Unaweza kumsomesha mchumba wako?

Unaweza kumsomesha mchumba wako?

Brigedia Chan-ocha

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2014
Posts
1,353
Reaction score
2,849
Wana JF.

Napenda kupata maoni na mawazo mbali mbali toka kwenu, unaweza kumsomesha mchumba wako wa kike for instance, chuo cha ualimu au Nursing? hawezi kukusaliti baadae akisha pata kazi au akiwa huko?

Huwa nasikia kuwa kuna watu wengi sana walishatendwa wakati au baada ya kusomesha.

Maoni yako ni muhimu sana hapa.
 
Nishasomesha wawili na wote walizingua baadae ila kuwasaidia kwangu kusomesha hakukua na nia kwamba lazima awe na mimi. Na ukiachia kunisumbua kwao kunitaka, tuko kirioho safi. Kwenye swala la mapenzi, usifanye kitu kutegemea malipo, fanya kwakua unampenda, ukifanya hivyo hutaajutia lolote.
 
Unaogopa tu kumsomesha? Kuna watu wametoa vikuu zaidi ya hivyo na kumwagwa vile vile. Ndoa sio kombe kusema unamzawadia mtu.
 
Wew wekeza tu mkuu kwa moyo mmoja kama unavyomsaidia nduguyo malipo kwa mungu
 
Unaogopa tu kumsomesha? Kuna watu wametoa vikuu zaidi ya hivyo na kumwagwa vile vile. Ndoa sio kombe kusema unamzawadia mtu.
Hakuna zawadi inayoshinda elimu... mtu akiamua kukupeleka shule kakupa zawadi kushinda zote...
..ila nawe ukimpeleka mtu shule usitegemee malipo, fanya kwa ubinadam..
 
Kwani wewe kuna malipo unayatarajia baada ya kumsomesha?? Ukiwaza malipo tu imekula kwako, we toa msaada kama unasaidia mtu mwingine yoyote especially ndugu yako. Hii itakusaidia pindi pakitokea jambo litakalokwenda kinyume na matarajio yako, hutaumia.
 
Msomeshe kama msaada ila usimsomeshe ili eti uje kumuoa,
ikitokea sawa ila Maisha yanabadilika sana!
 
Mchumba ? NO ! Wanawake ni watu wabaya sana tena sana tena sana. Hawastahili kusaidiwa hata kidogo na ni wasaliti namba 1, kukubwaga ni jambo dogo sana na huwa hawakumbuki wema wala ihisani.

Let them go to hell.🐜
 
Wana jf.

Napenda kupata maoni na mawazo mbali mbali toka kwenu, unaweza kumsomesha mchumba wako wa kike for instance, chuo cha ualimu au Nursing? hawezi kukusaliti baadae akisha pata kazi au akiwa huko?

Huwa nasikia kuwa kuna watu wengi sana walishatendwa wakati au baada ya kusomesha.

Maoni yako ni muhimu sana hapa.

Onja sumu tu
 
nimeshuhudia mwalimu wangu akisomesha kuanzia form one mpaka form four kwa makubaliano ya kuja kuweka mzigo ndani,

baadae mtoto wa watu akaonja matunda mema ya nje, akamruka mwalimu wangu wa soil profile maneenah zake,

mwalimu mpaka leo anaugulia makato ya mshahara aliyotumia kama ada....

dickhead.... wanawake ni kama biashara, usipokuwa na insurance unaumia mazima kabisa..!

dont trust too much, ndio maana wengine kwanza wanatiwa mimba na kuzalishwa ndio wanaanza sasa kusomeshwa
 
Kwani wewe kuna malipo unayatarajia baada ya kumsomesha?? Ukiwaza malipo tu imekula kwako, we toa msaada kama unasaidia mtu mwingine yoyote especially ndugu yako. Hii itakusaidia pindi pakitokea jambo litakalokwenda kinyume na matarajio yako, hutaumia.

ok poa poa regards
 
nimeshuhudia mwalimu wangu akisomesha kuanzia form one mpaka form four kwa makubaliano ya kuja kuweka mzigo ndani,

baadae mtoto wa watu akaonja matunda mema ya nje, akamruka mwalimu wangu wa soil profile maneenah zake,

mwalimu mpaka leo anaugulia makato ya mshahara aliyotumia kama ada....

dickhead.... wanawake ni kama biashara, usipokuwa na insurance unaumia mazima kabisa..!

dont trust too much, ndio maana wengine kwanza wanatiwa mimba na kuzalishwa ndio wanaanza sasa kusomeshwa

good advice, will be considered well!
 
Kumsomeshaje?


  1. Kutoa poketi mane
  2. Kulipia ada
  3. Kumfanyia mitihani
​

​Wanaume tuna mambo......
 
Wana jf.

Napenda kupata maoni na mawazo mbali mbali toka kwenu, unaweza kumsomesha mchumba wako wa kike for instance, chuo cha ualimu au Nursing? hawezi kukusaliti baadae akisha pata kazi au akiwa huko?

Huwa nasikia kuwa kuna watu wengi sana walishatendwa wakati au baada ya kusomesha.

Maoni yako ni muhimu sana hapa.

Ukisikiliza ya watu huwezi fanya lolote la kimaendeleo hata ndoa haiwezi kuwepo! Kila mtu atakuja na mawazo yake. Fanya maamuzi yako binafsi ! Kama una uwezo wa kusomesha fanya hivyo kwa moyo mweupe ila akili itune kama unatoa msaada na si kutegemea payback in future! Haiwezekani wewe uendelee kujiendeleza kielimu halafu mchumba ako yuko home! Atapata wa kumsomesha ubaki unalia!


Mimi nilichukua jukumu la kumsomesha mchumba angu kwa level ya Diploma, akiwa mwaka wa pili tulifunga ndoa akawa mke halali, kwa sasa tunaishi hapily life tukiwa familia ya watu watatu.

Investment ya kielimu kwa mke wangu inanifanya niwe na imani kuwa hata nikifa leo atakuwa na angalau uwezo wa kuendesha maisha na kumpa malezi mazuri binti yetu! Mambo yakikaa vizuri tena nampeleka shule! Suala kutendwa najua lipo lakini halinizuii kumpa elimu! KAMA UNAJUA MAANA YA ELIMU KWA MWENZI WAKO UTAMSOMESHA! Endapo mambo yatabadilika endelea na maisha yako hilo litabaki kwenye kumbukumbu yake!
 
BIG NO, Si kweli, mimi nina wadogo zangu 2, wote walisomeshwa na wachumba na wakaolewa nao, ni tabia tu ya mtu + malezi
 
Mchumba ? NO ! Wanawake ni watu wabaya sana tena sana tena sana. Hawastahili kusaidiwa hata kidogo na ni wasaliti namba 1, kukubwaga ni jambo dogo sana na huwa hawakumbuki wema wala ihisani.

Let them go to hell.

Hili swala huwa najiuliza sana, unaweza umuokoe mwanamke kutoka kwenye kaburi lakini akishafika sehemu salama anakusahau kama hajawahi kukuona vile.
 
Back
Top Bottom