Mkuu eleven ni watu wachache sana wanapata bahati ya kujua nini dhumuni lao hapa duniani, wengi wetu tunabaki kama wasindikizaji tuu.
kutoka kwa mwana pyschologist Maslow aliweka bayana madaraja ya matamanio ya mwanadamu. hilo tamanio la kujua dhumuni lako ni la mwisho kabisa baada ya kufanikiwa madaraja yafuatayo:-
kutafuta mahitaji muhimu - chakula, malazi, mavazi ,
kutafuta ulinzi na usalama- kwa maisha yako au mali zako zipo
kutafuta familia, mahusiano, kupendwa, kujumuika na uwanajamii
kutafuta mafanikio
na mwisho baada ya kupata vyote hivyo apo mtu ndo anaanza kutafuta au kutekeleza dhumuni lake hapa duniani, mfano mzee Mengi aliona dhumuni lake kusaidia watanganyika waliokuwa katika hali ngumu, Bill Gates alianzisha foundation yake ya kutatua njaa na magonjwa, na sasa Aliko Dangote amepata dhumuni lake kama kuikomhoa Afrika kiuchumi, kiifanya kujitegemea hilo ndio dhumuni lake.
sithani kama itakuwa ni jambo la busara kuanza kuangaika na dhumuni lako wakati kuna baadhi ya madaraja mambo hayapo sawa.