Chimunguru
JF-Expert Member
- May 3, 2009
- 10,678
- 4,351
jamani kuna vitu flani vilikwepo zamani vilikuwa raha sana mojawapo ni hili la barua. kuna jamaa mmoja alikuwa anasoma ttc matogoro pale songea miaka ya 84&85 jamaa alikuwa anafukuzia sista angu mitaa ya mabatini pale jirani na chuo. jamaa bana alikuwa anacharaza barua si mchezo anaandika hata mara tatu kwa siku basi anakuja uwanjani ttc pale ananikuta nacheza mpira wakati huo niko std four kwenye bahasha anaweka sh ishirini za noti zile mbili basi mie nafungua barua natoa moja nyingine napeleka kwa sister, sista anavuta ile mbau anakauka. km miezi mitatu imepita jamaa hakijapata jibu one day likaja home eti linalazimisha majibu basi sister akakusaaanya barua zote akazichoma moto yale majivu akaweka kwenye bahasha akanipa nikampelekea jamaa alinitoa baruu akatukana huyooo nikazama home. two weeks later niko kwa class tunaambiwa kuna walimu wa mazoezi wamekuja wanatambulishwa na jamaa yupo si alikuwa mwanafunzi chuoni sasa wamekuja kufanya BTP, nilitetemeka ila tukaishia kumwita mwalimu majivu baada ya kuwapa story washkaji class. hizo ndo barua bana