zamani vilikuwa raha sana mojawapo ni hili la barua. kuna jamaa mmoja alikuwa anasoma ttc matogoro pale songea miaka ya 84&85 jamaa alikuwa anafukuzia sista angu mitaa ya mabatini pale jirani na chuo. jamaa bana alikuwa anacharaza barua si mchezo anaandika hata mara tatu kwa siku basi anakuja uwanjani ttc pale ananikuta nacheza mpira wakati huo niko std four kwenye bahasha anaweka sh ishirini za noti zile mbili basi mie nafungua barua natoa moja nyingine napeleka kwa sister, sista anavuta ile mbau anakauka. km miezi mitatu imepita jamaa hakijapata jibu one day likaja home eti linalazimisha majibu basi sister akakusaaanya barua zote akazichoma moto yale majivu akaweka kwenye bahasha akanipa nikampelekea jamaa alinitoa baruu akatukana huyooo nikazama home. two weeks later niko kwa class tunaambiwa kuna walimu wa mazoezi wamekuja wanatambulishwa na jamaa yupo si alikuwa mwanafunzi chuoni sasa wamekuja kufanya BTP, nilitetemeka ila tukaishia kumwita mwalimu majivu baada ya kuwapa story washkaji class. hizo ndo barua bana
 
Nilishawahiandikiwa barua lakini niikumbukayo mpaka leo ni ile niliyoipokea nikiwa chuoni...........mwandishi alitumia peni za rangi zote nne, nyeusi, kijani, nyekundu, purple na blue..............hayo maneno aliyapanga yakapangika ...............It impressed me kwa kweli sema tu nilikuwa bado kinda na naive kimapenzi sikuwezajiuliza wala baini what it meant kwa Mkaka mzima wa mwaka wa tatu kumuandikia binti wa mwaka wa kwanza barua kama ile........... niliichukulia juu juu tu kuwa alikuwa domo zege ........but kaka wa watu hakuwaga hivyo. Nway everything happens for a reason..........


hahahahah lohhh
hizo rangi zimenipa rahaa sana kwa kweli mmmhh
 
barua zilikuwa zina raha sana nakumbuka nilikuwa najifungua masaa mawili kuandika barua na baada ya kuifunga ukishenda kuiposti unahakikisha imeingia vizuri kwenye kile kibox ili mtu hasije kusema hajaipata. Na ukishaituma tu unakuwa makini kusikiliza barua zinaposomwa shuleni na ukitajwa unafurahi kupita maelezo. Nakumbuka kuna dada mmoja alikuwa anasoma Kibosho Girls enzi hizo kibosho girls kibosho girls kweli unaambiwa nilikuwa nikipata barua yake naoga kabisa napanda kwenye double decker juu shuleni naisoma mara kumi. Kuna siku alinitumia picha yake kavaa kishati kitovu kinaonekana unaambia nilidata sikusoma siku tatu kila mwalimu akiingia darasani akiwa anaandika ubaoni mie naichungulia ile picha mpaka ukachakaa kabisa ndani ya wiki

Mnakumbuka stempu za kufoji, mtu unasugua stempu kichwani kuondoa ule muhuri wa posta halafu unaitumia stempu hiyo hiyo kumwandikia barua mtu mwingine, halafu posta wakiishtukia inarudishwa kupitia address uliyoondika
mkuu hapo umeniua kabisa duh
 
Sijui kwa nin shirika la posta serikali inaliua, Barua/posta ndio means muhm ya mawasiliano kiofisi! Writen documents km 1 ya principle za bureaucracy inapatikana posta
 
Sijui kwa nin shirika la posta serikali inaliua, Barua ndio means muhm ya mawasiliano!
Serikali haijaliua shirika la posta; ni maendeleo ya teknolojia - introduction ya mobile phones (kumbuka hata handsets za sh 10,000 zipo) ndiyo imefanya umuhimuwa posta kupungua sana. Kwa ninimtu aandike barua wakatianaweza kumpigia simu huyo ambaye angemuandikia barua?! Barua zimebaki za kiofisi tu.
 
