Unafiki wa Wabunge wa Tanzania: Kwanini hawalipi kodi?

Gagurito

JF-Expert Member
Feb 11, 2011
5,600
804
Nchi hii haiwezi kuendelea kama wananchi wa nchi hii hawatafanyakazi na kulipa kodi.

Tupo takribani 44,929,002 ila wanaokadiliwa kulipa kodi (watu pamoja na mashirika) ni 2.7 m.

Cha ajabu wabunge wetu licha ya kupata mishahara minono (takribani 12m kwa mwezi) hawalipi kodi. Mwalimu wa sekondari mwenye degree ambaye mshahara wake ni laki 532,000 anakatwa shilingi 56,400 (kodi kwa mwezi) anachangia shilingi laki 672,000 kama kodi kwa maendeleo ya taifa hili kwa mwaka licha ya mishahara yao kuwa midogo.

Swali la kujiuliza hapa ni juu ya uhalali wa wabunge wetu kuishauri na kuhoji mambo mbali mbali serikali juu ya mapato na matumizi (ya kodi) wakati wao hawalipi kodi.

Je, huu sio unafiki wa Wabunge wetu kwa wananchi na taifa?
Kweli watanzania wengi ni wavivu sana wa kusoma na kufanya utafiti lakini ni wepesi wa kulalamika na kulaumu. Nani alikwambia kuwa wabunge hawalipi kodi? Nani alikwambia kuwa mawaziri au rais halipi kodi? Hawa wote wanalipa kodi kutoka kwenye mishahara yao.

Kwa faida tu kila mtumishi wa umma bila kujali wadhifa hulipa PAYEE kama ifuatavyo:

Kiwango cha Kodi
Mapato ya jumla yasiyozidi Shilingi 2,040,000/=
Asilimia sifuri (0%)
Mapato ya jumla yanayozidi Shilingi 2,040,000 lakini hayazidi shilingi 4,320,000/=
13% ya kiasi kinachozidi Shilingi 2,040,000/=

Mapato ya jumla yanayozidi Shilingi 4,320,000/= lakini hayazidi shilingi 6,480,000/=
Shilingi 296,400/= + 20% ya kiasi kinachozidi Shilingi 4,320,000/=

Mapato ya jumla yanayozidi Shilingi 6,480,000/= lakini hayazidi shilingi 8,640,000/=
Shilingi 728,400/= + 25% ya kiasi kinachozidi Shilingi 6,480,000/=

Mapato ya jumla yanayozidi Shilingi 8,640,000/=
Shilingi 1,268,400/= + 30% ya kiasi kinachozidi Shilingi 8,640,000/=
 
Namnukuu Mwl J K Nyerere
".......serikali corrupt haikusanyi kodi......"

Nadhani ifike wakati kila Mtanzania alipe kodi kutokana na kipato anachopata. Ukiangalia wanachofanya hawa waheshimiwa huko Bungeni unaweza hata ukasema kuna wakati kama wanapoteza muda, au wanatudhulumu sisi wananchi tuliowachagua nk. Iweje waanze kulumbana mambo yasiyo na msingi;

Mfano wa kero zilizonichefua roho:
Mh Leticia Nyerere "Kujengwe Chuo Cha kujifunza kutongoza"
Mh. Nkamia, "Naongea na mwenye mbwa siongei na mbwa"
Mh. Lusinde, "Ondoeni picha za wanyama ili thamani ya pesa ipande"

Hawa watu hawa wakitoka hapo wanasaini sitting allowance ambayo ni sawa na mshahara wangu wa mwezi yeye anachukua kwa siku moja tu na pumba hizo halafu bila kukatwa kodi. Hapana ili waone thamani halisi ya muda wao pale Bungeni na ili watumie muda wanaopewa wakautumia kwa tija waanze kulipa kodi.

Ikiwa hawa waheshimiwa wangekuwa hawalipwi mshahara kwa mwezi hasa kusipokuwapo vikao vya Bunge ningefikiria vinginevyo. Kuna Organs TATU za Serkali ambazo ni BUNGE, MAHAKAMA na EXECUTIVES kama organs zingine wanalipa kodi kwanini hawa wabunge wasilipe.

Mtu asiyelipa kodi tafsiri yake ni kwamba anaiibia serikali. Tanzania itajengwa na wenye moyo safi ambao wanaitumikia, kuiibia serikali ni dhambi sana. Ili kuonyesha kuwajibika kwa dhati sasa anzeni kulipa kodi hakuna sababu ya msingi ya nyie kutolipa kodi, wear our shoes to feel the pinch.
 
