Unapanda Basi gani kuelekea 2015

Unapanda Basi gani kuelekea 2015

wanasema eti basi la pili ni la kijerumani na la kwanza ni la kichina,yakianza safari,eti wanasema basi la kichina linachoka mapema haliwezi kupanda milima,ila eti hilo la mjerumani mwendo wake ni kama kinyonga na mlima lazima upandwe.

hilo basi la kichina limeshindwa kupanda mlima sekenke ,, abiria wote wameshuka
 
mkuu unakitu unataka kukiweka sawa,ila bado hujakimalizia vyema,hebu tupe darasa hapo kuhusu EATV

Nina maanisha kwamba kwa vile EATV inaangaliwa na vijana wengi na watu wa rika mbalimbali ingekuwa kioo kwa jamii kuwaeleza ukweli watu wa rika tofauti umuhimu wa kuchagua viongozi bora na si bora viongozi.

Ingeweza kuwekeza katika kuielimisha jamii kwa kuwaita watu mbalimbali wenye mawazo chanya kuhusu Taifa letu na si pro vyama ambao wataenda kuelezea uzuri wa vyama vya na ubaya wa vyama vya upinzani.

Ni TV ambayo ingeweza kuwaibua vijana wenye ,maono ambao wangeweza kuwa viongozi wazuri baadaye mfano kuna akina betlehem,The Big show,Mchambuzi na wengine kama hawa ambao wako tayari kutetea utaifa wao.

Hata JF kuna wengi tu ambao wangeweza kuitwa kuielezea jamii yetu nini tunatakiwa kufanya,umuhimu wa vijana kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura na umuhimu wa jamii bila kujali umesoma au haujasoma umuhimu wa kupiga kura ili kuchagua viongozi bora.

Siyo sahihi kwa watanzania kukaa baa au sehemu yoyote kusubiri matokea ya uchaguzi wakati haujaenda kupiga kura ukiulizwa unasema ah nimeona ujinga kwenda kwani mwisho wa siku wataiba kura,sidhani kama watu wengi wakienda kupiga kura ile impact ya kuongeza kura za wizi itakuwa kubwa.

Hilo ndilo wazo langu kaka sina jingine zaidi ya hilo.Labda ulitengeneze vizuri zaidi kuliweka vyema ili lieleweke maana kiswahili ni chetu lakini kuna wakati kinazingua pia.
 
wanasema eti basi la pili ni la kijerumani na la kwanza ni la kichina,yakianza safari,eti wanasema basi la kichina linachoka mapema haliwezi kupanda milima,ila eti hilo la mjerumani mwendo wake ni kama kinyonga na mlima lazima upandwe.

mmmh hilo la kijani si kama guta
 
ACT..Basi makini lenye kasi na kiwango cha hali ya juu.... ACT ndio basi litakalowafikisha watanzania kwenye nchi ya maziwa na asali
ACT ni kama ADC na kuna kiongozi anaongoza vyama vyote viwili
 
Nina maanisha kwamba kwa vile EATV inaangaliwa na vijana wengi na watu wa rika mbalimbali ingekuwa kioo kwa jamii kuwaeleza ukweli watu wa rika tofauti umuhimu wa kuchagua viongozi bora na si bora viongozi.

Ingeweza kuwekeza katika kuielimisha jamii kwa kuwaita watu mbalimbali wenye mawazo chanya kuhusu Taifa letu na si pro vyama ambao wataenda kuelezea uzuri wa vyama vya na ubaya wa vyama vya upinzani.

Ni TV ambayo ingeweza kuwaibua vijana wenye ,maono ambao wangeweza kuwa viongozi wazuri baadaye mfano kuna akina betlehem,The Big show,Mchambuzi na wengine kama hawa ambao wako tayari kutetea utaifa wao.

Hata JF kuna wengi tu ambao wangeweza kuitwa kuielezea jamii yetu nini tunatakiwa kufanya,umuhimu wa vijana kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura na umuhimu wa jamii bila kujali umesoma au haujasoma umuhimu wa kupiga kura ili kuchagua viongozi bora.

Siyo sahihi kwa watanzania kukaa baa au sehemu yoyote kusubiri matokea ya uchaguzi wakati haujaenda kupiga kura ukiulizwa unasema ah nimeona ujinga kwenda kwani mwisho wa siku wataiba kura,sidhani kama watu wengi wakienda kupiga kura ile impact ya kuongeza kura za wizi itakuwa kubwa.

Hilo ndilo wazo langu kaka sina jingine zaidi ya hilo.Labda ulitengeneze vizuri zaidi kuliweka vyema ili lieleweke maana kiswahili ni chetu lakini kuna wakati kinazingua pia.

nimekuelewa mkuu
 
Back
Top Bottom