Unatoa wapi jeuri ya kulewa katikati ya wiki?

Unatoa wapi jeuri ya kulewa katikati ya wiki?

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,606
Salam!

Huwa nashangaa sana katikati ya wiki (j4 mpk Alhamisi) mtu anakunywa pombe mpaka mid night huku akijua kesho saa 1:30 asubuhi anaamkia kazini.

Binafsi nakunywa pombe lakini ni siku mbili tu za wiki yaani Ijumaa na Jmos, na nakesha club au bar! Jumapili sinywi pombe kabisa maana kesho yake naamkia kazini.

Zamani niliwahi kuamka na hang over siku ya juma3, ilinitesa sana kuhudumia watu kazini. Hamna kitu sikipendi kama kuwa na hangover kazini.
 
Tatizo ni kulewa au kunywa?Jeuri ya kunywa Ijumaa na jumamosi unaitoa wapi wakati ni siku za Ibada?
 
Mbinguni ndiyo sehemu ambayo Mungu amewaandalia wanadamu baada ya maisha haya. Jehanum imeandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika wengine wa giza (wale walioasi). So, kwenda mbinguni ni matakwa ya Mungu mwenyewe
Mungu jalia huyu jane lowasa awe mzuri kama Avatar yake.Nitauza majahazi yote niliyonayo ili nimpate
 
Kuna kunywa pombe kulewa na kuna kunywa pombe starehe/kufurahisha mwili, akili, sio katikati ya wiki tu bali mchana wa katikati ya wiki kwenye purukushani za hela huwa tunazimua tu, (who cares??)

Halafu kuna mdau kazungumza juu hapo, sio wote humu tunategemea kukinga mkono mwisho wa mwezi, hatupangiwi.

Mwisho kabisa nawasihi wanywaji/walevi wenzangu tuendelee kula beer tu kwa wingi, uchumi wa hii nchi unatutegemea kwa kiasi kikubwa Sana. 😅

Let's meet at the top, cheers 🍻
 
Uwe unaenda kazini asubuhi au unaenda kwenye biashara yako, pombe siyo kitu kizuri. Mungu anakataza na wanaokunywa wote hawataingia mbinguni. (Jaribuni kutafakari hili wakati mkiendelea kuchangia hii mada iliyoletwa).
Hata wewe hutaingia huko mbinguni....kasome kitabu chako cha imani vizuri ujue kama kinasema sababu ya kuingia huko ni kutokunywa pombe.
 
Sio kila mtu anaingia job asubuhi asubuh kama wewe mkuu..wengine kazi zao ni za shift..so yuko huru kula bia muda wowote.
 
Back
Top Bottom