Bubu Msemaovyo

mkuu nasiukuru kwa ufafanuzi wako, nakuunga mkono. Nchi SIASA NDIO IMEKUWA KIPAUMBELE KIKUBWA NA MUHIMU KULIKO HATA WANANCHI NA MAENDELEO YA TAIFA. Wabunge wengi hawajitambui, wanafanya madudu kama watoto wadogo bungeni, wanachezea kodi zetu pia wanatuibia sisi wananchi.

HIVI WATAWEZAJE KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA KODI ZETU WANANCHI WAKATI WAO HAWALIPI KODI? HIVI HUO UJASIRI WANAUTOA WAPI? Nadhani si vyema ktk hili, huku ni kuibiwa mchana mchana!
 
Last edited by a moderator:
ingawa nakuunga mkono kwenye suala la kila mtu kulipa lakini ukiangalia upande wa pili wa shillingi wa hayo matumizi yenyewe ya kodi nako pia ni tatizo kubwa kwahiyo inabidi kucheza on both sides of equation. je ukiongeza mapato huduma zitaboresheka au utawafanya wakubwa waongeze idadi ya mashangingi na marupurupu yao ?? bila kuwepo disciplinary ktk matumizi ya umma hata uongeze mapato kiasi haitoleta tofauti ni sawa na kutia maji kwenye gunia.
 
Ukweli ni kuwa kama serikali itakusanya kodi kwa ufanisi hatuwezi kukopa ovyo wala kutegemea misaada kwa ajili ya maendeleo.Cha ajabu hao wasiolipa kodi wanakimbilia nje ya nchi kuwekeza huko.

Hainiingii akilini hata kidogo mimi nilipe kodi (PAYEE) alafu mwenye nyumba wangu yeye anapokea hela yangu ya Pango bila kulipia mapato yoyote serikalini hata kodi ya nyumba kwa mwaka halipi!.

Tatizo la serikali yetu watumishi wanapenda kukaa ofisini na kusubiri kila kitu kijiendeshe bila ya kufuatilia sheria na taratibu, pia kuwa wabunifu wa vyanzo vipya vya mapato.
 
ingawa nakuunga mkono kwenye suala la kila mtu kulipa lakini ukiangalia upande wa pili wa shillingi wa hayo matumizi yenyewe ya kodi nako pia ni tatizo kubwa kwahiyo inabidi kucheza on both sides of equation. je ukiongeza mapato huduma zitaboresheka au utawafanya wakubwa waongeze idadi ya mashangingi na marupurupu yao ?? bila kuwepo disciplinary ktk matumizi ya umma hata uongeze mapato kiasi haitoleta tofauti ni sawa na kutia maji kwenye gunia.

Ni kweli upande wa matumizi pia bado ni tatizo, na wala sio matumizi tu, hata mfumo wa ukusanyaji kodi bado ni tatizo tena maradufu. Kiasi kinachokusanywa ni kiduchu sana ila matumizi yake yamekua ya hovyo sana. Ila kwa leo ningependa tujadili juu ya ushiriki wa wabunge wetu juu ya ulipaji wa kodi. Kwa nini hawalipi kodi? Je wao ni first class tanzanians? Why wapo tofauti sana na watumishi wa uma wakati wote wanatoa huduma kwa jamii? Je ni halali hii?
 
Ukweli ni kuwa kama serikali itakusanya kodi kwa ufanisi hatuwezi kukopa ovyo wala kutegemea misaada kwa ajili ya maendeleo.Cha ajabu hao wasiolipa kodi wanakimbilia nje ya nchi kuwekeza huko.

Hainiingii akilini hata kidogo mimi nilipe kodi (PAYEE) alafu mwenye nyumba wangu yeye anapokea hela yangu ya Pango bila kulipia mapato yoyote serikalini hata kodi ya nyumba kwa mwaka halipi!.

Tatizo la serikali yetu watumishi wanapenda kukaa ofisini na kusubiri kila kitu kijiendeshe bila ya kufuatilia sheria na taratibu, pia kuwa wabunifu wa vyanzo vipya vya mapato.

Tena wakati ufike sasa kila nyumba ibainike kulingana na matumizi yake. Kama ni nyumba ya makazi basi iwe kwa ajili ya familia na wao waendelee kulipa ile sh. 12,000 kwa mwaka kama ilivyokawaida. Zile nyumba zinazopangisha watu zithaminishwe kulingana na ukubwa wa nyumba na zilipe kodi. BABA MWENYE NYUMBA YANGU HANA TOFAUTI NA MBUNGE KWANI WOTE HAWALIPI KODI. Shwaaaain.
 
Nchi hii haiwezi kuendelea kama wananchi wa nchi hii hawatafanyakazi na kulipa kodi. Tupo takribani 44,929,002 ila wanaokadiliwa kulipa kodi (watu pamoja na mashirika) ni 2.7 m. Cha ajabu wabunge wetu licha ya kupata mishahara minono (takribani 12m kwa mwezi) hawalipi kodi. Mwalimu wa sekondari mwenye degree ambae mshahara wake ni laki 532,000 anayekatwa shilingi 56,400 (kodi kwa mwezi) anachangia shilingi laki 672,000 kama kodi kwa maendeleo ya taifa hili kwa mwaka licha ya mishahara yao kuwa midogo. Swali la kujiuliza hapa ni juu ya uhalali wa wabunge wetu kuishauri na kuhoji mambo mbali mbali serikali juu ya mapato na matumizi (ya kodi) wakati wao hawalipi kodi. Je huu sio unafiki wa Wabunge wetu kwa wananchi na taifa? Nawasilisha.


umenipa kitu kipya sikuwa najua kama wabunge hawalipi kodi ili hali Rais na Jaji Mkuu wanalipa. Hili tulibebee Bango ndo maana wengi wao ni bomu.
 

tena si kidogo mkuu. Yale yanayogeuza bunge kuwa kama kampeni za uchaguzi ama mipasho kwa kodi zetu ndio yanaboa zaidi. Wananchi cha ajabu tunawashokea na cheo cha UHESHIMIWA TUMEMPA!
 
umenipa kitu kipya sikuwa najua kama wabunge hawalipi kodi ili hali Rais na Jaji Mkuu wanalipa. Hili tulibebee Bango ndo maana wengi wao ni bomu.

Ndio hivyo mkuu, wanakula gud time kwa kodi za wananchi, wanavalishwa mavazi yao kwa kodi yetu, usafiri ule wa mashangingi kwa kodi yetu, BAADHI YAO HAWACHANGII CHOCHOTE BUNGENI NA WENGINE WANACHANGIA UPUUZI USIO NA TIJA KWA TAIFA LICHA YA KWAMBA TUNAWAHUDUMIA BURE KWANI HAWALIPI KODI.
 
Halafu mimi ndio maana namfagilia Fisadi Bw.Lowasa, kaiba hela nyingi na sasa hivi anairudisha kwenye jamii kwa kutoa michango mingi sana kwenye mambo ya kijamii, kuanzia jimboni kwake mpaka maeneo mengine ya nchi, lkni hawa wengine Wabunge wote wanatuibia na kupata fedha ya Dhuluma na hawafanyi chochote kwenye jamii!

Halafu wakitoka huko Bungeni utawaona kwenye majukwaa na kuanza kuita wenzao Majina kama mafisadi wakati wao ndio mafisadi namba moja, wanalipwa fedha ya kuwalipa Madereva lkn hawaajiri madereva na pesa wanachukua, wanalipwa fedha ya jimbo na ofisi lkn muda wote wako Dar na ofisini kwao (Jimboni) hawakai, lakini kutwa nzima utasikia Bw.Lowasa Fisadi!
 
Halafu mimi ndio maana namfagilia Fisadi Bw.Lowasa, kaiba hela nyingi na sasa hivi anairudisha kwenye jamii kwa kutoa michango mingi sana kwenye mambo ya kijamii, kuanzia jimboni kwake mpaka maeneo mengine ya nchi, lkni hawa wengine Wabunge wote wanatuibia na kupata fedha ya Dhuluma na hawafanyi chochote kwenye jamii!

Halafu wakitoka huko Bungeni utawaona kwenye majukwaa na kuanza kuita wenzao Majina kama mafisadi wakati wao ndio mafisadi namba moja, wanalipwa fedha ya kuwalipa Madereva lkn hawaajiri madereva na pesa wanachukua, wanalipwa fedha ya jimbo na ofisi lkn muda wote wako Dar na ofisini kwao (Jimboni) hawakai, lakini kutwa nzima utasikia Bw.Lowasa Fisadi!

Mwizi ni mwizi tu no matter anatumia vp pesa zake za wizi. Ila atleast Lowassa anarejesha kwa wananchi japo kwa kiwango kidogo!
 
Halafu mimi ndio maana namfagilia Fisadi Bw.Lowasa, kaiba hela nyingi na sasa hivi anairudisha kwenye jamii kwa kutoa michango mingi sana kwenye mambo ya kijamii, kuanzia jimboni kwake mpaka maeneo mengine ya nchi, lkni hawa wengine Wabunge wote wanatuibia na kupata fedha ya Dhuluma na hawafanyi chochote kwenye jamii!

