Unawafahamu Vipi Wairani?

Unawafahamu Vipi Wairani?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,471
Reaction score
33,012
UNAWAFAMU VIPI WAIRANI?

Vita vya Iran na Israel vimevuruga ratiba yangu ya kazi kwani muda wangu mwingi unakuwa katika kufuatilia vita hivi katika vyombo vya habari mashuhuri ulimwenguni – Al Jazeera, CNN, BBC, Fox News halikadhalika nafuatilia katika media nyingine si maarufu kama hizo lakini zina mengi ya ‘’maana’’ mtu anaweza kujifunza hasa katika somo la ‘’propaganda.’’

Vyombo hivi vya habari visivyorusha mabomu ni mstari wa mbele katika mapambano haya ya silaha.

Hili ni jeshi bila silaha.

Vyombo hivi vinatumika kwa njia ya ujanja sana kupiga vita upande ule ambao wao wanauona ni wa adui yao na kwa kufanya hivyo kuutia nguvu upande ambao wao wanaupenda.

Iran na Sudan ni katika nchi ambazo mimi nimefika na ninaweza kusema kitu.

Yemen nimefika lakini sitaizungumza hapa.

Iran na Sudan ni katika nchi duniani ambazo ni ‘’pweke’’ zimetengwa na dunia.

Iran na Sudan zimetengwa kwa sababu ya Uislam wao.

Iran na Sudan nchi hizi mbili kwa hivi sasa zote zinakabiliwa na vita.

Iran inapigana na Israel na Marekani na Sudan wako katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Historia ya kale ya nchi hizi inasisimua.

Nini nimekiona Sudan ambacho kimebaki katika kumbukumbu yangu?

‘’Masjid Kabir,‘’msikiti mkubwa uko mjini Khartoum ambao msikiti mzima baada ya sala kuna darsa watu wameweka duara wanasoma.

Naogopa kukupa hesabu ya darsa hizo lakini ni watu wengi wa kukustaajabisha ikiwa wewe ni mgeni.

Lakini starehe utaipata Masjid Kabir, Sala ya Fajr usikilize, ‘’Kiraa.’’

Imam hana haraka.

Siwezi kueleza yote itahitaji kuandika kitabu.

Wasudani wana msemo wanasema, ‘’Sisi hatupendwi na dunia nzima sisi tunapendwa na Allah.’’

Hili linawatosha.

Nimeingia Tehran na Emirates, Al Fajr.

Kitu kilichonishtua ni kuwa uwanja wa ndege nimeukuta mtupu una watu wachache sijapata kuona kote duniani nilipopita.

Kawaida ni kuwa viwanja vya ndege muda wote vimejaa watu.

Uwanja wa Tehran nimeukuta umetulia, tuli.

Mtupu hakuna watu wengi.

Ninachokisikia ni Qur’an inasomwa katika vipaza sauti.

Barabarani nikaona picha nyingi za watu zimewekwa mfano wa matangazo ya biashara ambayo hapa kwetu yametundikwa katika ‘’billboards’’ yakitangaza kila aina ya bidha kuanzia pombe hadi vitu vingine, matangazo mengi yakiwa na picha za wanawake warembo.

Nilipowauliza wenyeji wangu hizo picha katika barabara za Tehran ni za nani wakaniambia hao ni mashahidi waliouliwa katika njia ya Allah.

Siwezi kuandika yote.

Natokea Berlin na Egypt Air narudi Dar es Salaam.

Mwezi wa Ramadhani niko Uwanja wa Ndege Cairo nasubiri ndege kurudi Dar es Salaam.

Niko transit na nimekuta watu wengi wake kwa waume wamevaa Ihram wanakwenda Umra katika Mwezi wa Ramadhani.

Abiria tuliofunga tunasubiri Adhana tufungue.

Vipaza sauti vilivyoko hapo uwanja wa ndege vinapiga miziki kwa fujo kama vile ni mwezi wa kula mchana.

Huu ni Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Cairo.

Nimetoa radio yangu na kuipitisha FM Station zote zilizoingia kutafuta Qur’an ili ikifika wakati wa kufungua nisikie Adhana.

Hakuna kitu.
Napokelewa na miziki ya kila aina.

Nikajisogeza kwenye mgahawa na kuuliza muda gani wa kufungua?

Wakanifahamisha na pia kunionyesha menu.

Naangalia menu.

Muda wa kufungua umefikia.
Hakuna Adhana.

FM Stations zinaendelea na muziki.
 
mimi na wafahamu wa congo,sudani na somaria huko kote nikafate nini
 
Hongera sana Mohamed said!

Angalau wewe unaishi mkuu!Tena unaishi kweli kweli!!

Unaenda nankurudi na unaandika!what a life!

Big up sana mkuu!!
 
Mohamed
Sikubaliani na vita kwasababu ni maisha ya Wanadamu. Ni kweli kwamba kuna vita zinatengenezwa kwa masilahi fulani. Mathalani, Hamas walipovamia Israel Dunia nzima ililaani. Wapalestina wanapouawa kwa mabomu na njaa Dunia kimya. Juzi tu Iran imeshambuliwa Dunia Kimya si kama ilivyokuwa Ukraine.

Kuhusu vyombo vya habari nakubaliana nawe kabisa! Vyombo hasa vya magharibi vinatoa habari kwa masilahi yao. Mfano, kuna TV moja Marekani imewafukuza wale wote walohoji ukatili dhidi ya Wapalestina.

Wenyewe wanasema, kwa uliyoeleza '' I get it'

Kuna upande wa pili usio uongelea kama ambavyo vyombo vya magharibi vinavyofanya.
Sikubaliani nawe kwamba 'Vita ni kwasababu ya Uislamu wao''. Hata kama ni hivyo, mantiki inakataa

1. Saud Arabia ipo busy na Ibrahim accord na Israel. UAE na Nchi zimekaa kimya Wapalestina wakipigwa mabomu na kuuawa kwa njaa . Hakuna hata kikao cha kudanganya au kauli, na kama zipo ni za kujificha uani. Saud Arabia '' at the heart of Islam'' imekaa kimya bila kuongoza jitihada za kuwasaidia Wapalestina. Unawezaje kusema ni suala la Uislam !

2. Iran: Nchi zinazotoa 'logistic' za mashambulizi dhidi yake ni hizi
a. Saud Arabia inasaidiana na Marekani kutoa eneo kwa makazi ya base za Marekani
b. Jordan inasaidia katika kutungua makombora ya Iran na kutoa anag ndege zipite
c. Iraq ina kambi ya US inayotumiwa kwa mashambulizi Iran
d. Qatar ina US base kubwa middle east

Unaposema vita ni kwasababu ya Uislam, mbona mantiki inakataa!!!

JokaKuu
 
Mohamed
Sikubaliani na vita kwasababu ni maisha ya Wanadamu. Ni kweli kwamba kuna vita zinatengenezwa kwa masilahi fulani. Mathalani, Hamas walipovamia Israel Dunia nzima ililaani. Wapalestina wanapouawa kwa mabomu na njaa Dunia kimya. Juzi tu Iran imeshambuliwa Dunia Kimya si kama ilivyokuwa Ukraine.

Kuhusu vyombo vya habari nakubaliana nawe kabisa! Vyombo hasa vya magharibi vinatoa habari kwa masilahi yao. Mfano, kuna TV moja Marekani imewafukuza wale wote walohoji ukatili dhidi ya Wapalestina.

Wenyewe wanasema, kwa uliyoeleza '' I get it'

Kuna upande wa pili usio uongelea kama ambavyo vyombo vya magharibi vinavyofanya.
Sikubaliani nawe kwamba 'Vita ni kwasababu ya Uislamu wao''. Hata kama ni hivyo, mantiki inakataa

1. Saud Arabia ipo busy na Ibrahim accord na Israel. UAE na Nchi zimekaa kimya Wapalestina wakipigwa mabomu na kuuawa kwa njaa . Hakuna hata kikao cha kudanganya au kauli, na kama zipo ni za kujificha uani. Saud Arabia '' at the heart of Islam'' imekaa kimya bila kuongoza jitihada za kuwasaidia Wapalestina. Unawezaje kusema ni suala la Uislam !

