Unadhani mtuhumiwa huyu atapona?

Unadhani mtuhumiwa huyu atapona?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
361,078
Reaction score
831,704
POLISI MBEZI KWA YUSUFU MNASTAHILI PONGEZI!

Mtu huyu (pichani) aliyejitambulisha kwa jina la Juma kutokea maeneo ya Bulula - Kimara Suka alikuwa amekamatwa akituhumiwa kufanya vitendo vya wizi leo mchana eneo la Rift Valley, Kimara Suka. Watu wenye hasira walikuwa wakimshambulia kwa mawe, mapanga, nk! Ilikuwa ni neema ya Mungu nilikuwa natoka kumsindikiza Mchungaji aliyenitembelea ndipo nikasikia mayowe na kelele. Nilipofika eneo la tukio nilikuta hali ya mtuhumiwa siyo nzuri! Nilichofanya ni kwenda kusimama kando yake na kutoa ishara ya kuwataka watu waache kumpiga.

Ninamshukuru Mungu watu wale walitii sauti yangu ingawa wapo waliokuwa wakisubiri niondoke ili waendelee .......
Niliamua kupiga simu katika kituo cha Polisi Mbezi Kwa Yusufu. Wakati Polisi wakijipanga kuja na nilipogundua kuwa mazingira yale yalikuwa hatarishi kwa mtuhumiwa, nilifanya utaratibu na nikafanikiwa kumsogeza mbele kidogo ili kuokoa maisha yake. Ninaushukuru sana Uongozi wa Kituo cha Polisi cha Mbezi kwa Yusufu kwa kuitikia wito wangu wa ghafla.

Kipekee ninamshukuru sana Afande Zena aliyeongoza Kikosi cha Polisi waliokuja kumchukua mtuhumiwa kwa kutumia gari la Polisi. Ninawashukuru pia watu waliokuwa wanampiga mtuhumiwa kwa kutii sauti yangu kama mtumishi wa Mungu ya kuwataka kuacha kumpiga na hivyo kuepusha umwagaji wa damu ya mtu katika eneo lao. Ninamshukuru sana Mungu kwa kuwa sasa mtuhumiwa yupo salama katika mikono ya Polisi ambako taratibu za kisheria zitaendelea. Mtuhumiwa aliumia sana maeneo ya kichwani ila sikutaka kamera yangu ionyeshe majeraha. Tumuombee mtu huyu ili Mungu ampe neema ya kuokoka na kumwamini Yesu.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki 12 Oktoba 2007.​

PHOT.jpg
 
Wanaookolewa na wasamaria wema ni wengi Ila hufia vituoni ama hospital kwa kukosa huduma stahiki ama kwa wakati
Mifano ni mingi na kuna hata ambao walifika kituo cha police wakiwa na afya njema lakini wakatoka kwenye machela
 
Katika amri 10 za Mwenyezi Mungu, ipo moja inaamrisha " usiibe" , maana yake nini? inapotokea ukaikiuka na kwenda kinyume, basi tatizo lolote litakalo kupata, utakuwa ni mshahara wako kwa kile ulicho kifanya.
 
Watu wanapiga na kuua mwizi wa Kuku, lakini wanaoiba mabillioni ya Kodi zetu wanashangiliwa na kuimbwa mitaani na ndugu wanaojiita chawa
Hili ni jambo la kushangaza sana. Wananchi walitakiwa kuanza na haya mafisadi ya ccm yaliyo jimilikisha nchi na raslimali zake.

Yaani ilitakiwa ukiyakuta mahali popote yamezubaa, unayavamia na kuyashambulia! Na siyo hawa vibaka ambao mpaka kufikia hapo, usikute chanzo ni huu utawala dhalimu wa ccm.
 
POLISI MBEZI KWA YUSUFU MNASTAHILI PONGEZI!

Mtu huyu (pichani) aliyejitambulisha kwa jina la Juma kutokea maeneo ya Bulula - Kimara Suka alikuwa amekamatwa akituhumiwa kufanya vitendo vya wizi leo mchana eneo la Rift Valley, Kimara Suka. Watu wenye hasira walikuwa wakimshambulia kwa mawe, mapanga, nk! Ilikuwa ni neema ya Mungu nilikuwa natoka kumsindikiza Mchungaji aliyenitembelea ndipo nikasikia mayowe na kelele. Nilipofika eneo la tukio nilikuta hali ya mtuhumiwa siyo nzuri! Nilichofanya ni kwenda kusimama kando yake na kutoa ishara ya kuwataka watu waache kumpiga.

Ninamshukuru Mungu watu wale walitii sauti yangu ingawa wapo waliokuwa wakisubiri niondoke ili waendelee .......
Niliamua kupiga simu katika kituo cha Polisi Mbezi Kwa Yusufu. Wakati Polisi wakijipanga kuja na nilipogundua kuwa mazingira yale yalikuwa hatarishi kwa mtuhumiwa, nilifanya utaratibu na nikafanikiwa kumsogeza mbele kidogo ili kuokoa maisha yake. Ninaushukuru sana Uongozi wa Kituo cha Polisi cha Mbezi kwa Yusufu kwa kuitikia wito wangu wa ghafla.

Kipekee ninamshukuru sana Afande Zena aliyeongoza Kikosi cha Polisi waliokuja kumchukua mtuhumiwa kwa kutumia gari la Polisi. Ninawashukuru pia watu waliokuwa wanampiga mtuhumiwa kwa kutii sauti yangu kama mtumishi wa Mungu ya kuwataka kuacha kumpiga na hivyo kuepusha umwagaji wa damu ya mtu katika eneo lao. Ninamshukuru sana Mungu kwa kuwa sasa mtuhumiwa yupo salama katika mikono ya Polisi ambako taratibu za kisheria zitaendelea. Mtuhumiwa aliumia sana maeneo ya kichwani ila sikutaka kamera yangu ionyeshe majeraha. Tumuombee mtu huyu ili Mungu ampe neema ya kuokoka na kumwamini Yesu.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki 12 Oktoba 2007.​
Mshana Jr Hii tarehe imekaa sawa kweli 12 Oktoba 2007.
 
Back
Top Bottom