Wala sio ufisadi, ni kuridhika mapema kwa Wahindi walikuwa wakimilki hicho kiwanda. Walikuwa na monopoly ya aina yake miaka ya 80, nakumbuka malori ya akina Paul Ngwani na Chacha nini cjui walikuwa yanapanga foleni pale kiwandani Arusha kwa hata wiki nzima kusubiria mzigo.
Shida ilianza Mengi alipoanzisha Bonite bottlers, akajaza Coke sokoni watu wakawa hawanunui tena Double cola, Wahindi baadae wakawauzia Pepsi kiwanda kikageuzwa godown. Huo ndio ukawa mwisho wa Double cola, ilikuwa inatesa sana wakati wa kipaimara na Xmas wakasahau kujiendeleza kibiashara