2. Iran: Nchi zinazotoa 'logistic' za mashambulizi dhidi yake ni hizi
a. Saud Arabia inasaidiana na Marekani kutoa eneo kwa makazi ya base za Marekani
b. Jordan inasaidia katika kutungua makombora ya Iran na kutoa anag ndege zipite
c. Iraq ina kambi ya US inayotumiwa kwa mashambulizi Iran
d. Qatar ina US base kubwa middle east

Unaposema vita ni kwasababu ya Uislam, mbona mantiki inakataa!!!

JokaKuu
Mohamed
Sikubaliani na vita kwasababu ni maisha ya Wanadamu. Ni kweli kwamba kuna vita zinatengenezwa kwa masilahi fulani. Mathalani, Hamas walipovamia Israel Dunia nzima ililaani. Wapalestina wanapouawa kwa mabomu na njaa Dunia kimya. Juzi tu Iran imeshambuliwa Dunia Kimya si kama ilivyokuwa Ukraine.

Kuhusu vyombo vya habari nakubaliana nawe kabisa! Vyombo hasa vya magharibi vinatoa habari kwa masilahi yao. Mfano, kuna TV moja Marekani imewafukuza wale wote walohoji ukatili dhidi ya Wapalestina.

Wenyewe wanasema, kwa uliyoeleza '' I get it'

Kuna upande wa pili usio uongelea kama ambavyo vyombo vya magharibi vinavyofanya.
Sikubaliani nawe kwamba 'Vita ni kwasababu ya Uislamu wao''. Hata kama ni hivyo, mantiki inakataa

1. Saud Arabia ipo busy na Ibrahim accord na Israel. UAE na Nchi zimekaa kimya Wapalestina wakipigwa mabomu na kuuawa kwa njaa . Hakuna hata kikao cha kudanganya au kauli, na kama zipo ni za kujificha uani. Saud Arabia '' at the heart of Islam'' imekaa kimya bila kuongoza jitihada za kuwasaidia Wapalestina. Unawezaje kusema ni suala la Uislam !

2. Iran: Nchi zinazotoa 'logistic' za mashambulizi dhidi yake ni hizi
a. Saud Arabia inasaidiana na Marekani kutoa eneo kwa makazi ya base za Marekani
b. Jordan inasaidia katika kutungua makombora ya Iran na kutoa anag ndege zipite
c. Iraq ina kambi ya US inayotumiwa kwa mashambulizi Iran
d. Qatar ina US base kubwa middle east

Unaposema vita ni kwasababu ya Uislam, mbona mantiki inakataa!!!

JokaKuu
Nguruvi...
Hapana tatizo.
Una haki na fikra zako.
 
Dini, dini, dini..... Aliyeleta huu ushenzi Africa alituweza sana
 
Mohamed huu ni mnakasha, tatizo liko wapim Sheikh!
Nimetatizika kidogo nahitaji msaada. Kwamba, Wanaoshambuliwa ni Waislam kwasbabu ya Uislam wao! kwa mujibu wako. Nami nauliza kwanini wanaosaidia mashambulizi ni Waislam? Uislam upi unashambuliwa?
Nguruvi...
Nimekujibu katika huo mnakasha.
 
Mohamed huu ni mnakasha, tatizo liko wapim Sheikh!
Nimetatizika kidogo nahitaji msaada. Kwamba, Wanaoshambuliwa ni Waislam kwasbabu ya Uislam wao! kwa mujibu wako. Nami nauliza kwanini wanaosaidia mashambulizi ni Waislam? Uislam upi unashambuliwa?
Wanaoshambuliwa ni Shia muslims. Sunni wakiongozwa na Saudia, washakuwa compromised kitambo.
 
Wanaoshambuliwa ni Shia muslims. Sunni wakiongozwa na Saudia, washakuwa compromised kitambo.
Gagnija,
Hakika viongozi wa nchi za Kiarabu wako kimya.
Watakuwa kimya kwa muda mrefu.

Lakini lipo ambalo halionekani lakini ipo siku litajitokeza.

Mwananchi wa kawaida katika nchi hizi anaungulia ndani
kwa ndani.

Huu ni moto wa makumbi.
Uko siku In Shaa Allah utajitokeza.
 
Gagnija,
Hakika viongozi wa nchi za Kiarabu wako kimya.
Watakuwa kimya kwa muda mrefu.

Lakini lipo ambalo halionekani lakini ipo siku litajitokeza.

Mwananchi wa kawaida katika nchi hizi anaungulia ndani
kwa ndani.

Huu ni moto wa makumbi.
Uko siku In Shaa Allah utajitokeza.
Jambo lililonifurahisha kwenye hii vita ni uwezo wa makombora ya Iran kupenya ngome za ulinzi na kusababisha uharibifu mkubwa kwenye miji ya Israel.

Vita hii isipomalizwa mapema inakwenda kuyavuta vitani mataifa yenye silaha za kinuklia.

Inatisha sana ukizingatia rais wa Marekani alivyo kibaraka wa Uzayuni.
 
Jambo lililonifurahisha kwenye hii vita ni uwezo wa makombora ya Iran kupenya ngome za ulinzi na kusababisha uharibifu mkubwa kwenye miji ya Israel.

Vita hii isipomalizwa mapema inakwenda kuyavuta vitani mataifa yenye silaha za kinuklia.

Inatisha sana ukizingatia rais wa Marekani alivyo kibaraka wa Uzayuni.
Gagnija,
Nimeandika hayo hapo chini siku tatu zilizopita:

''Allah hakika ni muweza.

Naangalia Haifa leo inafanana na mitaa ya Ghaza.
Wayahudi wanatolewa chini ya vifusi kwa wale waliohai.

Nani juzi tu hapa iliyompitikia hata kwa mbali kuwa Israel itajikuta katika hali hii.
Iron Dome imeshindwa.

Taarifa zinasema Israel inaomba msaada Pentagon Waamerika waingie vitani kupigana na Iran.

Pentagon iko katika shinikizo kubwa asubuhi nilipokuwa nasoma taarifa hii Pentagon ilikuwa bado wapo kwenye kikao kirefu.

Suala kubwa wanasema USA itaanzaje katika hali kama hii?

Daud alipokuwa anamkabili Jalut alisoma dua maarufu akimuomba Allah aithibitishe miguu yake ardhini.

Israel inaona mwenye uwezo wa kuwanusuru ni Mmarekani.

Mmarekani bila shaka katatazika anajiuliza.
Kimetokea nini?''

Makala hii fupi niliiweka katika Group moja ambalo nimeona wenzangu
wanafurahia watu kuuliwa Iran.

Niliiweka kuwatahadharisha.

Wameshindwa kustahamili imebidi nijiondoe katika Group hiyo kwani sikupenda
kuwaumiza wenzangu kwa kalamu yangu.
 
nadhani nikiwa rais nitapiga marufuku kujadili maswala ya nchi yeyote nje ya africa ,tujikite kwenye umaskini wa burundi ndo jambo la msingi
 
N
Ozon,
Una uhuru na haki ya kuamini upendacho.
Hakika, nina uhuru na haki kama ulivyo wewe. Hata hivyo, kuamini peke yake hakutoshi, tunaomba utuainishie hoja zako zinazounga mkono ulichokisema. Je, unazungumzia ukweli unaotegemea hoja na takwimu (facts), au ni hisia binafsi? Tunatarajia usaidizi wako katika hili, hasa wewe kama mkongwe na mzoefu katika jukwaa hili, ambaye tumemzoea kwa hoja zenye uzito na maarifa.
 
Udini unakupunguzia ubora wako.
 
N

Hakika, nina uhuru na haki kama ulivyo wewe. Hata hivyo, kuamini peke yake hakutoshi, tunaomba utuainishie hoja zako zinazounga mkono ulichokisema. Je, unazungumzia ukweli unaotegemea hoja na takwimu (facts), au ni hisia binafsi? Tunatarajia usaidizi wako katika hili, hasa wewe kama mkongwe na mzoefu katika jukwaa hili, ambaye tumemzoea kwa hoja zenye uzito na maarifa.
Ozon,
Ukihitaji ushahidi wa kimahakama kwa hakika sina.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom