Ok! sasa wooote mnasema ooh changu hivi mara vile sasa nataka niwaonyeshe njia kumi bora za kutambua kipaji chako, na hii haijalishi wewe ni nani na uko wapi ilimradi tu maisha yanaenda, hapana ukijua kipaji chako maisha yatakuwa rahisi sana, kiujumla mfano mtu ana kipaji cha kupiga ngenga saana,asa badala ya kukaa kijiweni, anakurupuka na slogan ya Mungu,yaani huyu anakuwa mchungaji wanasemaga eti wameitwa na Mungu.na mwingine akijaribu wanamshushua na maneno Umeitwa? niliwahi kuyasema haya maarifa kipindi fulani mwaka jana. ila kwa faida ya watu woote wa JF nitarudia hapapa tena kama ifuatavyo;
(1)Kazania sana kufanya jambo ambalo unalipenda sana kutoka moyoni,na jambo hili lisiwe la
kuiga kwa mfano umekua hujui kuimba ghafla unamuona Diamond anaimba tayari na wewe unataka,
(2},Weka mkazo kwa kila jambo ambalo unalitimiza kirahisi, tu bila kutumia nguvu nyingi.utajuaje?
rahisi tu marafiki zako na watu wako wa karibu kama familia, wanafunzi wenzako wata kusifia
katika utekelezaji wa jambo lililo kubwa kwao watasema muite fulani aje.kama mashauri, ku
fix home appliance,kutunza mifugo nk.
(3} Ni kitu gani ulipendelea sana kufanya ukiwa mtoto mdogo chini ya miaka mitano yaani hicho
kitu ulikifanya mara kwa mara,mfano toy za gari za udongo,au waya waya, kucheza
mpira nk,pia kama ilitokea wazazi walipokupeleka shoping ulitamani nini pale
Dukani kuliko kile baba yako alikuchagulia,
(4) kile unachokiogopa saaana hata kujaribu tu ,kifanye kwa moyo wako wote anza kujaribu
kidogo kidogo hapo ndo kipaji kime lala.