Unavuta watu wa aina yako

Unavuta watu wa aina yako

Himidini

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2013
Posts
5,534
Reaction score
4,190
^^
Bila shaka wewe si mgeni katika safari ya maisha!
Hata kuwa na uwezo wa kuingia ktk mitandao na kuchangia fikra zako basi ni dalili njema kuwa una ufahamu.
...
Kuna watu katika maisha wanatafuta mafanikio na kama tujuavyo,faraja ya wengi ni kupata ndoa yenye amani upendo na furaha.Hapo ndipo ilipo hamu ya kutafuta pesa,jumba,gari na malengo mengi.
...
Lakini kwa nini hupati mwenza mnaendana nae? Kwa nini siku zote wanaokuja kwako sio wale wanaokufaa mahitaji yako? Kwa nini muda unapita na jamii inakushangaa tu uko pale pale? Maswali ni mengi na majibu hali kadhalika
...
Moja ya jambo usilolizingatia ni kuwa UNAVUTA WATU WA AINA YAKO PASIPO WEWE KUJUA.
...
Saikolojia inasema siku zote,kuna watu ni wepesi kuchangamana na wenzao,wengine husita,huhoji na hata kutopenda makundi.
Ndivyo yalivyo maisha yako,kama una mashaka jikague!
...
Ukipenda kuvaa ovyo ovyo utawavuta watu wa aina yako,Ukipenda kusema kwa usitaarab ndivyo wakuzungukao watakavyosema "fulani mchangamfu",Fulani mwungwana,Fulani hafai,Unataka kumuoa fulani? Achaaa sikushauri n.k
...
Mfano rahisi,kuna watu wanakuja humu Jf kutafuta Mke mwema au Mume mwema,,lakini wanawakosa..mtu anasema 'nataka wa kunigegeda' basi utawavuta wa aina hiyo.
...
UNAVUTA WATU WA AINA YAKO.
Unapochangia jukwaani,unapoishi ulipo,unapokuwa ofisini,bado ukweli unasimama unavuta watu wa aina yako.
Ukiwa mtu wa kuthamini nje ya mtu mf.urefu ufupi,uzuri,mavazi n.k utawavuta wa aina yako.
Ukiwa mtu wa kuthamini ndani ya mtu mf. Busara,utu wema,msimamo na utulivu utawapata wa aina yako.
^^
 
''Show me your friend and I will tell you who you are..'' inawezakua na ukweli ukweli mkuu [MENTION]Himidini[/MENTION]?

^^
Naam ni ukweli,,na hao marafiki wamevutika kwako kwa sababu umewavutia iwe ni nje yako au ndani yako
^^
 
hivi kuna watu sura zao zinafanana na hela jamani eti???????

Dogo here we're talking about characters and not sura ..............!:A S-alert1:


Hence, it's money characterised people ............. ... understand?
 
The world is play ground mzee atakae kaa Sawa Ndio huyo mtacheza nae unawaza ukawa bahili ila super spender akazimika nawewe nawe ukawa huna jinsi!!
 
Ni kweli kabisa Himidini jinsi unavyojiprotray kwa watu ndivyo wanavyokusoma kutokana na tabia zako,mavazi yako,mienendo yako n.k Haileti mantiki yoyote kwamba mtu anayejiheshimu na kujitambua avutie watu wenye tabia chafu...Ukiwa mkarimu na mstaarabu utawavuta wenye hulka hizohizo...
 
Upo sahihi nakubaliana nawewe. shemeji zangu wa Igbo wanasema " NDINACHI" yaani EXACTLY!
 
Avatar yangu watahusika!!Lol majanga

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ni kweli kabisa Himidini jinsi unavyojiprotray kwa watu ndivyo wanavyokusoma kutokana na tabia zako,mavazi yako,mienendo yako n.k Haileti mantiki yoyote kwamba mtu anayejiheshimu na kujitambua avutie watu wenye tabia chafu...Ukiwa mkarimu na mstaarabu utawavuta wenye hulka hizohizo...

Umesema vyema saaaaaana, na ndivyo ilivyohakuna ubishi
 
sio kweli.. mimi binafsi sio mtu wa kuvaa ki-gentlemen, sina busara flani ambazo zinaweza kumfanya mtu avutike kuongea na mimi ila mara kadhaa nishakamatia mademu ambao hata menyewe huwa najishangaa nilivyowatia tunduni.. kuanzia tabia muonekano hata background huwa hatuendani ila ndo' ivo akijaa kesho atarudi tu!

^^
Bado upo palepale..unawavuta wanaotazama nje yako
^^
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom