Umeme umekatika nchi nzima?

Umeme umekatika nchi nzima?

The Saver

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2014
Posts
204
Reaction score
751
Sasa hivi ni saa 19.58

Lakini inavyoonekana TANESCO wamekata umeme sehemu kubwa ili wananchi wasione kilichozungumzwa ubungo hasahasa alipoingia mwenyekiti wa CDM

Serikali na Tanesco wana mambo ya kizamani sana

TUNAJUA HUU UMEME UMEZIMWA MAKUSUDI HILI WATU WASIONE TAARIFA YA HABARI LAKINI SISI TULISHAJUA KUWA SIKU ZOTE SERIKALI INAPOTAKA KUWANYIMA WANANCHI HABARI INAKIMBILIA TANESCO, IKITAKA KUIBA HELA INAKIMBILIA TANESCO

JE KWEKO HUKO UMEME UPO?MIMI NIPO TEGETA
 
Duh,ni Tabu tupu hata hapa nilipo umekatika sasa hivi.. Ila no sweat,jenereta ipo tatizo Dstv nayo itaboot hadi taarifa iishe..
 
Acha uzushi mbona huku mbagara, kongowe mpaka mkuranga upo. Haya machagadomo yanatabu sana.
 
Usihofu, impact ya ripoti za magazeti ni kubwa kuliko TV. Jiandae kupate gazeti kesho na picha murua kabisa!
 
nlijua mtaani kwetu tu ndo wamekata
 
Nchi nzima? Mbona hapa kiteto upo, ten nimewasiliana na jamaa anasema matui pia umeme upo, labda we unakaa msumbiji au Zambia
 
Bavicha ni baraza lilojaa vijana wajinga na waropokaji wengi!
Mimi nimeangalia habari na umeme hupo...
 
Dar umeme upo kama kawa. Nimeangalia ITV habari mbowe hajapata nafasi ya kuongea kwa vile yeye ndo alikuwa chanzo cha huo mgomo. Alienda ubungo kuchochea. Thanks kijana Paul Makonda kwa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu
 
Bavicha ni baraza lilojaa vijana wajinga na waropokaji wengi!
Mimi nimeangalia habari na umeme hupo...
Kwani mkuu usipotukana keybord inagoma?? jaribu kutumia maneno ya staha kidogo, ujumbe utafika tu.
 
Nyie labda kwenu kuna gundu lkn Jk ameondoa tatizi la umeme na kuwa la kihistoria.
 
Back
Top Bottom