Serikali haijaliua shirika la posta; ni maendeleo ya teknolojia - introduction ya mobile phones (kumbuka hata handsets za sh 10,000 zipo) ndiyo imefanya umuhimuwa posta kupungua sana. Kwa ninimtu aandike barua wakatianaweza kumpigia simu huyo ambaye angemuandikia barua?! Barua zimebaki za kiofisi tu.

kwa hiyo barua ina umuhimu au hizi teknolojia zetu???
 
Yaani hizi barua nazo, zilikuwa zinaleta kesi sana majumbani mwetu. unajaladia daftari then unaificha humo mara mama ako anaigundua au mwalimu hakuna rangi utaacha ona
 
Yaani hizi barua nazo, zilikuwa zinaleta kesi sana majumbani mwetu. unajaladia daftari then unaificha humo mara mama ako anaigundua au mwalimu hakuna rangi utaacha ona

haha ha ha ni kweli kabisa mama aliwah tandika vidole alipokuta kimsg cha fatuma wangu nkiwa drs la 6 na skuli akaja tukakungutwa tena ndo -+ za barua!
 
Kwani mmesahau enzi za vistika vyenye ujumbe wa mapenzi vilivyokuwa vinabandikwa kwenye barua iliyoandikwa kwenye karatasi ya maua maua ambayo ilikuwa lazima ichombezwe na dedication ya wimbo wa blues au RnB toka Marekani bila ya kujali kuwa huko boarding ulipo wala huwezi kuusikiliza huo wimbo labda mpaka urudi home wakati wa likizo.
 
Kwako Dena Amsi, Utakapokujua hali yangu mimi na wana JF ni bukheri wa Afya. Hofu ni kwako ulie mbali ya upeo wa macho yetu. Kama barafu umeyeyuka hapa JF, tumejaribu kukutafuta kila kona hatujakuona rafiki.&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Nia au madhumuni ya kuandika barua hii ni kutaka kukufahamisha kuwa tunakumiss hapa JF, umepotelea wapi mpenzi au umehamia Face book. Kama tumekukosea tunaomba utusamehe. Au mzee amekuwa mkali siku hizi hataki uonekane hapa JF? Kama kompyuta yako ina Virus tunao wataalam hapa watakusaidia. Mara tu upatapo barua hii tunaomba utumie njia yoyote kutufahamisha wapi uliko. Kama upo kwenye fungate mbona umeondoka bila kutuaga, Jamani dena rudi basi mpenzi wetu.&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Namtuma njiwa akuletee barua hii iliyojaa upendo juu yako&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Wako akupendae&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
GAZETI &amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
wasalam!
&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Ha ha ha wanianza uchokozi weye mie siku hz ni Guest nipo nipo GAZETI nakusoma sana tu
 
&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Ha ha ha wanianza uchokozi weye mie siku hz ni Guest nipo nipo GAZETI nakusoma sana tu

Ok, Ahsante Dena. Ingawa tulikuwa tunatoa mfano tu wa barua za siku zile. Bora umeonekana sasa nimetulia. Nilikuzoea kabla sijawa memba, yaani wewe hapa JF ni kama Messi Kule Barcelona.
 
Ok, Ahsante Dena. Ingawa tulikuwa tunatoa mfano tu wa barua za siku zile. Bora umeonekana sasa nimetulia. Nilikuzoea kabla sijawa memba, yaani wewe hapa JF ni kama Messi Kule Barcelona.
<br />
<br />
Jamani wewe.....mie miss wewe pia
 
Niliwah mtumia dem barua akaniona wakuja et why dont you use emails ?i hate tht shit sentence
 
ndo mana kuna kitu kinaitwa GENERATION.ukilijua hilo hutalishangaa hilo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom