Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
Najua watu wengi walikua wanajiuliza sana Pesa ya Tanzania inatengenezwa wapi ? Ni maswali ambayo mimi na wewe tulia tunajiuliza sana? Je Tanzania Ina kiwanda cha kutengeneza pesa zake ??
Maswali yote Leo utaweza kupata majibu yake kwa ufupi TU kupitia makala hii 😋, kwanza inapaswa kujua Pesa huwa azitengenezwi nchi moja TU hutengenezwa kupitia nchi mbalimbali hapa Duniani.
Pesa zinatengenezwa kwenye nchi zilizoendelea kama vile Marekani, Ujerumani, Ufaransa, Uswizi, Saudi Arabia, Sweden na Uingereza.
Ila kwa upande wa Afrika nchi zinazotengeneza pesa ni zifuatazo:
- Misri
- Morocco
- Nigeria
- Ghana
- South Africa
- Sudan
- Algeria
Kwa upande wa Ethiopia na Zimbabwe kuna kipindi walikuwa wanatengeneza pesa zao lakini baadae walizuiliwa kutokana na sheria maalum za kimataifa zinazo husika na taratibu za kumiliki kiwanda cha kutengeneza pesa.
Nchini Kenya kuna kiwanda cha kutengeneza pesa kinachoitwa De La Rue kutoka nchini Uingereza na kwa hivyo kiwanda hicho kipo Kenya kama tawi kwa upande wa Afrika mashariki.
Je pesa ya Tanzania inatengenezwa wapi sasa ??
Pesa ya Tanzania kamwe haitengenezwi nchini Tanzania.
Mwanzoni baada ya uhuru pesa ya Tanzania ilikua inatengenezwa Nchini Uingereza kuanzia sarafu na Noti ambapo serikali ya Tanzania ilikua inaipa Tenda nchi ya Uingereza.
Kwa sasa pesa za Tanzania haitengenezwi Tena Uingereza isipokuwa Ujerumani ndio inatengeneza pesa Za TANZANIA aina ya Noti ambazo ni;
⚡ ELFU KUMI
⚡ ELFU TANO
Wakati nchi ya Sweden inatengeneza Pesa za nchi ya Tanzania ambapo kuanzia NOTI na SARAFU;
⚡ ELFU MBILI
⚡ELFU MOJA
⚡SARAFU
Ulikua unajua hii au lah tuachie maoni yako??