Unalifahamu kundi la UB40?

Unalifahamu kundi la UB40?

Nyimbo za UB40 nizipendazo ni pamoja na Red Red Wine, Here I'm Baby, I Got You Baby, If it Happens Again, Sing Our Own Song na Tell it Like it is.

Huyo Chrissie Hynde aliyewaona UB40 na kisha kuamua kuwafadhili ndiye aliimba nao wimbo wa "I Got You Baby".

Pia Chrissie Hynde akiwa na kundi lake la The Prentenders wametoa vibao vingi sana. Mwezi July 1985, UB40 na The Prentenders walishiriki onyesho moja kubwa sana lililoitwa "Live Aid" ambalo ilifanyika Wembley Stadium nchini Uingereza ili kuchangia wahanga wa njaa nchini Ethiopia. Kati ya nyimbo zilizoimbwa na The Prentenders kwenye tamasha hilo ni pamoja na "Message of Love", "Stop Your Sobbing" na "Talk of the Town".

Washiriki wengine katika tamasha hilo walikuwa ni mzaliwa wa Zanzibar Freddie Mercury na kundi lake la Queen, Mark Knopfler na kundi lake la Dire Straits, The Beach Boys, Bono na kundi lake la U2, David Bowie, The Who, Simple Minds, Madonna, Phil Collins, Paul Young na Santana kwa uchache.
 
Nilienda kwenye concert yao .
I had a great time.
I love UB40.

Sikuwa najua sana historia yao nimejifunza mengi asante .
mimi pia nliwahi kwenda kwa concert yao kwa kweli sintokaa nisahau. Nashkuru zidi kutembelea MTOKAMBALI kwa mengi kuhusiana na MAISHA, MUZIKI, AFYA NA MENGINE MEENGI .
 
Msondo Ngoma wanaimba Ila wapate pombe Na mademu
HA HA HA HAAAAAAAAAAAAAAAA
Nyimbo za UB40 nizipendazo ni pamoja na Red Red Wine, Here I'm Baby, I Got You Baby, If it Happens Again, Sing Our Own Song na Tell it Like it is.

Huyo Chrissie Hynde aliyewaona UB40 na kisha kuamua kuwafadhili ndiye aliimba nao wimbo wa "I Got You Baby".

Pia Chrissie Hynde akiwa na kundi lake la The Prentenders wametoa vibao vingi sana. Mwezi July 1985, UB40 na The Prentenders walishiriki onyesho moja kubwa sana lililoitwa "Live Aid" ambalo ilifanyika Wembley Stadium nchini Uingereza ili kuchangia wahanga wa njaa nchini Ethiopia. Kati ya nyimbo zilizoimbwa na The Prentenders kwenye tamasha hilo ni pamoja na "Message of Love", "Stop Your Sobbing" na "Talk of the Town".

Washiriki wengine katika tamasha hilo walikuwa ni mzaliwa wa Zanzibar Freddie Mercury na kundi lake la Queen, Mark Knopfler na kundi lake la Dire Straits, The Beach Boys, Bono na kundi lake la U2, David Bowie, The Who, Simple Minds, Madonna, Phil Collins, Paul Young na Santana kwa uchache.
Dah! aksante sana ndugu wewe ni muziki na muziki ni wewe. I like that.
 
HA HA HA HAAAAAAAAAAAAAAAA

Dah! aksante sana ndugu wewe ni muziki na muziki ni wewe. I like that.
Nafikiri mwezi wa 10 Mwaka Jana, nilienda kuwaona Msondo Ngoma, aisee wamechakaa vibaya sana. Baba yake Chid Benz Na Romario wamelewa vibaya sana sasa sijui ni stress au ndio stimu, maana wenyewe ndio wakongwe waliobaki Na hawana Hali.
 
Nafikiri mwezi wa 10 Mwaka Jana, nilienda kuwaona Msondo Ngoma, aisee wamechakaa vibaya sana. Baba yake Chid Benz Na Romario wamelewa vibaya sana sasa sijui ni stress au ndio stimu, maana wenyewe ndio wakongwe waliobaki Na hawana Hali.
Kumbe baba yake Chid Benz nae ni mwanamuziki na yuko Msondo?
 
Nafikiri mwezi wa 10 Mwaka Jana, nilienda kuwaona Msondo Ngoma, aisee wamechakaa vibaya sana. Baba yake Chid Benz Na Romario wamelewa vibaya sana sasa sijui ni stress au ndio stimu, maana wenyewe ndio wakongwe waliobaki Na hawana Hali.
Tatizo ni kwamba waliokua wakiiamsha msondo wote washatangulia mbele za haki.
 
