kagombe
JF-Expert Member
- Mar 1, 2015
- 3,511
- 1,643
Ukweli ilaUsipende kwenda kwa ndugu au kukaa kwa ndugu. MAISHA NI MAGUMU.
Unajua una pln b
Ukweli ilaUsipende kwenda kwa ndugu au kukaa kwa ndugu. MAISHA NI MAGUMU.
Njooni mumuone ndugu mwingine huyutatizo wengi wetu tumejijengea imani kwamba kukaa kwa ndug lazima utaonewa au kunyanyaswa...
Yaaan unataka ukae kwa ndug usiguswe kwa lolote kama malaika..?
Ukiambiwa osha vyombo piga deki chota maji kalishe mifugo kapike kutumwa sehém, haya yote unaona manyanyaso wakat kwenu kwa baba na mamako shida tupu au unafanyishwa kazi ngumu na wadogo zako au Kaka/dada zako wapo sebuleni wanaangalia TV na hulalamiki... Ila kwa ndug unasema unaonewa. Sikilizeni vijana huwez kukaa kwa mtu burebure umjazie choo ule ulale kama malkia, no way out utavitolea jasho tu... Alafu mambo ya kukaa kwa ndug yalikua ya kizamani sikuhiz pambana na hali yako
Mzee alikuwa hana uwezo nn, au ujana ulikuwa mwingi akakwepa majukumuNina uzoefu mbaya na mzuri, mzuri ndio umenona sana ingawa kauchafu kadogo kakiingia kwenye mchuzi, mchuzi unaharibika.
Nimelelewa, nimesomeshwa hadi walipoutua mzigo kwa Serikali kwenye elimu ya Juu(Chuo).
Nimekuwa mwanafamilia wa moja kwa moja nilipolelewa ingawa wazazi wangu wapo pia ila mzee ndio miyeyusho sasa(sina mapenzi naye hata kidogo, huu ni ukweli mchungu maana ndio kasababisha nikalelewe kwingine kuanzia udogoni hadi nikawa mkubwa)..
NB: Unaweza ukamlea mtoto ukidhani unamtesa na kumkomoa kumbe unamjenga/unamfunza uvumilivu, umahiri wa kupambana na shida na raha.
Walezi tusibague watoto( wako na wasio wako) katika malezi, tulee watoto kwa usawa.
Ujuaji tu ila.Mzee alikuwa hana uwezo nn, au ujana ulikuwa mwingi akakwepa majukumu
Aliendekeza Umwinyi na pride ya kuoa wake 4, ila kwenye kuhudumia na maono ya kutafuta alikuwa na zero. Halafu ugomvi ndio ilikuwa jadi yakeMzee alikuwa hana uwezo nn, au ujana ulikuwa mwingi akakwepa majukumu
Hisia zimezirai polee ndugu wengine mtihani kwelidah...umenikumbusha, kaka yangu alinisingizia kuwa ninamkimbizia mkewe ili anifukuze tu nyumbani. Niliumia sana. Baada ya wiki mbili nikapata kazi nikahama kwake. Jeraha aliloniwekea ilinichukua muda sana kuliondoa. Na wakati huo ninatafuta kazi, natembea kama mbuzi tangatanga wa mjini, hata hormones zote zimezirai kabisa.
Ulikuwa hutaki wageni, nyie ndio wale watoto mgeni akinywa soda basi mnamkodolea macho Hadi iishe ukisubilia kubakiziwaMimi ilikuwa akija mgeni lazima ni pige tukio sema mala nyingi nilikuwa nasanukiwa naishia kula mikanda na dingi.
Malezi ya ajabu sana mno sitaki hata kuyakumbuka asante BABU kwa ile caring yako unahakikisha nimekula nimeshiba ndio nirudi nyumbani nikalale tuu na hapo na maji ya kunywa unanipa mimi inakuwa ni kitanda tuu na mahali pa kuoga na kubadili the rest are history.Kuna zile family hasa zinapatikana Dar es salaam. Yaani kila mtu anajinunulia chakula kivyake. Mfano asubuhi atakaejisikia kupika chai atajinunulia sukari yake robo na vitafunwa vyake mwenyewe. Mchana utaona huyu kaja na chips, yule kaja na mihogo , mwingine kaja na firigisi. Mpaka unafikiria hii ni familia au ni watu wanaishi ghetto tu!
Ndio ulivyoaminishwa? Mjini ni nadra sana watu kwenda kukaa kwa mwingine kama huna sababu...Wakishua sio
Na mbaya zaidi uwe Jobless...Siku zote ukikaa kwa ndugu wanachowaza wenyeji wako ni umekuja kula na kujaza nafasi sasa kila jambo utakalo fanya liwe hata zuri tu utaonekana huna la maana, mbaya zaidi huwe umeenda kukaa muda mrefu
Hapo utafurahi,Na mbaya zaidi uwe Jobless...