Unalifahamu kundi la UB40?

Unalifahamu kundi la UB40?

Ninachofahamu juu ya UB 40 ni kwamba kuna jamaa mmoja alikuwa mahiri saana kwa kuimba kwenye safu ya mbele akiitwa Duncan Campbell almaarufu kama the "Voice of UB 40" na punde baada ya jamaa kuwamwaga na kundi likafia hapo.

Nadhani ukisikiliza kwa umakini nyimbo nyingi za UB 40 utagundua kuna sauti unaisikia zaidi kuliko zingine basi huyo ndo Duncan Campbell.

Nawakubali saana UB 40.
Samahani mkuu. Nikusahihishe kidogo. Kwanza kundi la UB40 bado halijafa lipo linapiga mzigo japo halina umaarufu kama ilivyokuwa kwenye miaka ya themanini na tisini.

Pili huyo Duncan Campbell uliyemtaja siyo yule aliyevuma na kundi kwa miaka mingi kwani yeye na mdogo wake Robin Campbell walijiunga na kundi hilo mwaka 2008 baada ya mdogo wao aitwae Alistair maarufu kwa jina la Ali Campbell kuwa ameondoka kwenye band. Ndugu hao wawili Robin (ambaye ndiye mkubwa kabisa) na Robin bado wapo kundini hadi hii leo.

Hivyo usahihi ni kwamba Ali Campbell ndiye alikuwa mwimbaji kiongozi wa kundi hilo na ndiye sauti yake imesikika kwenye nyimbo zao nyingi maarufu kama Red Red Wine, If it Happens Again, Sing Our Own Song, Rat in the Kitchen n.k. Yeye alikuwa ni mmoja wa waanzilishi wa kundi na alidumu kundini kwa zaidi ya miongo miwili.

Ali Campbell aliamua kujiengua kwenye kundi kutokana na kutokuelewana na uongozi na hii ilitokea muda mfupi baada ya kundi zima la UB40 kutoka katika ziara yake nchini Uganda mwanzoni mwa mwaka 2008.

Baada ya Ali kuondoka na kuamua kuwa mwanamuziki wa kujitegemea umaarufu wa kundi umeporomoka kwa kiasi kikubwa kama thamani ya shilingi ya Tanzania kwa Dola ya kimarekani.
 
Back
Top Bottom