Ninapoongelea UB40 hapana shaka kwa wewe mpenzi wa burudani ya Muziki utakua unajua anwaongelea wakina nani. Kwa namna moja ama nyingine utakua umekwisha kusikia kibao kama vile “Red Red Wine, I got the Cup” na ule wa Falling in Love with You. Sasa pata kujua nyimbo zote hizo ni kazi za kundi hili la muziki kutoka huko Kusini mwa Birmingham, England. Kundi hili lilikua na vichwa kama vile Brown, Bria Travers, Trecence Oswald na Norman Hassan

Mwanzo wa kundi hili.
Wana kikundi hicho walikua marafiki tangu wakiwa shuleni na Ugumu wa maisha walio kua nao ndio uliosababisha kuunanisha vipaji vyao na kutengeneza kikundi hicho ili kufanya muziki na kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini waliokua nao.

Jina la Ub40 lilikuja kutokana na wananchi wa Uingereza kutoa waraka wenye kurasa 40 uliohusu mafao yao ya afya na ajira . hivyo basi kundi hili likaamua lijiite Ub40.
Brian Travers alijiunga na kundi hilo akiwa na zana yake ya Saxophone huku wengine wakija na magitaa. Na mara walianza kubandika mabango katika mitaa ya Uingereza wakitangaza bendi yao.
Wimbo wao wa kwanza ulisikika katika Ukumbi wa The Hare na Hounds Pub Februari 1979 katika shereh za kuzaliwa rafiki yao.
Chrissie Hynde ndiye aliye waona vijana hao wakiimba katika ukumbi mmoja ndipo alipoamua kuwafadhili na kuwapa nafasi ya kurekodi wimbo wao wa kwanza “King/Food for Thought” wimbo ambao ulishika nafasi ya 4 katika chati za muziki nchini humo.
Albamu yao ya kwanza iliitwa “Signing Off” wakimaanisha wanayamaliza malalamiko yao ya ukosefu wa ajira na mafao ya afya. Albamu hii ilizinduliwa rasmi Agosti 1980.
Ikumbukwe kua mnamo mwaka 2010 mahakama ya Uingereza ilitangaza kuwa UB40 imefilisika. Kufilisika kwao kumekuja baada ya wanamuziki wane kina Jimmy Brown, Bria Travers, Trecence Oswald na Norman Hassan kushindwa kulipa madeni yao ya kodi.
Kundi hili ndilo kundi linalotajwa kuwahi kuuza nakala nyingi duniani katika nyanja ya Muziki.

Japo kwa ufupi nmeweza kukupatia historia ya Kundi hili amabalo liliwika mno miaka ya nyuma.

Nimeandika Makala nyingi zihusuzo MAISHA, MUZIKI na MICHEZO Ili kuzisoma zote tafadhali tembelea >>HAPA<<<
Hebu ongea na moderator akusaidie kurekebisha heading
 
Ninachofahamu juu ya UB 40 ni kwamba kuna jamaa mmoja alikuwa mahiri saana kwa kuimba kwenye safu ya mbele akiitwa Ali Campbell almaarufu kama the "Voice of UB 40" na punde baada ya jamaa kuwamwaga na kundi likafia hapo.

Nadhani ukisikiliza kwa umakini nyimbo nyingi za UB 40 utagundua kuna sauti unaisikia zaidi kuliko zingine basi huyo ndo Ali Campbell.

Nawakubali saana UB 40.
 
Huyu hapa dio Ali Campbell, kwenye picha hiyo ya wengi ndie anaeonekana wa kwanza alikuwa lead singer watu wakampachika jina la "The voice of UB 40".

Cheers!
 

Attachments

  • 1459449700786.jpg
    1459449700786.jpg
    6.5 KB · Views: 41
  • 1459449711486.jpg
    1459449711486.jpg
    7.9 KB · Views: 34
Mid nakipenda kibao cha wise man say a.k.a I can't help falling in love with you yaani sauti, midundo na vyombo vyake sichoki kuusikiliza. Ingawa wimbo wenyewe kiuhalisia ulianza imbwa na Elvis presley
 
Ninachofahamu juu ya UB 40 ni kwamba kuna jamaa mmoja alikuwa mahiri saana kwa kuimba kwenye safu ya mbele akiitwa Duncan Campbell almaarufu kama the "Voice of UB 40" na punde baada ya jamaa kuwamwaga na kundi likafia hapo.

Nadhani ukisikiliza kwa umakini nyimbo nyingi za UB 40 utagundua kuna sauti unaisikia zaidi kuliko zingine basi huyo ndo Duncan Campbell.

Nawakubali saana UB 40.
yeah
 
Back
Top Bottom