Mvumbo
JF-Expert Member
- Aug 20, 2015
- 3,444
- 11,943
Salaam
Maisha yana mapito mengi mazuri na mabaya na pia yapo yale ambayo unaona kabisa hiki ndiyo kifo chako ila unajikuta hai tena bila kutarajia!
Binafsi nimepitia mengi na namshukuru Mungu kuniepusha, leo nitashea nanyi. Twende pamoja.
Wakati bado ni kijana wa miaka kama 20 hivi nilikwenda likizo kijijini kwa dada yangu ili kubadilisha mazingira kidogo, ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kwenda huko na wenyeji wa huko asilimia kubwa ni ndugu hivyo nilipangiwa nikalale kwa kijana wa rika langu ambae pia alikuwa mwanafunzi kipindi hicho.
Huyo mwenzangu hakuwa mtu wa matembezi kabisa muda wote ni ndani kujisomea tu hivyo nikaungana na vijana wengine ambao pia ni ndugu kwenda kuangalia video kwenye banda nyakati za usiku, ilikuwa kama saa nne kasoro hivi na kumbe muda huo wanaweka picha za ex kwa siri lakini na hii ni baada ya watoto kutoka.
Tulibaki watu wachache tu na picha likaanza ila ghafla tukashangaa mtu anakuja mbio huku akiwa na panga akajichanganya na sisi! Mara wakavamia polisi kama nane na bunduki na huku wananchi wakiita kelele ya wizi!
Hapo sote tulitoka nduki kutokana hakukuwa na usalama tena, kwa bahati mbaya wenzangu wote walipita chochoro pamoja na yule mwizi ila mimi kutokana na ugeni wangu nikakimbia njia iliyonyooka kuelekea nyumbani...ghafla nikaunganishiwa mimi na jeshi kubwa la wananchi wakiniitia mwizi wakiwa na silaha za kila aina na kunifuata speed sana!
Nilikimbia mpaka ninapolala nikamuita jamaa dirishani afungue lakini alikuwa akiitikia tu, jeshi linakuja cha kufanya sikijui ila nikapata akili ya kuingia kwenye uwa wa chooni na hakuna hata mlango nikabana huko na jeshi likapita na kusonga mbele huku wakisema huyu tumuue wenyewe asiingie mikononi mwa polisi.
Nilinusurika ila hii siku kwangu ilikuwa ni nzito sana na bado ni nzito mpaka sasa pamoja ya kuwa imeshapita miaka mingi.
Pia nilishanusurika kukatwa kichwa kipindi kile cha watu wanaouwa na kutoweka na vichwa, hapa sitaki kukumbuka pia. Na mkasa mwengine ni ule wa kuwapa watu lift kwenye gari na ghafla kamba ikarushwa kutokea siti ya nyuma waninyonge wachukue gari ikiwa bado mpya kabisa!
Namshukuru Mungu kwa yote nipo bukheri wa afya.
Iwapo na wewe yamekukuta yeyote tueleze tujifunze na kumtukuza Mungu.
Alamsiki!
Maisha yana mapito mengi mazuri na mabaya na pia yapo yale ambayo unaona kabisa hiki ndiyo kifo chako ila unajikuta hai tena bila kutarajia!
Binafsi nimepitia mengi na namshukuru Mungu kuniepusha, leo nitashea nanyi. Twende pamoja.
Wakati bado ni kijana wa miaka kama 20 hivi nilikwenda likizo kijijini kwa dada yangu ili kubadilisha mazingira kidogo, ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kwenda huko na wenyeji wa huko asilimia kubwa ni ndugu hivyo nilipangiwa nikalale kwa kijana wa rika langu ambae pia alikuwa mwanafunzi kipindi hicho.
Huyo mwenzangu hakuwa mtu wa matembezi kabisa muda wote ni ndani kujisomea tu hivyo nikaungana na vijana wengine ambao pia ni ndugu kwenda kuangalia video kwenye banda nyakati za usiku, ilikuwa kama saa nne kasoro hivi na kumbe muda huo wanaweka picha za ex kwa siri lakini na hii ni baada ya watoto kutoka.
Tulibaki watu wachache tu na picha likaanza ila ghafla tukashangaa mtu anakuja mbio huku akiwa na panga akajichanganya na sisi! Mara wakavamia polisi kama nane na bunduki na huku wananchi wakiita kelele ya wizi!
Hapo sote tulitoka nduki kutokana hakukuwa na usalama tena, kwa bahati mbaya wenzangu wote walipita chochoro pamoja na yule mwizi ila mimi kutokana na ugeni wangu nikakimbia njia iliyonyooka kuelekea nyumbani...ghafla nikaunganishiwa mimi na jeshi kubwa la wananchi wakiniitia mwizi wakiwa na silaha za kila aina na kunifuata speed sana!
Nilikimbia mpaka ninapolala nikamuita jamaa dirishani afungue lakini alikuwa akiitikia tu, jeshi linakuja cha kufanya sikijui ila nikapata akili ya kuingia kwenye uwa wa chooni na hakuna hata mlango nikabana huko na jeshi likapita na kusonga mbele huku wakisema huyu tumuue wenyewe asiingie mikononi mwa polisi.
Nilinusurika ila hii siku kwangu ilikuwa ni nzito sana na bado ni nzito mpaka sasa pamoja ya kuwa imeshapita miaka mingi.
Pia nilishanusurika kukatwa kichwa kipindi kile cha watu wanaouwa na kutoweka na vichwa, hapa sitaki kukumbuka pia. Na mkasa mwengine ni ule wa kuwapa watu lift kwenye gari na ghafla kamba ikarushwa kutokea siti ya nyuma waninyonge wachukue gari ikiwa bado mpya kabisa!
Namshukuru Mungu kwa yote nipo bukheri wa afya.
Iwapo na wewe yamekukuta yeyote tueleze tujifunze na kumtukuza Mungu.
Alamsiki!