Umuhimu wa kutembelea makaburi upo?

Umuhimu wa kutembelea makaburi upo?

Ahsante kwa
aaaah imani tu hapo...ukiamini kua ukiacha kwenda mambo yako hayatoenda bhas jua itakua ivyo..ila ukiwa kama mimi don care mambo yako yanaenda vizuri tu..angalia imani yako tu inakusukuma ufanye nini mkuuu.

Madhara au Faida hamna mtu ataekuja kuthibitisha hapa 100% kua kuna madhara au faida,ndio mana hata usiku wakat wa kulala au wakat wa kula kuna wanaoamini bila kuomba kumshukuru mungu Si vizuri na kuna wasio amini lkn wote mambo yanaenda na maisha yanasonga.

Angalia imani yako mkuuu.
Ahsante kwa wazo mkuu.......umeniongezea kitu
 
Mkuu maandiko yanatuambia mtu akifariki, uyo ndio kashaondoka hivyo na kafunga hesabu, hakuna ata kivuli atakacho kiacha nyuma wala hakuna mambo ya spiritual hapo au mizimu sijui.
Lakin watu wengi wamethibitisha kuendelea kwa pirika pirika za watu walokufa hapa duniani.....nafsi zao
 
Faida ipo, vp ushajiuliza sababu inayotufanya tuwakumbuke waliotutangulia kwa maombi??
Mara nyingine ndugu waliotutangulia yawezekana ndiyo walikuwa mashujaa wetu; sasa kwa nn tusitembelee mahali tulipo wapumzisha?
Kutembelea makaburi siyo vibaya japo usihusishe na changamoto unazopitia.
Hata hivyo kuna relief utapata, tembelea ukafanye na usafi kabisa....
Mmmhh sawa mkuu....lkn ushujaa wake pindi alipokua duniani unakusaidia nn wewe pindi huyo aliyekuwa shujaa wakat WA uhai wake anapokua amekufa.
 
kutembelea ni muhimu japo kwakutofanya ivyo sio sababu ya kupata mikosi na wali kwakufanya ivyo sio sababu ya kuwa na ustawi maishani.MUNGU alimuumba mwanadamu na kumpa thamani na daraja la juu na hata waliolala makaburini MUNGU anawathamini pia maana ndiye aliyetoa na kutwaa. wao kuwa makaburini haina maana kuwa thamani yao ndio imeisha kabisa.
Nice one.......pia Ni wazo zur mkuu....ahsante
 
Mpe Yesu maisha no misukosuko anymore.Hachana na habari za ibada za wafu huo ni.ushetani maana unataka kujilisha upepo kwamba ukitembelea makaburi ndio misukosuko itaisha hiyo ni ibada ya wafu.
Ukiokoka tu kila kitu kitakaa sawa kwenye tatizo Yesu atakutetea na zaidi ya yote utaupata uzima wa milele.
Ameen......sawa mtumishi WA bwana
 
Sioni sababu na mimi binafsi hakuna haja.maana biblia ninayo isoma inasema "hakuna uhusiano wowote wa mfu na alie hai"

~Pia kwa swala hilo ni imani namna mtu anavyo amini,maana kwa hiyo misukosuko yakini kuna madhabahu inafanya kazi badala yako ili ww utudi kwenye maagano.km huja okoka,okoka.

~Na utumie damu ya YESU kuvunja misingi yote mibovu ambayo babu,baba zako waliiweka kwa kujua au kuto kujua na kukuambatanisha na ww.
 
Faida ipo, vp ushajiuliza sababu inayotufanya tuwakumbuke waliotutangulia kwa maombi??
Mara nyingine ndugu waliotutangulia yawezekana ndiyo walikuwa mashujaa wetu; sasa kwa nn tusitembelee mahali tulipo wapumzisha?
Kutembelea makaburi siyo vibaya japo usihusishe na changamoto unazopitia.
Hata hivyo kuna relief utapata, tembelea ukafanye na usafi kabisa....
Siamini km kweli ww ni msomaji wa biblia,sio kwa kanisani bali hata ww kitenga muda kuisoma.

