Je rafiki yako alijua kama aliefunga nae ndoa alikuwa mpenzi wako? Je mpenzi wako alijua kuwa jamaa ni rafiki yako wa karibu? Kama hawakujua basi endelea kuwa nao kiurafiki tu basi na wasamehe, na ni vizuri rafiki yako akijua kuwa ulikuwa nae kimapenzi yule alie muoa, ila muhakikishie umevua mkanda mbele ya mungu, maana akija kusikia kwa wengine au mkewe itakuwa noma, atajiuliza kwanini haukumwambia.
Na kama rafiki yako alijua uhusiano wenu kati ya wewe na yule, basi huyo rafiki ni mnafiki, rafiki mbaya sana, anapenda kuiba vya watu, ni ****, anasubiri wengine watafute yeye ale tu, mjinga mpumbavu. Kwaiyo hata ukioa mke mwingine atakuja kumla vile vile muepuke huyo, ni mshenzi sana, kata mawasiliano nae moja kwa moja.
Na kama binti ulietaka kumuoa alijua uhusiano wenu na yule rafiki yako, basi nae ni mshezi kama huyo bwana. Kama alikupenda hasingelaghaiwa kiuraisi namna hiyo, au ndio tamaa yake ya kuolewa haraka haraka na aliona haupo activ?
sijui kaka unatokea mazingira gani na dini gani. Kama huku kwa waislam, ulikuwa nae binti kimapenzi kisiri bila mtu kujua, na mukaaidiana muoane nawe, ila mambo yako hayapo sawa, labda unasoma nk, akija rafiki yako au binamu yako kuleta posa, anakubaliwa na mwanamke akiona haupo activ nae, au anazani ushapata mwingine ulipo, basi yeye atakubali kuolewa pia. Pole ila wewe mwenyewe unajua mazingira yalivo na mapenzi yenu yalivo kuwa, utapata jibu nazani. Au muulize huyo mwanamke kwanini kakufanyia hivo?