Halafu wakitoka huko Bungeni utawaona kwenye majukwaa na kuanza kuita wenzao Majina kama mafisadi wakati wao ndio mafisadi namba moja, wanalipwa fedha ya kuwalipa Madereva lkn hawaajiri madereva na pesa wanachukua, wanalipwa fedha ya jimbo na ofisi lkn muda wote wako Dar na ofisini kwao (Jimboni) hawakai, lakini kutwa nzima utasikia Bw.Lowasa Fisadi!

Mwizi ni mwizi tu no matter anatumia vp pesa zake za wizi. Ila atleast Lowassa anarejesha kwa wananchi japo kwa kiwango kidogo!
Kama hajasema JAMANI EHHH NILIIBA SASA NARUDISHA mwogope kama ukoma.

Atakuwa anatumia alichoiba ili kupata nafasi ya kuiba vingi zaid!.
 
Kama hajasema JAMANI EHHH NILIIBA SASA NARUDISHA mwogope kama ukoma.

Atakuwa anatumia alichoiba ili kupata nafasi ya kuiba vingi zaid!.

Hiyo sio ishu, hata kukaa kimya pia ni jibu vile vile, isitoshe kama swala ni kuiba hakuna Mtanzania anayefaa kuwa Raisi labda awe amekulia diaspora huko lkn sio ndani ya Bongo, kwani wote kwa namna moja ama nyingine tunaiibia nchi yetu wenyewe, tofauti tu ni kwamba ni nani anapata nafasi ya kuiba zaidi ya mwingine, kuanzia mesenja maofisini mpaka watu wa Masjala wote wezi tu, ukija Madereva wa mgari ya Serikali wote wezi tu, kutwa wanauza Mafuta ya Magari mitaani, na ndio maana kiongozi mkubwa wa Kiroho nchini kwetu Kardinali Pengo alisema, ktk jamii yetu anayelalamikia UFISADI ni kwamba hajapata nafasi, ndio maana analia, siku akipata na yeye ataiba tu!

Kwa kifupi hakuna Mtanzania anayeishi na kufanya Tanzania mwenye haki ya kumyooshea Fisadi Bw.Lowasa kidole!
 
Hiyo sio ishu, hata kukaa kimya pia ni jibu vile vile, isitoshe kama swala ni kuiba hakuna Mtanzania anayefaa kuwa Raisi labda awe amekulia diaspora huko lkn sio ndani ya Bongo, kwani wote kwa namna moja ama nyingine tunaiibia nchi yetu wenyewe, tofauti tu ni kwamba ni nani anapata nafasi ya kuiba zaidi ya mwingine, kuanzia mesenja maofisini mpaka watu wa Masjala wote wezi tu, ukija Madereva wa mgari ya Serikali wote wezi tu, kutwa wanauza Mafuta ya Magari mitaani, na ndio maana kiongozi mkubwa wa Kiroho nchini kwetu Kardinali Pengo alisema, ktk jamii yetu anayelalamikia UFISADI ni kwamba hajapata nafasi, ndio maana analia, siku akipata na yeye ataiba tu!

Kwa kifupi hakuna Mtanzania anayeishi na kufanya Tanzania mwenye haki ya kumyooshea Fisadi Bw.Lowasa kidole!

Sio wote, wengine tunajitambua!
 
Cha ajabu wabunge wetu licha ya kupata mishahara minono (takribani 12m kwa mwezi) hawalipi kodi.

mshahara wa mbunge unakatwa kodi kama watumishi wengine isipokuwa tatizo lipo kwenye utaratibu wa kuwapa misamaha ya kodi pale wanapoagiza vifaa toka nje ya nchi. hapo ndio penye udhaifu.
 
Sio wote, wengine tunajitambua!

Basi labda wewe umekulia nje ya Tanzania au ni diaspora au unafanya UN ambako wanakubana huwezi hata kutoa upepo wa tairi, au uko kwenye Kampuni za Wazungu, lkn kama ni Mbongo wa kawaida na Unafanya Serikalini au sijui kwenye Mashirika ya Umma, HAKUNA MSAFI, au sijui unafanya Biashara Bongo lazima utakuwa tu kuna mahali umeidanganya Serikali aidha haulipi Kodi ipasavyo au unawabana Wafanyakazi na huwalipii NSSF na hayo yote unayafanya kwa kuhonga tu hivyo tunaruddi pale pale, hakuna mwenye haki ya kumsema fisadi Bw.Lowasa!

Hivyo Kauli ya Kardinali Pengo bado inasimama!


 
mshahara wa mbunge unakatwa kodi kama watumishi wengine isipokuwa tatizo lipo kwenye utaratibu wa kuwapa misamaha ya kodi pale wanapoagiza vifaa toka nje ya nchi. hapo ndio penye udhaifu.

Unahuhakika wee jamaa?
 
Back
Top Bottom