~hivi ulisha wahi kusoma waebrania 9:27?na Ufunuo 20:12?mwenzetu tukwambie tu baada ya kifo ni hukumu.hakuna kutubu,hakuna kusamehewa wala hakuna neema nyingine.

~Muda ni huu na wakati ni sasa ukisha kufa huna uchanguzi.takaa unapo stahili sawasawa na matendo uliyo yatenda duniani.

~Shida ipo penye uongo tunao jifariji "eti alazwe pema peponi"hiyo pepo ni ipo?eti Mungu umuhurumie kwa lipi?"Mungu hadhiakiwi kile upandacho ndicho utakacho vuna"hakuna mahali panaposema tuwaombee wafu.

Nb:Nimaelekezo tu sijabisha maana shika sana ulicho nacho.
 
Ni muhimu sana. Hata RC tuna utaratibu wa kuwaombea misa. Ni vema ukawakumbuka bado wangali hai kiroho.
 
Kwa mtazamo wangu siamini kuhusu uwezekano wa mawasiliano kati ya walio hai na hao wapendwa wetu walio lala mauti. Kwani hao waliolala mauti hawajui lolote linaloendelea kwa walio hai. Kwa maana hiyo kutembelea au kutokutembelea makaburi yao hakuondoi au hakuwezi kukuletea mikosi yoyote.

Ninashawishika kuamini hilo kwa mfano mdogo tu kwamba kama mtu aliye hai pale anapokuwa amelala usingizi tu mzito asipoota ndoto yoyote hapati hisia zingine zozote hadi atakapoamka. Sasa iwe amekufa?!

Pia mtazamo wangu unaniaminisha kuwa kutembelea makaburi ya wapendwa wetu na pia kuyafanyia usafi si jambo baya kwa sababu kwa kufanya hivyo utakuwa ukikumbuka matendo au maneno/wosia wa hao ndugu zako waliotangulia na pengine hii inaweza kukukumbusha wajibu wako ukiwa bado ungali hai.

Kwa ujumla binafsi sioni mantiki ya kwenda majumba ya makumbusho kuangalia makaburi au mafuvu ya watu wengine wasionihusu lakini walio mashuhuri nchini/duniani, mabaki ya vitu mbali mbalimbali vilivyovumbuliwa katika nyakati tofauti (mfano old stone age) kama nashindwa walau kujenga na kutunza kaburi la babu, bibi, baba au mama yangu aliyenileta duniani ili kuweka tu kumbukumbu za kudumu kwa ajili ya kizazi changu kijacho.
 
Kutembelea makaburini, kupalilia,sio tatizo ni sawa kwa sababu ni njia mojawapo ya kukukumbusha kuwa na wewe ipo Siku utalala kama hao waliozikwa makaburini. Kama wewe ni Mkristo, ambacho hupaswi kufanya ni ibada ya kuombea au kuomba usaidizi toka kwa wafu . Hilo ni chukizo kwa MUNGU . ukifanya matambiko makaburini, unjiunganisha wewe na watoto wako katika nafsi za wafu ambao watakusumbua wewe na watoto wako. Tembekea, jengea kwa ajili ya kumbukumbu tu ,na sio vinginevyo.
 
Sisi waislam tinafundishwa hivi
.
Atakapokufa mwanadamu kila kitu chake kinatoweka isipokua mambo Matatu.

1=Sadaka yenye kudumu
2=Elimu yenye manufaa
3=Watoto wema watakaokuombea dua huko uliko

Hivi ndivyo vitakavyokua na Msaada kwako,huko kutembelea makaburi ni mbwembwe tu. Mfanyieni dua mzee wenu kumuombea kwa Mungu amhifadhi.
 
Faida ipo, vp ushajiuliza sababu inayotufanya tuwakumbuke waliotutangulia kwa maombi??
Mara nyingine ndugu waliotutangulia yawezekana ndiyo walikuwa mashujaa wetu; sasa kwa nn tusitembelee mahali tulipo wapumzisha?
Kutembelea makaburi siyo vibaya japo usihusishe na changamoto unazopitia.
Hata hivyo kuna relief utapata, tembelea ukafanye na usafi kabisa....
Unamuombeaje mfu? Hizo ni ibada za umizimu, au wafu ni MACHUKIZO KWA MUNGU,
 
Back
Top Bottom