UMEME WA DC KTK MACHINE ZITUMIAZO SOLAR/ BATTERY

UMEME WA DC KTK MACHINE ZITUMIAZO SOLAR/ BATTERY

Makini joo

Member
Joined
Mar 28, 2017
Posts
22
Reaction score
43
Kuna swala linanisumbua hapa kidogo..
KWA ANAEJUA HILI ANIFAFANULIE ILI KUOKOA GHARAMA ZA UMEME..

1. Mfano. Una Friji inayotumia umeme wa AC V240 na una friji unayotumia umeme wa DC 12V. Hii ya AC unaconnect kwenye switch ya umeme, na hii Ya DC unatumia waya wenye Adapter yake nayo una connect kwenye switch ya umeme mkubwa ili hii adaptor i convert Ac into DC.. Swali, je, matumizi ya units za umeme kwenye mita ya luku ni sawa? Kama ukiziacha hizi friji zi operate kwa same masaa 10. ?. Kama ni sawa kwa nini na kama ni tofauti kwa nini?.

2. Mfano mwingine..
Nina mashine yangu ya kutotoleshea vifaranga. (Automatic incubators) inayotumia both AC na DC. . kwa DC inabidi uweke/u-connect nyaya zake direct kwenye Battery iliyofull. Hii ni ili walau kupunguza makali ya umeme wa AC.. Swali, Je,! Adaptor ya hizi machine zinaweza patikana? Ili badala ya kutumia solar/ battery, ukatumia adapter wire ili uunganishe kwenye umeme mkubwa wa AC.. Na je, kama adaptor zipo, matumizi ya umeme yatakuwa yamepungua kwa kutumia hiyo adapter??. Karibuni sana wana jamii ktk hili.. Naomba kuwasilisha.kwa kuanzia hapo.
 
Iwe AC au DC, issue muhimu ni Wattage ya chombo unachotaka kutumia.

Adapter utakuwa unamaanisha Inverter/Rectifier/Converter?

Kama ni 120W, basi tumia DC au AC, mziki utakuwa almost ule ule ukiondoa zile tofauti ndogo ndogo za kitaalamu sana, sisi huku mtaani tuishie kujua tu, source yako au storage yako iwe tu na uwezo wa kusukuma huo mzigo na kwa muda mrefu.
 
Ok. Kwaio hapa ishu ni watt.. Kama chombo unachotumia kina tumia watt 100 kwa kutumia AC, na kama hicho chombo Kwa kutumia DC ni watt izo izo 100, means ulaji wa umeme ni ule ule... Dah. Asante
 
Wattage ya hivyo vifaa ndio inatafsiri matumizi yake. Matumizi yatafanana kama hivyo vifaa vina wattage sawa,

na ukienda ndani zaidi kitaalamu ni sawa kusema hiyo friji ya DC ambayo unatumia kwenye AC kupitia adaptor itatumia umeme zaidi kama 2% kuzidi hiyo ya direct AC, kwa sababu kuna energy loss. Power conversion inapofanyika kuna heat inazwalishwa hapo kwenye converter, hiyo heat ni loss inayoongezeka toka kwenye original power source

Kuhusu AC/DC incubator, adaptor zipo lakini kuhusu kupunguza gharama jibu ni kama nilivyoeleza hapo juu
 
Nimekupata vizuri sana.. Sasaiv inabidi nitambae na logic ya kujua kwanza wattage ya vifaa.. Ndio nifanye conclusion. Asante sana
 
Consider formula nime google kidogo.. Chukulia friji linalotumia AC. 240V with 40Amps.
Alafu tu conside friji la Dc, 12V na Watt tuchukue tutakazo zipata za kwenye Ac, je, amps ni kweli itakuwa kubwa sana ya kwenye DC compare to ya kwenye AC?. Is it possible?.
Karibu unielimishe kidogo apo
Screenshot_20220824-193211.jpg
 
Usichanganywe na neno Volt (V) ili kuelewa vizuri Volt ifanye kama pressure kweny bomba la maji. Maji yanaongezwa pressure ili yaweze kwenda mbali zaidi, Vile vile umeme unaongezwa Volt (Pressure) ili uweze kwenda/kusafiri mbali zaidi. Hii ndo sababu umeme unatoka Mkoa hadi Mkoa unaona unakua kwa HT na voltage kubwa ili uweze kufika mbali.
Unaposafirisha maji kwa umbali mrefu itafika sehemu pressure itakua hakuna kabisa na maji yatashindwa kwenda vivyo hivyo na kwa umeme. Ili uweze kuusafirisha umbali mkubwa lazima uongeze pressure na baada ya umbali flan utaweka Station ambayo itaongeza pressure (Volt) za umeme uweze kusafiri kwa kasi tena bila kuwa na Voltage drop.

HIVYO:
ikiwa kifaa kinatumia AC/DC ila Watts ni 100 tambua kwamba kifaa hicho kikiwa connected kwa umeme kwa masaa 10 bila kuzimwa kitatumia 1000Watts (1 kWh) ambayo ni sawa na unit 1 ya umeme wa luku. Volt hazina maana sana kweny upande wa consuption ila ina maana kubwa kuutoa umeme point A to B.

Ikiwa kuna sehemu hujaelewa karibu.
 
Back
Top Bottom