Umekata tamaa? Soma ujumbe huu utakusaidia!

Umekata tamaa? Soma ujumbe huu utakusaidia!

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,672
18485951_1372694509489457_5850822570181001878_n.jpg

Kuna vijana fulani wa mjini, wamekaa kijiweni na kuyajadili maisha kwamba ni magumu, wamekata tamaa na kudai kwamba kamwe hawawezi kufanikiwa! Wengine wanakwenda mbali na kusema kwamba wao wamezaliwa na masikini hivyo watakuwa masikini milele, labda kama wazazi wao na ndugu zao.

UNAKOSEA! Kumbuka utajiri si bahati na ndiyo maana hakuna tajiri anayetajirika kwa kulala tu ndani. Ingekuwa Mengi kapata utajiri kwa kulala tu ndani, Dewji kaupata hivyo au Bill Gates kaupata kwa kulala tu ndani, ningeamini kwamba kweli utajiri ni bahati, ila kwa kuwa walipambana, basi utajiri si bahati bali ni matokeo ya yale yote uliyoyafanya, ni matokeo ya juhudi zako na ufanyaji kazi kwa nguvu.

Mwangalie mzee huyu! Mpaka amefika umri wake, bado anaendelea kupambana! Inawezekana watoto wake wapo mjini, wanakula maisha lakini nguvu ya kupambana bado inaishi ndani yake.

Kwa muonekano, ni masikini, lakini bado hajakata tamaa, sasa kwa nini wewe ukate tamaa? Kwa nini useme kwamba utajiri ni bahati tu na ukae nyumbani? Kama mzee huyo anapambana! Kwa nini wewe usipambane? Amekuzidi nini tofauti na umri? Kwa mzee kama huyo angekaa tu nyumbani na kuweka visingizio kwamba umri umekwenda basi akae asubiri aletewe chakula, lakini cha kushangaza, bado anaendelea kupambana shambani! Una sababu gani za kutoa kusema kwamba ulishindwa kwa kuwa ulikata tamaa?

Ndugu yangu AMKA! Kuupata utajiri si lelemama tu na kamwe utajiri hauji kwa kutulia chumbani ukisoma magazeti! Upo tayari kupambana kama mzee huyu?

TWENDE KAZI!
 
Sitaki kuamini kuna kijana anayependa kukaa ndani. Tatizo kama huna mtaji utafanya nini?? Utazurura tu town? Au utaenda kushinda sokoni na watu usiowajua? Inachanganya sana hii hali bro. Kila MTU anataka good life, lakini bongo kunakasha tamaa sana. Unajua kilichowakuta wakulima was nanasi??? Bro we unaajira au ulukua na mtaji umewahi kujiajiri?
 
18485951_1372694509489457_5850822570181001878_n.jpg

Kuna vijana fulani wa mjini, wamekaa kijiweni na kuyajadili maisha kwamba ni magumu, wamekata tamaa na kudai kwamba kamwe hawawezi kufanikiwa! Wengine wanakwenda mbali na kusema kwamba wao wamezaliwa na masikini hivyo watakuwa masikini milele, labda kama wazazi wao na ndugu zao.

UNAKOSEA! Kumbuka utajiri si bahati na ndiyo maana hakuna tajiri anayetajirika kwa kulala tu ndani. Ingekuwa Mengi kapata utajiri kwa kulala tu ndani, Dewji kaupata hivyo au Bill Gates kaupata kwa kulala tu ndani, ningeamini kwamba kweli utajiri ni bahati, ila kwa kuwa walipambana, basi utajiri si bahati bali ni matokeo ya yale yote uliyoyafanya, ni matokeo ya juhudi zako na ufanyaji kazi kwa nguvu.

Mwangalie mzee huyu! Mpaka amefika umri wake, bado anaendelea kupambana! Inawezekana watoto wake wapo mjini, wanakula maisha lakini nguvu ya kupambana bado inaishi ndani yake.

Kwa muonekano, ni masikini, lakini bado hajakata tamaa, sasa kwa nini wewe ukate tamaa? Kwa nini useme kwamba utajiri ni bahati tu na ukae nyumbani? Kama mzee huyo anapambana! Kwa nini wewe usipambane? Amekuzidi nini tofauti na umri? Kwa mzee kama huyo angekaa tu nyumbani na kuweka visingizio kwamba umri umekwenda basi akae asubiri aletewe chakula, lakini cha kushangaza, bado anaendelea kupambana shambani! Una sababu gani za kutoa kusema kwamba ulishindwa kwa kuwa ulikata tamaa?

Ndugu yangu AMKA! Kuupata utajiri si lelemama tu na kamwe utajiri hauji kwa kutulia chumbani ukisoma magazeti! Upo tayari kupambana kama mzee huyu?

TWENDE KAZI!


Huyo babu anafanya nini hapo?
Hilo shamba lina mazao machanga, sijaelewa kama analima au anafanya palizi au anavuna viazi... hilo jembe amelifanyia nini hapo shambani, isije ikawa babu ametumika tu kufikisha ujumbe
 
Huyo babu anafanya nini hapo?
Hilo shamba lina mazao machanga, sijaelewa kama analima au anafanya palizi au anavuna viazi... hilo jembe amelifanyia nini hapo shambani, isije ikawa babu ametumika tu kufikisha ujumbe

Au wasamaria wamemuonea huruma wamempa kibarua cha palizi. Kwanza najisikia vibaya kumuona na umri huo bado anashika jembe LA mkono. Mambo ya kifukara kabisa. Bongo inakatisha tamaa jamani. Tujisomee vitabu tubadili mtazamo labda watawala watajua tumeamka kutoka usingizini. Lakini hii siasas
 
Kongole kwa huyo mzee
Tanzania tunapenda sana kupongezana...na hii imetapakaa serikalini...wanasiasa...
Huyu Mzee ni wa kumpa pole sio pongezi!
Kwani yote hii ni njaa na umasikini uliopitiliza,Mzee alitakiwa sasa hivi akae makao ya wazee ale vizuri apumzike,sasa shida hizi ndio zimempeleka hapo shamba,huku si ni kujimaliza?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom