voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Waziri Byabato: "tumelazimika kuleta wakandrasi wenye gharama kubwa ili kurekebisha hitilafu kwenye mitambo ya Gesi ya Kinyerezi"
Baada ya Mvua kunyesha, wamebadili visingizio?
Bado CCM mnazidi kuhangaika na "UFISADI" tu.
Waziri Makamba alituambia Magufuli aliizeesha Mitambo,hivyo tumpe Muda airekebishe!
Akaenda mbele zaidi kwa kutuletea mkataba na kampuni ya "Mahindra" toka India.
Kwamba inarekebisha mfumo na uratibu wa utendaji wa "Tanesco" kuwa wa kisasa.
Baadae akabadili ikawa ni Uchakavu wa njia za kusafirishia Umeme!
Akaingia mkataba mwingine tena,kwamba inakuja kuboresha mitambo yoote aliyodai yeye Makamba ilichakazwa na Magufuli(R.I.P).
Baadae tena ikawa ni Ukame,ingawa aliumbuliwa na Meneja wa Bwawa la Mtera!
Pale alipotumia helikopta za Magufuli kukagua Vina vya Maji mto Ruvu na Wami.
Majuzi tena ametuambia ni Ukame nchi nzima!
Sasa Mvua zimeanza amebadili gear kwamba ni Mitambo ya Gesi ya kinyerezi?
Makamba huyohuyo anatuambia Tanesco inao uwezo wa kuzalisha Megawati 1900.
Mahitaji na Matumizi halisi ya Watanzania nchini ni Megawati 1500 pekee.
Hivyo tunayo ziada ya megawati 400.
Lakini tunayo shortage ya Megawati 2oo kutokana na Ukame!
Je! Hizi Megawati zingine 200 kati zimeenda wapi?
Kama zipo mbona hatuoni zikitumika badala yake Wizara ikihangaika na huu udanganyifu?
Hivi hili bunge letu la JMT,halina kamati ya Nishati?
Kwa nini isiende kukagua Chanzo halisi cha Tatizo?
Au kwa sababu ma-Chawa kina "Musukuma" ndio wajumbe wa kamati hiyo?
CCM mnatia aibu Sana!
CCM mnatuudhi sana!
CCM mmezeeka mpaka mmeuchoka uzee!
Sasa mnatamani kuzama na CCM yenu!
Ambayo iliokolewa na ujio wa JPM 2015.
Marehemu Rais wetu mpendwa JPM(R.I.P) aliwahi kutabiri kuhusu Umeme na Maji alisema kuwa akiondoka matatizo yatarudi kama zamani na leo hii yamerudi tena matatizo ya Umeme na Maji kwa njia ya mgao.
Utabiri wa Magufuli Unazifi Kutimia!
Baada ya Mvua kunyesha, wamebadili visingizio?
Bado CCM mnazidi kuhangaika na "UFISADI" tu.
Waziri Makamba alituambia Magufuli aliizeesha Mitambo,hivyo tumpe Muda airekebishe!
Akaenda mbele zaidi kwa kutuletea mkataba na kampuni ya "Mahindra" toka India.
Kwamba inarekebisha mfumo na uratibu wa utendaji wa "Tanesco" kuwa wa kisasa.
Baadae akabadili ikawa ni Uchakavu wa njia za kusafirishia Umeme!
Akaingia mkataba mwingine tena,kwamba inakuja kuboresha mitambo yoote aliyodai yeye Makamba ilichakazwa na Magufuli(R.I.P).
Baadae tena ikawa ni Ukame,ingawa aliumbuliwa na Meneja wa Bwawa la Mtera!
Pale alipotumia helikopta za Magufuli kukagua Vina vya Maji mto Ruvu na Wami.
Majuzi tena ametuambia ni Ukame nchi nzima!
Sasa Mvua zimeanza amebadili gear kwamba ni Mitambo ya Gesi ya kinyerezi?
Makamba huyohuyo anatuambia Tanesco inao uwezo wa kuzalisha Megawati 1900.
Mahitaji na Matumizi halisi ya Watanzania nchini ni Megawati 1500 pekee.
Hivyo tunayo ziada ya megawati 400.
Lakini tunayo shortage ya Megawati 2oo kutokana na Ukame!
Je! Hizi Megawati zingine 200 kati zimeenda wapi?
Kama zipo mbona hatuoni zikitumika badala yake Wizara ikihangaika na huu udanganyifu?
Hivi hili bunge letu la JMT,halina kamati ya Nishati?
Kwa nini isiende kukagua Chanzo halisi cha Tatizo?
Au kwa sababu ma-Chawa kina "Musukuma" ndio wajumbe wa kamati hiyo?
CCM mnatia aibu Sana!
CCM mnatuudhi sana!
CCM mmezeeka mpaka mmeuchoka uzee!
Sasa mnatamani kuzama na CCM yenu!
Ambayo iliokolewa na ujio wa JPM 2015.
Marehemu Rais wetu mpendwa JPM(R.I.P) aliwahi kutabiri kuhusu Umeme na Maji alisema kuwa akiondoka matatizo yatarudi kama zamani na leo hii yamerudi tena matatizo ya Umeme na Maji kwa njia ya mgao.
Utabiri wa Magufuli Unazifi Kutimia!