Umewahi 'kushare' na mke au mume wa mtu, unajisikiaje ukikutana na mumewe au mkewe?

Umewahi 'kushare' na mke au mume wa mtu, unajisikiaje ukikutana na mumewe au mkewe?

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,292
Reaction score
6,768
Kwa upande wangu sijawahi kutoka na mke wa mtu isipokuwa yuko mmoja ambaye alinisumbua sana, yaani ni yeye ndiyo alikuwa ananitongoza lakini nimekuwa nikitumia siasa fulani hivi kumkatalia.

Tatizo ninalolipata ni kwamba kila nikikutana na mumewe huwa najihisi kukosa amani na uhuru. Mimi sijafanya chochote na wala sio mimi niliyemtongoza mkewe.

Hebu nije kwenu ndugu zangu ambao mmewahi kufanya hivyo.

HIVI UNAJISIKIAJE HASA UNAPOKUTANA NA MWENYE MKE AU MWENYE MUME?
 
Unapokuwa unatembea na mke wa mtu, ukikutana na mume wake tu. Nafsi yako inakuhukumu hata kabla ya kusemeshwa na mtu yeyote kuhusu suala hilo!

Inakuwa kama alarm ya moyoni inayokudai deni unalodaiwa.
 
Niliwahi kuwa na mahusiano na mke wa mtu ila siku moja nikaona kaweka mumewe kwenye status, WhatsApp. Huruma iliniijia sana maana yule msela kumbe ni shabiki wa Arsenal.

Niliona siku jamaa akijua mkewe anachepuka na hali ya timu yake anaweza kuwa kwenye hali mbaya sana.
 
Kula mke au kutembea na mume wa mtu ni dhulma na dhulma ni dhambi anyways.

Nawashangaa watu watakaoshabikia japo wengi wetu hii huwa mitihani migumu sana ku deal nayo.

Sijiviki utakatifu ila kimsimgi sijawahi kutembea na mke wa mtu na wala hilo silifikirii. Ni sawa na nilivyoweka nadhiri ya kutotembea na mwanafunzi.
 
Ni wakat mgumu

Kwanza unashtuka,halafu unajikausha fasta...kisha unapinda USO,shingo,macho degree 45...kama hujamwona kabisa

au unazugia simu,huku ukipimia uelekeo aliko asije ghafla kukuchoma na kitu chenye ncha kali
 
This is JF....mambo ya humu usiyachukulie serious, shauri yako 😂😂
Mkuu ni kweli ila mimi na akili zangu naelewa vizuri mno lakini kunawengine hawachuji mambo, mwingine anaweza katoka hapa akaenda kufanya kweli (akafikiri kucheat ni haki ya mwanaume). Kumbe sisi tumempoteza
 
Back
Top Bottom